Exile
JF-Expert Member
- Feb 21, 2021
- 1,434
- 3,455
Maimamu ambao waliondoka nchini Morocco ili kuendesha ibada kwa Wamorocco wanaoishi Ulaya katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, wametokomea kusikojulikana na hawajarejea nyumbani hadi leo.
Taarifa kutoka Morocco zinasema Maimamu 13 waliotumwa na Wizara ya inayojihusisha na mambo Kidini kwenda nchi za Ufaransa, Ubelgiji na Ujerumani “walitoweka” wakati wakijiandaa kurejea nchini mwao.
Inaelezwa kuwa Maimamu hao wasomi wenye shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na hata udaktari...hulipwa kila mwezi na serikali ya Morocco kwa kufanya kazi katika misikiti na hunufaika na safari ya kwenda Ulaya kuongoza sala ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa gharama za serikali.
Hata hivyo, baada ya kazi yao kuisha tarehe 12 April, maimamu hao waliotumwa na Wizara ya Habbous na Masuala ya Kiislamu hawakufika kwenye uwanja wa ndege na tangu wakati huo hawajapatikana.
Source: Maimamu 13 wa Morocco waliotumwa ulaya kwa ajili ya Ramadhani watoweka
Taarifa kutoka Morocco zinasema Maimamu 13 waliotumwa na Wizara ya inayojihusisha na mambo Kidini kwenda nchi za Ufaransa, Ubelgiji na Ujerumani “walitoweka” wakati wakijiandaa kurejea nchini mwao.
Inaelezwa kuwa Maimamu hao wasomi wenye shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na hata udaktari...hulipwa kila mwezi na serikali ya Morocco kwa kufanya kazi katika misikiti na hunufaika na safari ya kwenda Ulaya kuongoza sala ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa gharama za serikali.
Hata hivyo, baada ya kazi yao kuisha tarehe 12 April, maimamu hao waliotumwa na Wizara ya Habbous na Masuala ya Kiislamu hawakufika kwenye uwanja wa ndege na tangu wakati huo hawajapatikana.
Source: Maimamu 13 wa Morocco waliotumwa ulaya kwa ajili ya Ramadhani watoweka