Umeme: TANESCO yatahadharisha kuwapo kwa mgao!

MwanaHaki

R I P
Oct 17, 2006
2,401
705
Wana-JF,

Pamoja na Waheshimiwa Wabunge kuukataa muswada wa kurekebisha sekta ya umeme nchini, ili kuleta ushindani zaidi na unafuu wa bei kwa mteja, Waheshimiwa Wabunge wameukataa muswada huo, kwa mantiki kwamba hauna manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Lakini kinachoshangaza, labda kufurahisha pia, ni kwamba, kinyume na kauli yao ya awali (hili sikumbuki kama ni TANESCO au Wizara ya Nishati waliosema) kwamba hakutakuwa na mgao wa umeme nchini kutokana na kuwapo kwa mvua za kutosha na kujaa kwa mabwawa ya kuzalishia maji ya Kidatu, Kihansi na Mtera, sasa TANESCO wanageuka na kusema kwamba - tena mapema - mgao huenda ukawapo.

Tafadhalini nendeni mkasome habari hizo hapa http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/3/20/habari3.php.

Tujadili.

(Mtazamo wangu: Kama JK ataruhusu kuwapo kwa hali hii, ambayo itawaathiri zaidi Watanzania, kwani umeme kwa sasa ni sawa na anasa kutokana na kutozwa kwa bei ya juu sana, basi, hali hii ni mojawapo ya sababu zitakazochangia yeye kutoruhusiwa kugombea tena Urais mnamo 2010... ambayo haiko mbali sana!)

Tumetahadharishwa!

./MwanaHaki
 
Kuna haja ya kuangalia mambo makubwa ya kuangalia ikibidi haya maswala yawekwe kwenye mambo ya dhalula: Kuna hatari tunakoelekea tusifike, Jk sijui anaona haya. Mkapa, Lowassa, Aziz na wengine wotwe waliosaini mikataba ya umeme itabidi tushitane masharti either wanataka hawataki.

 
Naweza kusema kuwa mgao wa umeme ukianza Tanzania tena rasmi (kwani huko mikoani mgao unaendelea kama kawa), Kikwete ataanza tena safari nje ya nchi na wala hatafanya chochote zaidi ya kutafuta karichmond kengine ..... haya ni maoni yangu tu but watch this space wana JF
 
Why are we then paying IPTL, RICHMOND, SONGAS hefty monies....still kuwepo na mgao....something is really wrong.........naanza kuuamini msemo wa Mkuu Nyani.....hivyo ndivyo tulivyo!!.....damn!
 
Why are we then paying IPTL, RICHMOND, SONGAS hefty monies....still kuwepo na mgao....something is really wrong.........naanza kuuamini msemo wa Mkuu Nyani.....hivyo ndivyo tulivyo!!.....damn!

Inawezekana serikalini huko ndio wanaendeleza na kuthibitisha msemo wa ndivyo tulivyo.... kinachoumiza zaidi ni kuwa come the election, tunawachagua hawa hawa baada ya kupewa chumvi .. kwa hiyo tena theory ya FMES kuwa viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe inakuwa proved!
 
tuna'natural gas' ambayo mwenyezi mungu ametujalia.
Kwa nini tulipishwe bei ghali?
Kwa nini tupate mgao wa umeme?
 
Najua hiyo bill imekataliwa na sio popular kwa wengi humu JF,lakini kuendelea kuipa monopoly Tanesco na kutobadilisha sheria za umeme za sasa sio solution,na umeme utendelea kutopatikana na kuwa bei mbaya kila siku....no energy=no economy!
 
tuna'natural gas' ambayo mwenyezi mungu ametujalia.
Kwa nini tulipishwe bei ghali?
Kwa nini tupate mgao wa umeme?

....sheria za sasa haziruhusu yeyote zaidi ya Tanesco kufanya biashara ya umeme,na Tanesco hawana uwezo wa kutumia hiyo gas kuzalisha umeme ndio maana wamebaki kuingia mikataba ya kitapeli kila siku,cha ajabu hawawezi kununua power plant(which is cheaper) kutumia hiyo gas kuzalisha umeme lakini wanaweza kununua bogus and expensive contracts kuliko hiyo mitambo.
 
Najua hiyo bill imekataliwa na sio popular kwa wengi humu JF,lakini kuendelea kuipa monopoly Tanesco na kutobadilisha sheria za umeme za sasa sio solution,na umeme utendelea kutopatikana na kuwa bei mbaya kila siku....no energy=no economy!

Koba,

hii bill bado haijakataliwa rasmi na kuna uwezekano mkubwa kuwa itapita tu kuruhusu makampuni binafsi kuzalisha umeme. Tatizo kubwa hapa ni kuwa ni kitu gani kifanyike kwa kina IPTL na wenzake?
 

Je mwajua hili?

Website ya TANESCO inasema 'Serikali imeamua kuibinafsisha TANESCO'
 
Naomba usome kwanza tundiko lote ndio uende kwenye hizo kurasa ulizo niuliza.

http://www.tanesco.com/reforms.html

Hapo wao wenyewe wanasema kwamba serikali iliamua kutaifisha TANESCO.

Na uthibitisho ni kwamba Serikali ilishaipa tenda kampuni ya Ki-South kushauri jinsi ya kubinafsisha na kuipanga upya TANESCO. Na hii nimeipata hapo hapo kwenye website: http://www.tanesco.com/mancontractor.html

Kama bado hawajaibinafsisha ina maana mapesa yetu ya huu mkataba yalitupwa bure. (Nielewe, sisemi wabinafsishe au wasibinafsishe).

Mwisho, ukarasa wa kwanza kabisa wa website yao unasema TANESCO ni kampuni ya Serikali. Kwa maana nyingine, hali yake ya sasa hivi hata wao wenyewe hawaielewi!

Halafu hawawezi hata kurekebisha michongo yao wenyewe iendane. Inawezekana Serikali ilishabadili mawazo na tangazo likatolewa kuhusu mwelekeo wa TANESCO lakini TANESCO wakaacha michongo za zamani ibaki hivyo hivyo kwenye website yao.


Unaona nchi yetu inavyo endeshwa?
 
Oh, {mancontractor}!

Mbona hii web ya TANESCO haifunguki kwangu? I was so interested on reading these stuffs.
 
Mimi natka kujua kitu kimoja,hivi kwa gharama hizo inazotoa Tanesco hazitoshelezi kununua mitambo yake yenyewe ya kuzalishia umeme,kuliko kuingia gharama zote hizo.naombeni msaada wenu kimawazo
 
Mimi natka kujua kitu kimoja,hivi kwa gharama hizo inazotoa Tanesco hazitoshelezi kununua mitambo yake yenyewe ya kuzalishia umeme,kuliko kuingia gharama zote hizo.naombeni msaada wenu kimawazo

Kama Tanesco ikiweza kuzalisha umeme wake kisha kina Rostam Azizi watakula wapi na richmonduli yao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…