Dada mleta mada,pole sana kwa yanayokusibu,ila katika kupita magumu yote ulichokosea ni kumtukana Mungu,omba Toba,na Mungu wa rehema atakusamehe...Nyakati ngumu zipo kwa kila binadamu ila huwa zinapita,unapita nyakati ngumu ili uwe bora,Mimi niliwahi pita nyakati ngumu sana nilipauka,nilikonda ila zilipita na zimenifanya imara zaidi,Usikate tamaa hivyo mdogo wangu,kikubwa acha kufuatilia page ya huyo tiktoker yaani wapotezee wote...Mungu akusaidie kupona nafsi yako