Duu, mbona haya mambo yanajirudiarudia katika mashule mengi ya sekondari? Nakumbuka tatizo la udini liliwahi kutokea miaka ya 2002 pale Minaki Sekondari-Kisarawe na sababu zilizotolewa mojawapo ilikuwa "Kwanini kila mara viongozi wengi wa wanafunzi ni wa kristu?" Pili- eti Kitimoto kilipikwa kwenye masufuria ya chakula cha jumuia, binafsi sikukubaliana kwani wapishi walikuwa waislaam, Na wakagoma kula chakula cha shule kwa wiki, ila kila jioni kulikuwa na Maprado yanawaletea misosi na kupikia msikitini mwisho kukawana fujo.
Imetokea maeneo mengi ya shule ila hamna suluhisho la kudumu na siasa zinaingilia, hadi UDOM pia, je ujinga huu unatupeleka wapi? Inakera sana.
Suluhisho: kwa kila sehemu watafute nini chanzo kwa haki na wakidhibiti kwa kutoa mapendekezo sahihi ya kukoma tabia hii,