Hahaha hapana sio Mafinga, japo Mafinga nina historia nayo nzuri!
Kuna bidada mmoja enzi hizo nipo Njombe nilikuwa nadate naye! Unaambiwa bi dada alikuwa ananielewa kichizi, alinipenda Ile kinoma noma! Alikuwa haambiwi kitu kuhusu Mimi! Aliamini Mimi ndio Alfa na omega wake kwenye Dunia hii!
Huku na huku Mzee nikaingia tamaa kwa mlimbwende mwingine! Nikashindwa kumiliki injini Moja, ikanilazimu nichague chombo Moja niishi nayo! Si nikaacha mbachao kwa msala upitao! Nikampiga chini bi dada, sio kiupole nikamtolea shit kibao! Nikamchana makavu live unaambiwa madhaifu yake ikawa ndio mjeledi wa kumtwangia! Alilia Sana! Mtoto alinibembeleza Sana, anakuja home usiku labda nitamsamehe ila wapi, Hadi akapoteza Nuru, akawa dhoofu! Akawa mbaya Hadi mwishoni akakubali kisicho ridhiki hakiliki!
Sasa si nikachaguliwaga kwenda KJ 841 hapo Mafinga! Kwa mujibu wa Sheria hiyo! Siku ya siku nikaingia kambini doso likaanza! Kuna vikosi vya jeshi halafu Kuna Mafinga, unaambiwa Yale sio mateso, nilijitahidi kula shumbwela lakini wapi!!!
Muda wa kulala saa saba, halafu kuamka saa tisa kwenda kwenye mbio! Hapo sijui unakuwa umelala kitu gani maana sio usingizi aisee! Kurudi saa kumi na mbili tunaitwa majina, tunamwagilia maua halafu tunaenda kupiga kwata! Hapo Hadi saa nne tunaenda kunywa chai! Tukinywa chai tunaenda sehemu inaitwa mlima Nguruwe kuchukua tofali Moja Moja Kila mtu! Oyaaaah sio poa huo mlima Nguruwe ni mbali kinoma! Yaani hiyo kurudi ni saa nane au saa tisa! Tunapiga chakula Cha mchana! Halafu tunaenda kukimbia mbio Tena!
Tukitoka kwenye mbio tunakula chakula Cha usiku... Tunaenda Kuimba nyimbo za chenja Hadi saa Saba usiku tunaenda kulala! Saa tisa tunaamshwa halafu ratiba inajirudia! Hiyo ni Kila siku! Unaambiwa nilikonda, lile baridi nikawa mweusi kama oili chafu, Mzee nilikongoroka sio poa!
Siku ya siku tukapewa ruhusa twende Mafinga mjini tukaoshe macho! Safi Sana nikaoga chap, nikavaa nguo zangu... Hahahahah nguo nilizoenda nazo zinapwaya kama sio zangu, nikaazima mkanda nifunga fresh huyo nikaingia town! Hapo nimepiga kipara Cha kufa mtu na vipe Nina kakichwa kadogo nimekuwa kama charlie Chaplin.
Nikawa nazura town fresh... Ghafla ndinga inapaki kando yangu... Escudo Moja matata mpyaaaaa! Mlango unafunguliwa anashuka bi dada! Otea nani!!!!
Yule yule niliyemfanyia Violence miksa harassment pale Njombe mjini! Eeeh bwana eeeh Kawa mtu aisee! Bi dada anawaka Tena siku hizi anajua kuoga weeeh ni hatari yaani bi dada amejipata halafu Mimi Bado najitafuta na dalili zinaonyesha nishapoteana! Sijui tako kalipatia wapi, mihips hiyooo, ziwa hiloooo kudadeki.... Tumbo flatiiiiiiii.... Kavaa miwani mikubwa mwenyewe Hilo wigi mzeee yaani mtoto anaonekana kabisa shida sio mambo yake!
Ubaridi ukanipiga pale, nikawa nimeganda tu! Mtoto akasogea huku anatabasamu, "Vipi Dawa yenu... jamani za masiku"
Ikabidi nitoe tabasamu la aibu pale, "salama tu... Aiseee kitambo Sana... Kumbe upo huku?"
"Jamaniiiii Dawa yenu hata siamini... Kweli milima haikutani" akasema huku ananipa mkono...
"Aaah... Nipo bwana.... Si unajua maisha... Hahahah... Nipo jeshini hapo jeshi la JKT nafanya vitu vyangu" ilibidi nitoe kauli hiyo Ili asione kama vile nimepoteana saaaaana ... Yaani hiyo nilitaka aone mambo yangu sio mabaya!
"Ooh... Mimi nipo huku naishi na anti yangu namsaidia biashara zake za mbao mwaka wa nne huu"
Bi dada alichangamka Sana na bahati nzuri hakukumbusha kabisa ule ubumunda na ututusa wa harassment za mjini Njombe. Ni kama vile alisahau kabisa au aliamua kupotezea maana hali ya afya yangu ilionyesha nahitaji upendo, ukarimu na sio kuhukumiwa kwa mambo yaliyopita ambayo Si ndwele kwa kweli!
Mwishowe tuliingia kwenye gari lake, akanipeleka kwake! Alikuwa amepanga! Kwa kweli ilikuwa siku nzuri... Alipika ugali na nyama choma, hayo makachumbari, mapilipili, mtindi wa Assas kwa kweli japo lengo lilikuwa nirudi kambini siku hiyo hiyo ila nilishindwa ilibidi tu nilale pale pale!
Usiku nilioga maji moto hahahaha maisha haya kudadeki... Mishale ya saa Saba tulikuwa kitandani tukikumbushia Ile michezo tulifanyaga Njombe Tena time hii wote tupo na experience.... Show ilipigwa pale, dadeki.. nilianza vibaya unajua ugwadu unaambiwa zile romance, kunyonyana hapa na pale, huku na kule... Na Mimi nikawa nafight Sasa mmmmh kwenye kuingiza Ile kugusisha tu wazungu Hawa hapa! Sio kosa langu! Kurutu ni mdudu hizo nguvu ningetoa wapi?
Ngoma haikusimama Tena na tulilala hivyo yaani! Alinielewa nilimpa fact za kushato! Akanionea huruma pale tukalala! Kesho Yale nilishinda pale na baada ya chai tu mechi ilipigwa sawa sawia... Nilimla nikamla nikamtafuna nikampa vitu heavy... Najua Kuna vitu siwezi ila kumbato najua aisee! Hata mkisema najisifu ila ukweli naujua Mimi!
Jioni ya siku hiyo nilirudi kambini... Nilirudi kwa mguu Ili nipite porini nitokee tu hangani Ili mambo yasiwe mengi! Sasa karibia nafika nikakutana na wajeda wawili wanavuta bangi! Aisee nikacheza akili fasta ikabidi niwahonge vipande vya fedha! Nikawapa 10k wakanipeleka Hadi hangani (bweninj) nikavaa gwanda then hiyooo kukimbia mimbio ya hovyo!