Ulimwengu wa roho ni timilifu

Hauna makosa! Hauna mawaa kwa kizungu tunaweza kusema no errors no faults. ...najua utasema kuwa Mungu kasema hakuna mkamilifu!

Kumbuka kasema hakuna mkamilifu la hata mmoja akimaanisha mwanadamu sio roho. Makosa ya kiutendaji,makosa binafsi, makosa ya kukusudia na kutokusudia , habari za bahati mbaya na maneno kama heri ningejua....! Haya yote si ya kiroho ni ya kimwili

Ukisoma habari za jicho la tatu, machale ,ndoto taarifa ufunuo na maono unaona kwa usahihi kabisa ulimwengu wa roho ulivyotutangulia kufahamu yajayo kabla ya nafsi zetu kupata taarifa rasmi

Kila tukio liko preplanned. Hakuna bahati mbaya, ni limitations za ufahamu tu wa kibinadamu ndio umezuiwa kuona haya
Maisha yako na yangu yako kwenye mchoro kamili tangu kuzaliwa mpaka kufa...........

Utazaliwa lini na nani utapitia nini na wapi utakutana na nani! Utakuwa nani, utafanya nini, utaanguka wapi na kusimama wapi! Yote haya hayatokei kwa bahati mbaya

Jee huu ni ubaguzi?
Kwamba mmoja tangu kuzaliwa mpaka kufa yeye ni mafanikio tu?
Kwamba tangu kuzaliwa mpaka kufa ni yeye na matatizo matatizo na yeye?

Kwamba wengine husimama na kushamiri kisha huanguka na kupotea kabisa?
Kwamba wengine hukulia kwenye shida nyingi na matatizo lakini huja kutoboa na kutoka kimaisha?

Ulimwengu wa roho hauyumbishwi...formula zake ziko kama zilivyo michoro yake ni kamili na kamilifu unapojaribu kuisahihisha na ishu za waganga nyota na ngekewa unajitafutia dhahama usiyoiweza

Utafanikiwa kwa kipindi tu lakini asili itakurudisha kwenye shina lako kiroho..pale ulipotakiwa kuwa na hapo ni sawa na kujaribu kunyoosha bati lililopinda na kupondeka

Ulimwengu wa roho hauna modifications! Ishi maisha yako ukijibidiisha na ufanyayo katika mstari sahihi...usijaribu kutoka nje ya mstari kwa kuchanganya ya rohoni na ya kidunia ...hutafika mbali
Pumba. Asante kwa kunipotezea muda na kujaza seva ya JF...
 
Leo Mshana nakupinga 100%. Kama kila kitu kimeshapangwa basi kuwa na dini hakuna maana kwa vile dini zinatuambia tutende mema. Hapangekuwa na haja ya ibada wala kufunga iwe Ramadhani au Kwaresima. Dhambi ni tendo analolifanya mtu kwa kudhamiria-yaani kwa UAMUZI WAKE. Unaposema kila kitu kimepangwa una maana hata dhambi mtu anazofanya ambazo anaamua kuzifanya yeye mwenyewe kwa utashi wake ni kitu kilichokuwa kimepangwa? Nonsense. Sema Mungu ametupangia kila mmoja maisha mema (na kumpa kila mtu kipawa fulani cha kumfanikisha maishani), lakini shetani (kupitia binadamu wenzetu) anazuia mafanikio Mungu aliyotupangia. Kwa hivyo, mipango Mungu aliyotupangia kweli ipo (na ni mizuri) lakini sio kwamba eti kama ni uovu basi ni Mungu amemuumba mtu ili awe nao. HAPANA. Mungu amemuumba KILA MTU afanikiwe ila ni shetani tu anayeharibu.
 
Kama uyasemayo ni kweli basi mafundisho yoyote yanayo amini ktk hukumu ya mwisho si yakweli....
Kama tangu kuzaliwa ramani yako ya maisha imechorwa na huwezi badili lolote ktk ulimwengu wa roho, kwa nini kuwe na hukumu???

Najaribu kuwaza tu!
Hivi ulimwengu Wa roho ndo ulimwengu gani jamani? Tujuzani jamini sisi wengine hatuamini uwepo Wa mungu
 
Leo Mshana nakupinga 100%. Kama kila kitu kimeshapangwa basi kuwa na dini hakuna maana kwa vile dini zinatuambia tutende mema. Hapangekuwa na haja ya ibada wala kufunga iwe Ramadhani au Kwaresima. Dhambi ni tendo analolifanya mtu kwa kudhamiria-yaani kwa UAMUZI WAKE. Unaposema kila kitu kimepangwa una maana hata dhambi mtu anazofanya ambazo anaamua kuzifanya yeye mwenyewe kwa utashi wake ni kitu kilichokuwa kimepangwa? Nonsense. Sema Mungu ametupangia kila mmoja maisha mema (na kumpa kila mtu kipawa fulani cha kumfanikisha maishani), lakini shetani (kupitia binadamu wenzetu) anazuia mafanikio Mungu aliyotupangia. Kwa hivyo, mipango Mungu aliyotupangia kweli ipo (na ni mizuri) lakini sio kwamba eti kama ni uovu basi ni Mungu amemuumba mtu ili awe nao. HAPANA. Mungu amemuumba KILA MTU afanikiwe ila ni shetani tu anayeharibu.

Kwa mtazamo wangu, ulimwengu wa Roho upo. Ni mazingira (Misingi ya uhalisia ya mazingira yetu) kabla hujaja kwenye mwili tulikuwepo katika ulimwengu wa Roho, na hata vitu vingi kabla havijatokea kwa kuweza kuonekana vinaanzia ulimwengu wa Roho.

