Uliponiambia kuwa hawezi kazi niliamini lakini sikujua kuwa hawezi kwa kiwango hiki!

Hapa mzee umegusa penyewe kabisa, mimi nilikuwa nagombana na makatibu wa CCM wa kata yangu kwa kuwaambia kuwa mtu waliyeweka agombee alikuwa kimeo kama siyo kimeta.
 
TIP:
this is forum, usionyese ufundi wa kuandika, hapa mtu akifungua post anataka aone point moja kwa moja, be STRAIGHT, mtu hawezi kufatilia para hadi ya tatu bado kabla ya kuelewa point yako
Wewe nani alikuambia haya yote? Kama huwezi kufuatilia ukalale au ukaandamane kuwaunga mkono CCM kujivua magamba.
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana...wakati wakimteua hiyo 2005,nakumbuka tulibishana sana na rafiiki yangu mmoja,nikamwambia MOYO WANGU NI MZITO SANA KAMA HUYU JAMAA ANAWEZA..sababu: nikamwambia naona kama vyombo vya habari vinatumia nguvu nyingi mno kumtangaza,methali isemayo chema chajiuza,kibaya..inagonga mara kwa mara kichwani mwangu....tukajaribu kutathmini nini jamaa amekifanya cha kumfanya akiweze kiti kikubwa hicho,tukatapatapa huku na kule-wapi!ubaya ni kuwa rafiki yangu alikuwa tayari ameshaleweshwa na vyombo vya habari-hatukufanikiwa!...umenikumbusha tena kuwa ile Octoba watu walipoenda Diamond,nilikuwa department moja pale UDSM ambapo vijana wengi walipewa t-shirts na kofia,nilkuwa mmoja kati ya watu tuliopinga sana 'kutumika kwa vijana wasomi kwa kiasi hicho,lakini kilichotokea,sikukiamini hadi leo-maana walikuwepo watu nawamini sana katika uwezo wa kuhoji na kuchambua maamuzi-walikuwepo kwenye mkumbo ule wa kwenda Diamond bila kuhoji kama tulivyowazoea. Wachache tuliobaki na kukataa kile kitu tulionekana watu fulani mataahira!(nashukuru leo hii tunajivunia maamuzi yetu).
Nafikiri tuendelee kutafakari na kuchukua hatua..historia imetuhukumu..ni funzo kubwa..muda mwingine labda makosa haya hayatarudiwa...
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana...wakati wakimteua hiyo 2005,nakumbuka tulibishana sana na rafiiki yangu mmoja,nikamwambia MOYO WANGU NI MZITO SANA KAMA HUYU JAMAA ANAWEZA..sababu: nikamwambia naona kama vyombo vya habari vinatumia nguvu nyingi mno kumtangaza,methali isemayo chema chajiuza,kibaya..inagonga mara kwa mara kichwani mwangu....tukajaribu kutathmini nini jamaa amekifanya cha kumfanya akiweze kiti kikubwa hicho,tukatapatapa huku na kule-wapi!ubaya ni kuwa rafiki yangu alikuwa tayari ameshaleweshwa na vyombo vya habari-hatukufanikiwa!...umenikumbusha tena kuwa ile Octoba watu walipoenda Diamond,nilikuwa department moja pale UDSM ambapo vijana wengi walipewa t-shirts na kofia,nilkuwa mmoja kati ya watu tuliopinga sana 'kutumika kwa vijana wasomi kwa kiasi hicho,lakini kilichotokea,sikukiamini hadi leo-maana walikuwepo watu nawamini sana katika uwezo wa kuhoji na kuchambua maamuzi-walikuwepo kwenye mkumbo ule wa kwenda Diamond bila kuhoji kama tulivyowazoea. Wachache tuliobaki na kukataa kile kitu tulionekana watu fulani mataahira!(nashukuru leo hii tunajivunia maamuzi yetu).
Nafikiri tuendelee kutafakari na kuchukua hatua..historia imetuhukumu..ni funzo kubwa..muda mwingine labda makosa haya hayatarudiwa...

Hakika hili liwe fundisho kubwa kwetu na tusirudie makosa.
 
