Chawa hakai sehemu Safi na mtu msafi hawezi kuwa na chawa

RWANDES

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
1,615
3,909
Chawa hupenda kukaa sehemu chafu Sana na huzaliana kwa wingi na hufyonza damu na kiumbe kudhoofika. Hivyo chawa sehemu Safi hawapendi kwani chawa NI adui wa usafi.

Hapa namkumbusha mama anayetuoongoza asifurahi kuwa na chawa kwani kuwa na chawa asifikrie NI sifa katika serikali yake , wote tunajuwa huduma nyingi kwenye ofisi za umma zimezorota kwa kasi sasa hivi mwenye kisu kikali ni mtu mwenye fedha ndiye anayepata huduma Bora tena kwa ulinzi mkali wenzangu na Mimi ikifika ofisi hizo utazungushwa kwenda na kurudi hadi utachoka mwenyewe.

Bila rushwa au kujuana na watu wa mfumo wengi tusahau kupata huduma ambayo ungepata bure kabisa

Kwa kweli kinachonisikitusha Zaidi NI kwamba hii ndoo nchi yangu Tanzania yenye Kila Aina ya rasili Mali tunaziona kwa macho wanaofaidi NI wachache. National cake ni ya kundi flani kwenye nchi yetu.

Mungu tusikie kilio chetu 2025 tupate hata atakayekumbuka kututengenezea Barabara za kupita Bajaji zetu !

Biashara ya mchakato katika serikali hii ipo Kasi mno na upembuzi yakinifu na timu ya wataalamu.
 
Back
Top Bottom