BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,331
Nimeipenda hii, mrembo alishakutia machoni akawa anakuchora siku ukilewa anakusemea hovyo na siku ukiwa sober anakupa hongera zako. Kuja kustuka mkafahamiana na kujenga penzi mara mkafunga pingu za maisha. Hongera zenu.
Nilikua nimepanga mtaa mmoja maeneo ya Mbezi Beach ndio kwanza nimeanza kazi mishahara kama miwili hivi....Natoka Bar nimelewa tilalila mida kama saa tatu usiku...basi kuna nyumba kama ya tano kabla kufika nilikopanga huwa kuna mabinti warembo haswa siku hiyo napita nashangaa sauti inaniongelesha.... YANI MKAKA MZURI KAMA WEWE UNALEWA POMBE?? sikumbuki nilijibu nini that day...ila keshokutwa yake natoka job jioni nashangaa sauti tena inaniongelesha NAONA LEO UKO SOBER HONGERA.... aaah nikasimama ikawa ndio mwanzo wa kufahamiana...Nimetia ndani mazee mwaka wa tatu sasa nimejaliwa toto moja maridadi la kiume 2yrs ..na nategemea mwingine sometimes in November this year
CC\ Mentor acha ubazazi na viroba labda Heaven on Earth anaweza akarudisha majeshi bro
Last edited by a moderator: