MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Wana-JF,
Pamoja na Waheshimiwa Wabunge kuukataa muswada wa kurekebisha sekta ya umeme nchini, ili kuleta ushindani zaidi na unafuu wa bei kwa mteja, Waheshimiwa Wabunge wameukataa muswada huo, kwa mantiki kwamba hauna manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Lakini kinachoshangaza, labda kufurahisha pia, ni kwamba, kinyume na kauli yao ya awali (hili sikumbuki kama ni TANESCO au Wizara ya Nishati waliosema) kwamba hakutakuwa na mgao wa umeme nchini kutokana na kuwapo kwa mvua za kutosha na kujaa kwa mabwawa ya kuzalishia maji ya Kidatu, Kihansi na Mtera, sasa TANESCO wanageuka na kusema kwamba - tena mapema - mgao huenda ukawapo.
Tafadhalini nendeni mkasome habari hizo hapa http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/3/20/habari3.php.
(Mtazamo wangu: Kama JK ataruhusu kuwapo kwa hali hii, ambayo itawaathiri zaidi Watanzania, kwani umeme kwa sasa ni sawa na anasa kutokana na kutozwa kwa bei ya juu sana, basi, hali hii ni mojawapo ya sababu zitakazochangia yeye kutoruhusiwa kugombea tena Urais mnamo 2010... ambayo haiko mbali sana!)
Tumetahadharishwa!
./MwanaHaki
Pamoja na Waheshimiwa Wabunge kuukataa muswada wa kurekebisha sekta ya umeme nchini, ili kuleta ushindani zaidi na unafuu wa bei kwa mteja, Waheshimiwa Wabunge wameukataa muswada huo, kwa mantiki kwamba hauna manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Lakini kinachoshangaza, labda kufurahisha pia, ni kwamba, kinyume na kauli yao ya awali (hili sikumbuki kama ni TANESCO au Wizara ya Nishati waliosema) kwamba hakutakuwa na mgao wa umeme nchini kutokana na kuwapo kwa mvua za kutosha na kujaa kwa mabwawa ya kuzalishia maji ya Kidatu, Kihansi na Mtera, sasa TANESCO wanageuka na kusema kwamba - tena mapema - mgao huenda ukawapo.
Tafadhalini nendeni mkasome habari hizo hapa http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/3/20/habari3.php.
Tujadili.SHIRIKA la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) limeonya kutokea kwa mgawo wa umeme kutokana na kutokuwapo kwa mvua za kutosha pamoja na kuhitaji sh trilioni 1.6 kwa ajili ya kujiimarisha kiuchumi.
Hivyo, shirika hilo limeiomba serikali kutoa fedha mapema, ili kuweza kununua mtambo wa kuzalisha umeme wa IPTL ambao utabadilishwa mfumo wa kutumia mafuta hadi gesi, ili taifa liweze kukabiliana na tatizo la mgawo wa umeme.
Akiwasilisha mada kuhusu mpango wa TANESCO kujikwamua kiuchumi katika semina ya wabunge kuhusu miswada ya sheria za umeme na biashara ya mafuta, Mkurugenzi wa TANESCO, Dk. Idris Rashid, alisema tatizo kubwa linalowakabili ni kutokuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha, hali inayowalazimisha kununua umeme kutoka katika kampuni mbalimbali binafsi.
Alisema hivi sasa wanafanya mipango ya kununua baadhi ya hisa katika kampuni ya kuzalisha umeme wa gesi ya Songas, ili waweze kupunguza gharama za uzalishaji.
Alisema endapo watafanikiwa katika mpango huo dhidi ya Songas watakuwa wakiokoa kiasi cha sh bilioni moja kwa mwezi, fedha ambazo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kufikisha umeme maeneo ya vijijini.
Tuna tatizo kubwa la uzalishaji wa umeme, lakini pia kuna uwezekano wa mwakani kukawa na mgawo wa umeme hivyo tunaiomba serikali itusaidie kutupa fedha, ili tuweze kuinunua IPTL, alisema Dk. Idris.
Katika hatua nyingine, Dk. Idris alisema menejimenti iliyoondoka ya Net Group Solution kwa kiasi kikubwa ilisaidia kupunguza hasara iliyokuwa ikiipatia shirika hilo.
Kusema ukweli menejimenti ile kwa kiasi kikubwa imetusaidia kupunguza kupata hasara, kwani tangu waje hasara imekuwa ndogo zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali, alisema Dk. Idris.
Aidha, alisema kukamilika kwa mradi wa kuzalisha umeme wa makaa ya mawe wa Kiwira ambao unategemewa kutoa megawati 200 utakuwa mkombozi wa tatizo la umeme.
Alisema Tanzania ina vyanzo vingi vya kuzalisha umeme, lakini havitumiki ipasavyo, jambo ambalo linakwamisha juhudi za TANESCO kuwapatia umeme watu wengi zaidi.
Alisema mpaka hivi sasa ni asilimia 10 tu ya Watanzania Bara wanaotumia huduma hiyo huku wale Zanzibar wakipata umeme kwa asilimia 98.
Tunajipanga kuhakikisha wananchi wa bara nao wanapata umeme kwa idadi kubwa kama ilivyo kwa watu wa visiwani, lakini hali hii haitawezekana kama hatutapata fedha, alisema Idris.
Aidha, alisema kama fedha zilizoombwa hazitatolewa kwa wakati kuna hatari ya migodi ya Buzwagi na mingineyo kutopata umeme kwa kiasi kinachohitajika.
Alisema TANESCO mwaka jana imeongeza wateja hadi kufikia 32,000 na imepanga kuwa kila mwaka kuongeza wateja 100,000 sambamba na kwamba ifikapo mwaka 2012 ianze kuuza umeme katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Awali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema serikali itaendelea kuisaidia TANESCO, ili iimarike kiutendaji na kibiashara na ijiendeshe bila ya kuitegemea serikali.
Alisema kuna mpango wa kuliwezesha Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) lifanye biashara ya mafuta, ili kutathmini na kuisawazisha (checks and balances) biashara hiyo nchini inayofanywa pia na mashirika na makampuni mengine.
Waziri Mkuu Pinda alisema katika kuiimarisha TANESCO serikali pia inaazimia kuondoa ukiritimba wa shirika hilo.
Kuhusu TPDC, alisema shirika hilo litasaidia kuifanya serikali itathmini na kuiweka sawa biashara ya mafuta kwa sababu ni rahisi kupitia hesabu za shirika hilo na kuweza kubaini udanganyifu wowote katika biashara hiyo.
(Mtazamo wangu: Kama JK ataruhusu kuwapo kwa hali hii, ambayo itawaathiri zaidi Watanzania, kwani umeme kwa sasa ni sawa na anasa kutokana na kutozwa kwa bei ya juu sana, basi, hali hii ni mojawapo ya sababu zitakazochangia yeye kutoruhusiwa kugombea tena Urais mnamo 2010... ambayo haiko mbali sana!)
Tumetahadharishwa!
./MwanaHaki