Umegundua nini kwenye picha hii ya mwenge?

Umegundua nini kwenye picha hii ya mwenge?

mpayukaji

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2010
Posts
940
Reaction score
349
DSC_0115.JPG
 
Hata "Wakoloni" Waingereza won't, can't, and will never relate kwa kweli achilia mbali "Wapigania Uhuru".

For whatever sick reason, miaka 50 down the line, TANU aka CCM bado wamo tu na mbio za "Mwenge wa uhuru"? Bwahahaaa!
 
Jukwaa hili ni la magreat thinker sasa mbona unatudumaza akili zetu hapa? Kuwa makini ndugu yangu. Sioni issue hapo zaidi ya watu kula pesa za walipa kodi.
 
Kama hujagundua kitu nyamaza tu:
Mimi naona kuwa Mwenge unapokelewa na watu wachache sasa siku hizi yaani picha inaonyesha kuna Wakimbiza Mwenge kitaifa, Viongozi wa Serikali na Maaskari. Wananchi wengine siwaoni au niseme ni wachache.
 
Bado kitendawili hakijateguliwa kwani nilichotaka kigunduliwe hakijagunduliwa.
 
Inaonekana sasa ujumbe wa Mwenge ni kwa sisi wana CCM na Maaskari wetu.
 
nimegundua mwenge umebaki na watu nane tu nchi hii kama picha inavyoonyesha,tofauti na zamani mwenge ulikuwa ukipita maduka na mitaa inafungwa kwa umati wa watu.
 
mwenge ni mali ya ccm thats why huyo alie vaaa kijani anaukabidhi or kupokea.

mwenge umekua ni mali ya CCM tokea enzi hizo...hukumbuki harakati za kukimbiza mwenge zilikuwa zinaratibiwa kwa kiasi kikubwa na vijana wa CCM na chipukizi?
 
me naona tu moto unawaka bac. au mnataka tena kutuambia ni alama ya freemason?? maana hamchelewi. cku hizi hata ndizi ni alama ya freemason.
 
mwenge ni mali ya ccm thats why huyo alie vaaa kijani anaukabidhi or kupokea.

Hapana sio mali ya CCM, ni mali ya Watanzania. Ila wenye imani nao na wanaopaswa kuendeleza imani hiyo ni Chama tawala chochote kile. Lakini kabla hatujaanza kuhoji uhalali wa Mwenge inabidi tufahamu malengo ambayo mwenge huo ulianzishwa kutekeleza. Je, yalishatimia ? Kama lengo lilikuwa kuhimiza umoja na kuwakumbusha Watanzania kuhusu umuhimu wa uhuru na umoja wao, lengo hilo limeishatimia ? mbona bado watanzania wanaendelea kuzaliwa, hivyo wanapaswa kuendelea kuona hiyo kitu na kuelezwa maana yake.
 
Sitaki kukumbuka habari za mwenge kabisa,wakati nnasoma shule ya msingi tuliwahi kuchangishwa sana fedha kwa ajili ya mwenge.Mwenge hauna faida yoyote ni genge la wahuni ktk kutafuna fedha za walipa kodi bila sababu ya msingi.Gharama za kuutembeza mwenge ni kbwa wakati watu vijijini hawana maji/wanafuzi wanasomea chini ya miembe nk.
 
Mi nakumbuka mwaka 1995 ulitukutuka tukiwa safarini kutoka Kilimanjaro tunaelekea Arusha, ndo ulikuwa unakabidhiwa Mkoani Arusha jamaa walipoona hakuna watu wakushangilia mwenge (kumbuka kipindi hicho ndio Mrema amepamba moto na NCCR-Mageuzi yake) Askari wakaja kutuamuru tushuke kwenye mabasi kwenda kushangilia mwenge hatkuwa na namna ilibidi tushuke kwenda kushangilia japo kizushi. Hapa USA hakuna upuuzi kama huo pia nimezunguka nchi nyingi sioni upuuzi wa mwenge kama TZ. Sijui sisi tulipata wapi hili wazo. In short mimi nakubaliana na wana jamvi kuwa MBIO ZA MWENGE ni chaka zuri la kutafuna pesa.kuanzia pale wizara ya vijana, wakimbiza mwenge, halmashauri/wilayani na mashuleni (mwl. mkuu anapiga mkwara kwa walimu na wanafunzi kuchangia mwenge lakini mwishoni hatuambiwi makusanyo yalikuwa ngapi, na matumizi yake yalikuaje?) CAG mulika huko utakuta madudu!
 
Hapana sio mali ya CCM, ni mali ya Watanzania. Ila wenye imani nao ni Chama tawala. Lakini kabla hatujaanza kuhoji uhalali wa Mwenge inabidi tufahamu malengo ambayo mwenge huo ulianzishwa kutekeleza. Je, yalishatimia. Kama lengo lilikuwa kuhimiza umoja na kuwakumbusho Watanzania kuhusu uhuru wao, lengo hilo limeishatimia, mbona bado watanzania wanaendelea kuzaliwa, hivyo wanapaswa kuona hiyo kitu na kuelezwa maana yake ?
Dhana ya mwenge ilikuwa ni nzuri sana wakati inaanzishwa na sioni chama ambacho kitauondoa mwenge wa uhuru. Kati ya alama za taifa hili ni pamoja na mwenge wa uhuru. Nyerere alipowasha mwenge wa uhuru alisema" Sisi tunaka kuwasha mwenge, na kuuweka juu ya mlima wa kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo kuna uchuki na heshima ambapo pamejaa dharau" Maneno haya hayana chama wala hayamubagui mtanzania yeyote.

Ninakumbuka ulipofikishwa katika kijiji chetu uluzindua barabara iliyojengwa kwa nguvu za wananchi yenye urefu wa zaidi ya 30 km. Watu walijitolea weneyewe na hakuna cha serikali kutoa hata mfuko mmoja wa sementi. Ninakumbuka eneo letu lilikuwa kati ya maeneo duni katika wilaya Muleba na mkoa wangu wa Kagera. Mwenge huo uliondoka na dharau na ulikuwepo mwanzo mpya. Bahati mbaya CCM waliutumia vibaya. Watu wanachangia fedha nyingi na kuwakabidhi wakimbiza mwenge. Hakuna taarifa ya fedha wala wakaguzi wa fungu hilo. Mwenge unazindua miundo mbinu ilijengwa chini ya kiwango na hakuna hata ukemeaji. Zamani haikuwa hivyo bwana. Kila mwenge ukpita mahali ilikuwa ni lazima uondoke na kiongozi mbaya. Wananchi walilijua hilo. Siku ya mwenge ilikuwa ni siku ya ukombozi.

Nina imani CHADEMA kitakapo ingia madarakani kinatakiwa kuutumia kumulika mafisadi, wazembe na wezi wa mali za umma. Itautumia kuleta matumaini mahali ambapo pana chuki na heshima mahali palipojaa dharau.
Mwenge ni chombo cha kuhamasisha, ni chumbo cha itikadi. Kati ya maneno muhimu niliyo yatumia hapo ni "CHOMBO" MATUMAINI na HESHIMA dhidi ya dharau na chuki.
 
Back
Top Bottom