Ulevi wa mume unaelekea kuniharibia kazi

Ulevi wa mume unaelekea kuniharibia kazi

Sasa kwanini aje adanganye humu? Tuseme kwa mfano yeye ndo amekosea, anafaidika vipi kuja humu na kuandika uongo? kwamba anajipa moyo au anatafuta mtu wa kukubaliana nae? itamsaidiaje....

Au unataka kusema wanawake hawana mantiki wanaandika wanavyojisikia tu....

Sielewi
Sharing inamsaidia kupata relief, awe anaongopa au anasema ukweli bado anapata relief.

Ni wangapi humu wanaleta stories hadi zinagundulika chai au wahusika wanakuwepo humu na kubanana hadi mchawi kuonekana?

Kushauri story ya upande mmoja ni kujilisha upepo, hasa issues za ndoa.
 
Hakikaa manabii wataendelea kutajirika kwa akili kama hizi. Atafute msaada wa maombi! Kwanini yeye asiombe mwenyewe? BTW shida kama hizi kuzileta hapa hutapata ushauri mzuri kwani watu hawajui undani wenu na wamesikiliza upande mmoja. Kwanini unaogopa kuitisha kikao cha familia? Nina wasiwasi huko kanisani una uhusiano na ''mtume'' ndiyo maana mumewe anakwenda kutukana huko na wewe unaogopa kumshtaki kwa wazee.
Inaonekana pia kuna ka manyanyaso fulani anapitia toka kwako,kwaio wewe tumeshakusikiliza aje nayeye tupate ya upande wa pili,ili tatizo lisuluhishwe ukiona mwanaume yuko hivyo ujue kuna shida mahali,na pia kukosa kipato ndio kuna mfanya awe hivyo maana pia hajiamini lazima atakua mkorofi mkorofi....pambana nae mfungue kamradi asimamie atatulia tu,halafu mwamini MUNGU
Hakuna justification ya kumtetea mwanaume mlevi kwa hisia uchwara za mara ananyanyaswa, mara ni one sided story. Mwanaume mlevi kufa ni ana matatizo hakuna namna ya kumfichia aibu. Nyinyi mkiwa na shida huwa mnajikataa na kuanza ulevi?
Mwanaume gani anapata changamoto anaingia kwenye uraibu.

Kunao wanaume wapuuzi nawaona mtaani. Huyu mmoja karudishwa kwao, ni mara baada ya kulewa na kusinzia bar hadi asubuhi. Wanywa supu asubuhi mmoja akamtambua akapiga simu kwa workmate wa huyo mlevi, workmate akapiga simu kwa mke wa mlevi. Mke wa mlevi akagoma kwenda kumchukua mume wake akapigiwa mjomba wa mlevi. Jamaa kaja kuamka kajikuta kwa mjomba akapewa supu na tiketi mkononi. "Tumekushindwa nenda nyumbani na wazee wajaribu". Kazi kaacha bila likizo.

Sasa pale mtaani watu wasiojua wako wanamlalamikia mke wa mlevi mi nawashangaa sana. Jamaa mara ya nne hii analewa anaokotwa bar, mapafu yalishajaa maji akachomwa sindano 50k per day kwa wiki ngapi sijui, jamaa ana tatizo la uzazi sababu ya pombe mwaka wa pili huu hajatungisha mimba (wamepima), alikuwa na TB na ana baruza za onyo zimepitiliza. Ukitazama ana mke mzuri, mpole, mcha Mungu, mvumilivu ila mume anafanya upuuzi. Sasa mtu kama huyu mke akija kuuliza mnamuandama wa nini.

Kuna huyu mwingine kafungua biashara ya juice. Kapanga kibanda kaweka fridge na yeye wakiingia hawezi toshea mtu mwingine. Sasa mumewe hana kazi anakuja kuweka kiti hapo kukagua wateja, mara bodaboda wakiagiza juisi hata chupa tano unaona mume kanyanyuka kaenda kuchungulia mkewe akiongea nao. Huyu nae kama si ubabaifu na kutojiamini ni nini.
 
Back
Top Bottom