Kuntakinte
JF-Expert Member
- May 26, 2007
- 701
- 31
MBEA UMEMTOKA DK.SLAA
Pamoja na kutaka kuwapotosha Watanzania kuwa fedha zilizochotwa isivyo halali na makampuni 22 kutoka mfuko wa madeni ya nje (EPA) katika benki kuu ya Tanzania (BoT) ni za serikali, mbunge wa karatu mkoani manyara (CHADEMA) Dr. Wilbroad Peter Slaa wiki hii ameumbuka katika mkutano wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania unaoendelea mjini Dodoma.
Dr. Slaa mwanasiasa alieukimbia upadri wa kanisa katoliki aliumbuliwa bungeni na waziri wa fedha, MUSTAFA HAID MKULO aliyesisitiza kuwa kauli yake kuhusu fedha hizo kwamba sio za serikali iko palepale na ndio inayosema ukweli.
Mbunge huyo wa karatu ambaye pia ni katibu mkuu wa chadema aliumbuliwa pia na mbunge wa mtera mkoani Dodoma (CCM) mzee John Samuel Malecela kuhusu ni nani hasa aliyeanzisha hoja inayohusu fedha hizo bungeni kati ya Dr. Slaa na wabunge wa chama cha mapinduzi.
Kimsingi hoja hiyo ilianzishwa na mbunge wa Busega mkoani Mwanza (CCM) Dr. Rafael Masunga Chengeni na Kudakwa kichwa kichwa na Dr. Slaa akidhani ingemsaidia kisiasa au chama chake, lakini mambo yanazidi kwenda ndivyo sivyo.
Namshauri Dr. Slaa aachane na Umbeya afanye siasa za kweli kama wanavyofanya wenzake akiwemo mwenyekiti wa taifa wa UDP John Momose Cheyo ambaye ni mbunge wa Bariadi Mashariki mkoani Shinyanga.
Akionyesha kutokua mnafiki Cheyo ndiye mbunge pekee kutoka kambi ya upinzani aliyeunga mkono bajeti ya serikali ya mwaka 2008/2009 na kutoa ufafanuzi yakinifu kuhusu msimamo wake huo usioyumba na hata kuyumbishwa na wanasiasa Ucheara kama Dr. Slaa.
Pamoja na mambo mengine, Cheyo alisema ameiunga mkono bajeti hiyo kutokana na ukaweli kwamba serikali ya CCM imeonyesha usikivu mkubwa, inashurika na inajitahidi kufanya marekebisho takribabani kila iliporuhusiwa vinginevyo na kamati ya bunge ya hesabu za serikali ambayo mbunge huyo wa bariadi mashariki ndiye mwenyekiti wake.
Hakika Dr. Slaa hatimaye Umbea umemtoka na kama ni mtu wa kujifunza basi amepata fundisho litakalomsaidia huko mbele.
Mkubwa Umekosa Shabahaaaa!
Kwanini haya hamkuyasema kabla Dk. Slaa kumwaga mambo hadharani? Na nikiangalia hata kwa uwingi wa post zako unaonekana kabisa umekuja hapa kutetea yale uliyoajiriwa kuyafanya lakini naomba tu nikwambie hii ni JF na kama wamekutuma waambie kabisa kwamba JF HAIFUNGAMANI NA UPANDE WOWOTE, ILA KIKUBWA ZAIDI NI JUU YA MASLAHI YA TAIFA TU.
Mungu Ibariki TANZANIA
Mungu Ibariki JAMII FORUM