Mimi nilijua tu kuwa hawezi. Baada ya kuwa nimewahi kukaa naye maraka kadhaa vikaoni wakati akiwa bado anafukuzia wasichana kule Sinza nilijua kuwa jamaa yule alikuwa ni sifuri kabisa kichwani. Sikutegemea kuwa angeweza kuwa hata waziri ila nikashangaa kuwa aliwahi kutuwakilisha kama diplomat mkuu wa nchi kwa miaka kumi kabla hajawa mfalme wetu. Kwa jumla ya miaka 20, yeye ndiye anakuwa image ya watanzania nje ya nchi; yaani wababaishaji wasiojua kuchambua mambo kwa kina!!
 
Mimi nilijua tu kuwa hawezi. Baada ya kuwa nimewahi kukaa naye maraka kadhaa vikaoni wakati akiwa bado anafukuzia wasichana kule Sinza nilijua kuwa jamaa yule alikuwa ni sifuri kabisa kichwani. Sikutegemea kuwa angeweza kuwa hata waziri ila nikashangaa kuwa aliwahi kutuwakilisha kama diplomat mkuu wa nchi kwa miaka kumi kabla hajawa mfalme wetu. Kwa jumla ya miaka 20, yeye ndiye anakuwa image ya watanzania nje ya nchi; yaani wababaishaji wasiojua kuchambua mambo kwa kina!!

Hilo nalo ukifikiria unaweza ukauma meno! Kilaza namna hiyo anatuwakilisha
nje ya nchi kwa miaka 10 alahaulaaah!
 
Nikikumbuka inauma sana ijapokuwa hakuambulia kura yangu lakani the way vijana wa rika langu kipindi hicho walivyokuwa wakimshabikia kwa kweli nilinyongonyea kwa kuona Tanzania yetu ikidumbukia shimoni pasipo kuwa na msaada wowote.
Nakumbuka huyu jamaa kipindi hicho alikuwa na kashfa tayari ya IPTL, sikupata picha akipewa madaraka makubwa kama haya atafanya ufisadi kiasi gani lakini leo kila kitu kipo wazi. Nakumbuka siku jina lake linapitishwa dodoma ilikuwa ni jioni nikiwa na collegues ofisini tukipiga simu kwa jamaa zetu waliopo dodoma kutueleza kinachoendelea. Taarifa ilivyokuja kuwa amepitishwa niliugua ghafla na wiki nzima sikuwa kwenye mood ya kufanya kazi. Sio siri ni vibaya kumuombea mtu kifo ila kwa uchungu niliokuwa nao niliomba lolote litokee huyu jamaa asiwepo kwenye uchaguzi 2005.
Inauma sana kila ninapokumbuka kwamba tulifanya maamuzi ya kukurupuka wakati chaguo sahihi tulikuwa nalo. Natumai sasa Watanzania tumejifunza kutokana na makosa hatutarajii kurudia kosa kubwa kama hili linalogharimu uhai wa watanzania wengi hv sasa na wengi wetu kukosa matumaini maana hatuna pakushika wala kuegema. Ni hatari kwa kweli.
 
Nikikumbuka inauma sana ijapokuwa hakuambulia kura yangu lakani the way vijana wa rika langu kipindi hicho walivyokuwa wakimshabikia kwa kweli nilinyongonyea kwa kuona Tanzania yetu ikidumbukia shimoni pasipo kuwa na msaada wowote.
Nakumbuka huyu jamaa kipindi hicho alikuwa na kashfa tayari ya IPTL, sikupata picha akipewa madaraka makubwa kama haya atafanya ufisadi kiasi gani lakini leo kila kitu kipo wazi. Nakumbuka siku jina lake linapitishwa dodoma ilikuwa ni jioni nikiwa na collegues ofisini tukipiga simu kwa jamaa zetu waliopo dodoma kutueleza kinachoendelea. Taarifa ilivyokuja kuwa amepitishwa niliugua ghafla na wiki nzima sikuwa kwenye mood ya kufanya kazi. Sio siri ni vibaya kumuombea mtu kifo ila kwa uchungu niliokuwa nao niliomba lolote litokee huyu jamaa asiwepo kwenye uchaguzi 2005.
Inauma sana kila ninapokumbuka kwamba tulifanya maamuzi ya kukurupuka wakati chaguo sahihi tulikuwa nalo. Natumai sasa Watanzania tumejifunza kutokana na makosa hatutarajii kurudia kosa kubwa kama hili linalogharimu uhai wa watanzania wengi hv sasa na wengi wetu kukosa matumaini maana hatuna pakushika wala kuegema. Ni hatari kwa kweli.