Package nzima ipo kuanzia ulipozaliwa, utapita wapi (kuanzia kuzaliwa mpaka utakapokufa/ siku ya mwisho duniani) kwani asili ya kuumbwa kwa mtu kunabaraka ndani yake. Mungu alituleta ili tuitawale Dunia

Kinachotokea baada ya anguko (baada ya kufarakana na Mungu), shetani ndio akatawala Dunia na kumbuka dhumuni la shetani ni kutufarakanisha na Mungu.

Shetani anaweza kuingia katika mfumo wa Mwanadamu na kubadilisha destiny yake, na ndio maana tunaanguka katika dhambi, shetani anaweza kuweka tamaa kwenye moyo wa mtu... ambapo kwa hiyo tamaa ukaaungukia katika mauti.

Waefeso 6:10-12 yasema, “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”
 
Anachosema mshana jr ni kweli kulingana na bible. Biblia imeelezea predestination/kukusudiwa kimbele. Ndio maana Mungu alisema shukuruni kwa kila jambo. Liwe jema au baya tushukuru tu kwa sababu yeye ndiye kila kitu.

Ukitaka kuangalia pre destination kwenye Maisha yako chunguza hili. Ulipokuwa mtoto mdogo wakati ukikua uliwa na kupanga mambo mengi nanpengine kufikiria ungekuwa nani baadaye. Ungeoa mke yupi, watoto fulani, nyumba fulani etc.
Lakini leo almost mambo sivyo yalivyo salaaleh! Mahali ulipo hukuwahi kupawazia, status uliyonayo hukuwahi kuifikiria kabla, mke, watoto, mali na maisha kwa ujumla siyo yale uliyowazia zamani. Hii inaashiria nini??? PREDESTINATION.
Tangu unakuja Duniani ulishapangiwa njia ya kupita na huwezi kuikwepa. Hapa chini ni mfano wa pre destination unaoongelewa na Biblia:
Waefeso 1:3-5
[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;
[4]kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.
[5]Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake.

Kwa hiyo ukijiona ni mkristo leo hujifanyi hivyo, bali ulishakusudiwa hilo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Maana yake alikujua na kukuchangua kimbele ili uwe hivyo. Kwakuwa anajua mwisho kabla ya mwanzo ndio maana alikuwekea njia ya wewe kufikia kile alichokukusudia. Hilo ni kweli kabisa
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

Yeremia 1 : 5
 
kwahiyo maisha tayari yapo framed, sisi tunafuata tu kama train kwenye railway!, kwahyo mfano jambazi yeye alipangiwa atazaliwa, ataishi itafika muda ataiba ataua halaf mwisho wa siku motoni, na wengine reli yao imenyooka hadi peponi!?
Dah..... Wahubiri huwa Wanajichanganya sana...... Ukifikiria kwa utulivu utaona dini ni zaka na sadaka tu
 
Dah..... Wahubiri huwa Wanajichanganya sana...... Ukifikiria kwa utulivu utaona dini ni zaka na sadaka tu
a775a72d15c5245b1ebffba5e7b79a1f.jpg
 
Leo Mshana nakupinga 100%. Kama kila kitu kimeshapangwa basi kuwa na dini hakuna maana kwa vile dini zinatuambia tutende mema. Hapangekuwa na haja ya ibada wala kufunga iwe Ramadhani au Kwaresima. Dhambi ni tendo analolifanya mtu kwa kudhamiria-yaani kwa UAMUZI WAKE. Unaposema kila kitu kimepangwa una maana hata dhambi mtu anazofanya ambazo anaamua kuzifanya yeye mwenyewe kwa utashi wake ni kitu kilichokuwa kimepangwa? Nonsense. Sema Mungu ametupangia kila mmoja maisha mema (na kumpa kila mtu kipawa fulani cha kumfanikisha maishani), lakini shetani (kupitia binadamu wenzetu) anazuia mafanikio Mungu aliyotupangia. Kwa hivyo, mipango Mungu aliyotupangia kweli ipo (na ni mizuri) lakini sio kwamba eti kama ni uovu basi ni Mungu amemuumba mtu ili awe nao. HAPANA. Mungu amemuumba KILA MTU afanikiwe ila ni shetani tu anayeharibu.
Ujamuelewa vizuri na Mimi nilipoanza kusoma nikabaki nashangaa nimefuatilia reply zake zote anamaanisha kuwa kabla ujazaliwa Mungu anakuwa amekupangia njia yako utayopitia hadi utakapo kufa na njia hii ni njema maana mwishowe tutauona ufalme wa Mungu.

Tatizo linakuja pale tunapoacha kuufuta mchoro hule ( njia) mana njia hii ina up and down ila ni kwa mapenzi ya Mungu ili mwishoni tufikie destination ya kuuona ufalme wa Mungu think about Yusufu alifungwa hadi gerezani ila ilikuwa kwa mpango wa Mungu think about Samson hizi njia zilikuwa katika mchoro ili wamtukuze Mungu na kumbuka ukifuta mchoro wako lazima ufikie mwisho mwema mana Mungu anatuwazia mema.

Sasa tatizo ni pale ambapo tunaishi nje ya mchoro looh hapo inaitwa kukengeuza unaweza pitia magumu ukamwacha Mungu kumbe ilikuwa ndio pathway yako kuuona ufalme wa Mungu basi tukapanic tukaanza kutafuta nguvu za ibilisi zitupatie maisha mazuri totally wrong.

Cha msingi tusiache kuomba pia na shukuran regardless tunapitia mazingira gani Mungu anatuwazia mema.
 
Back
Top Bottom