MARA YA KWANZA KUJILIA LISHANGAZI
Nimeona na mimi leo nitie baraka kwenye huu uzi kwa kuweka japo kisa kimoja kilichonifundisha mchezo mbaya wa kula mijishangazi ya hapa town.
Story inaanzia mitaa ya Kurasini miaka ya 2013/2014 baada ya mwenye nyumba niliyokuwa nimepanga kuvuta kitita chake cha fidia ya Bomoa bomoa kupisha upanuzi wa Bandari akatuita kikao wapangaji na kutuchana kuwa kifuatacho ITV nyumba inakuja kupigwa chini kwahiyo kila mpangaji atafute usawa wa kuelekea kupisha zoezi hilo na kuturudishia kodi zetu za miezi iliyokuwa imebakia.
Katika kutafuta uelekeo nikaona bora nizame mitaa ya Mtoni kijichi maana pande za kwa Azizi Ally na Mtongani sikuzielewa wala nini.
Huku na huku nikajikuta nimepata ghetto pande za kijichi kama unaelekea Mbagala kuu kuna kituo cha daladala kinaitwa Upendo. Mara paap napata ghetto kwenye "Bangaroo" moja hivi lina vyumba kama kumi hivi huku wapangaji wengi wakiwa Single Mother, Masela kama watatu hivi mimi nikiwa mmoja wao na jamaa mmoja hivi alikuwa anaishi na familia yake.
Picha linaanza jina la nyumba lenyewe linajulikana kama "JUMBA LA MAUAJI" jina lilinitisha kidogo hivi ila kuuliza wenyeji wanakwambia TBT hilo jumba lilikuwa Guest House. Nikasema sio kesi acha wazinzi tufanye maisha.
Sasa kwenye hilo jumba kuna lishangazi moja hivi likawa linaleta ukarimu sana lakini nilikuwa sina hata wazo nalo nikaona ni kawaida tu labda kwavile mimi ni mteja wake maana alikuwa akiuza maandazi. Yaani nikiweka oda ya maandazi alikuwa hanifungii kwenye gazeti kama wateja wengine lazima aniwekee kwenye sahani ya udongo mixer na kunifunikia na wakati mwingine alikuwa analeta mpaka ghetto.
Siku moja nikiwa napiga mishe zangu kwenye PC nikiwa nimechomeka moderm ya vodacom enzi hizo kuna kifurushi cha WAJANJA NIGHT naendelea kuserereka mtandaoni nikaona friend request FB bila ajizi kwakuwa nimeona jina la demu bila kuhangaika kuangalia sura nikajikuta nimekubali ile request. Kilichofuata naona text ya fb imeingia naanza kuulizwa "Hujalala tu".
Macho ya udadisi yakaanza kutaka kujua huyu ni nani tena ananiuliza hivi mida hii na jina lenyewe hata simfahamu. Kupitia profile nikaona picha za lile lishangazi maana nilikuwa sijui jina lake kwakuwa alikuwa akiitwa mtaani kwa jina la mtoto wake. Nikamjibu tu kuwa nipo macho naangalia Dunia inavyokwenda, basi zikaanza chatting pale kumuuliza mbona na yeye hajalala mpaka muda huo akaniambia anajihisi upweke tu anatamani hata angekuwa na mume mida hii ambayo hana usingizi angekuwa anafanya majukumu ya wanandoa.
Basi Jemedari nikaona taa ya kijani imewaka ni mimi tu kukanyaga mafuta gari iende mbele. Nikachombeza nakuja tufanya hayo majukumu maana hata mimi sina usingizi akaniambia karibu. Nikajikuta tu shetani ananiambia leo nenda ukajaribu dhambi mpya ya kujilia lishangazi.
Nikajikuta tu naanza kuapply mbinu za kimedani kunyatia tunda la lishangazi, ilikuwa ni Combination ya mwendo wa pole na skills za night attack kuhakikisha hakuna kishindo adui anaweza kusikia katika harakati za kwenda kujaribu dhambi mpya.
Kiukweli kuanzia usiku ule nikajikuta nimepata kipozeo cha dharura na kutumbukia katika uraibu wa kula mashangazi mpaka leo hii.
Mpaka nahama kwenye Jumba la Mauaji nilifanikiwa kutafuta wapangaji wenzangu watatu. Hii imenipelekea kuwa na desturi ya kila ninapohamia lazima nimege jirani ndiyo maisha mengine yaendelee.
Nawasilisha.
Sent from my TECNO KC6 using
JamiiForums mobile app