Tunachoweza kufanya ni kumshukuru Mungu kwa kutupa fursa ya kujifunza umuhimu wa kutafakari kwa kina tunapochagua rais ajaye bila kujali propaganda za wapambe na vyombo vya habari ambavyo kwa nchi yetu ni rahisi kununuliwa. Pole sana!
 
M sure kama ccm wangekuwa wana utaratib wa kuachiana miaka 15 huyu jamaa kipindi cha tatu angepata kura 3 yaan yake mwenyewe, ridhiwan na mama salma...shame upon himslf!
 
Ndio mkuu imetugharimu watz tuliangalia umaarufu uliotokana na siasa chafu tukaacha ubora na kuudharau kwamba haufai sasa dhambi hii inatutafuna, haya ni madhara ya sisi watz kupenda matukio bila kuangilia matokeo yake sio siri jamaa ana miaka kama 6 sasa lakin kwangu mimi ukiniuliza kuna lipi kalifanya kanifurahisha hakuna siwez kukupa jibu labda wenzang mnaweza kunipa jibu la kunishawish kama nyie kawashawish kwa jambo lolote la maana nisaidien.
 
TIP:
this is forum, usionyese ufundi wa kuandika, hapa mtu akifungua post anataka aone point moja kwa moja, be STRAIGHT, mtu hawezi kufatilia para hadi ya tatu bado kabla ya kuelewa point yako

Hata mimi siyo mshabiki wa posting, au hata e-mail, ndefu. Lakini tukubaliane kuwa umahiri wa muandishi unaweza ukampelekea hata mtu kusoma posting ndefu hata kama siyo tabia yake. Vile vile, uandishi mbovu humfanya mtu kukacha kusoma hata posting ya mistari mitatu, baada y akusoma maneno matano ya kwanza.
 
Nakumbuka maneno ya aliyekuwa Mbunge wa BUTERE kenya! Martin Shikuku akihojiwa na Hamza Kasongo katika kipindi chake alisema, "UFISADI NI CHANZO CHA MAOVU YOTE"
 
tusirudie makosa mara ya ngapi ndugu yangu?nakiri mara ya kwanza alipoteuliwa kugombea,nilikuwa na imani nae kwa maneno matamu aliyotoa kinywani mwake.nikasema sasa huyu kijana mwenzangu,walau tutaelewana lugha,hasa ya 'zero tolerance to ujinga'.nilijuta kwa miaka mitano kwa kumuamini huku nikisema huenda atabadilikia njiani.sikuamini macho yangu nilipomuona akichukua fomu tena,ila nilivunjika moyo kuona ameshinda.nimekata tamaa ya maisha,nategemea uozo zaidi 2015!
<p>
Hakika hili liwe fundisho kubwa kwetu na tusirudie makosa.
</p>
<p>&nbsp;</p>
 
TIP:
this is forum, usionyese ufundi wa kuandika, hapa mtu akifungua post anataka aone point moja kwa moja, be STRAIGHT, mtu hawezi kufatilia para hadi ya tatu bado kabla ya kuelewa point yako

Mimi nimeweza kufuatilia.......
 
TIP:
this is forum, usionyese ufundi wa kuandika, hapa mtu akifungua post anataka aone point moja kwa moja, be STRAIGHT, mtu hawezi kufatilia para hadi ya tatu bado kabla ya kuelewa point yako
Wewe ndio Mtikila?
 
Kamwe katika maisha yangu siwezi kusahau kitendo cha wana CCM wengi kuwaweka Dr. Salim na JKikwete katika mzani mmoja. Hivi mtu unaanzia wapi kuwalinganisha Salim na Kikwete? Heshima na hadhi ya Dr. Salim, kitaifa na kimataifa ni ya kutukuka. Kumlinganisha na Kikwete ni aibu kubwa kwa watu wanaofikiri vizuri.
 
Back
Top Bottom