GE2025 Ukweli usioufahamu kuhusu wanaosema wataandamana

GE2025 Ukweli usioufahamu kuhusu wanaosema wataandamana

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
6,503
Reaction score
18,949
Wengi wenu mnajitahidi kuamini kuwa tarehe 29 watz wataandamana, ila kiuhalisia haiwezekani kwasababu zifuatazo.

1- Idadi ya wageni waliopo Tz ni kubwa mno, yaani wakongo, warundi, wamalawi, wahindi n.k. Hili kundi haliwezi kuandamana maana wapo nchini kwa hisani ya CCM. Kweli mhindi akaandamane akitaka haki?

2- Bado asilimia kubwa ya watz wapo vijijini hivyo hawajui yanayoendelea na asilimia chache iliopo mjini ndio wanajua.

3- Wengi bado wanaamini siasa sio vitu vyao, hata hafa JF tunaona mada zenye michango mingi huwa ni zipi.

4- Kuskiliziana, yaani kila mmoja anamsikilizia mwenzake aone kama ataandamana. Yaani nani alianzishe kutokana na woga.

5- Hofu ya kubambikwa kodi au makesi na kufilisiwa au hata kufukuzwa kazi.

6- Wengi wanaamini wakiandamana watauwawa au kuumizwa hivyo kuziathiri familia zao, umaskini utawafuata.

Kiuhalisia hakuna wakuandamana hiyo tarehe 29, kama tu mashabiki wa mpira walishindwa kuzomea wanasiasa siku ya matamasha ndio ije kuwa kutoka front.

Sina lengo lakuwakatisha tamaa, ila hata jana mahakamani wananchi walishindwa kuwa na umoja.
#TIMEWILLTELL
 
hivi ni kwa nini waafrika huwaona waafrika wenzao tu na ndiyo foreigners na siyo wahindi, waarabu, wachina au hata wazungu? hapo kwenye wageni umetaja waafrika tu kongo, malawi nk lkn no irani, india, pakis, why ? …
 
hivi ni kwa nini waafrika huwaona waafrika wenzao tu na ndiyo foreigners na siyo wahindi, waarabu, wachina au hata wazungu? hapo kwenye wageni umetaja waafrika tu kongo, malawi nk lkn no irani, india, pakis, why ? …
Upo sahihi hata hao wahindi waliopo nchini unadhani wataandamana?
 
Wengi wenu mnajitahidi kuamini kuwa tarehe 29 watz wataandamana, ila kiuhalisia haiwezekani kwasababu zifuatazo.

1- Idadi ya wageni waliopo Tz ni kubwa mno, yaani wakongo, warundi, wamalawi n.k. Hili kundi haliwezi kuandamana maana wapo nchini kwa hisani ya CCM.

2- Bado asilimia kubwa ya watz wapo vijijini hivyo hawajui yanayoendelea na asilimia chache iliopo mjini ndio wanajua.

3- Wengi bado wanaamini siasa sio vitu vyao.

4- Kuskiliziana, yaani kila mmoja anamsikilizia mwenzake aone kama ataandamana. Yaani nani alianzishe kutokana na woga.

5- Hofu ya kubambikwa kodi au makesi.

6- Wengi wanaamini wakiandamana watauwawa au kuumizwa hivyo kuziathiri familia zao, umaskini utawafuata.

Kiuhalisia hakuna wakuandamana hiyo tarehe 29, kama tu mashabiki wa mpira walishindwa kuzomea wanasiasa siku ya matamasha ndio ije kuwa kutoka front.

Sina lengo lakuwakatisha tamaa, ila hata jana mahakamani wananchi walishindwa kuwa na umoja.
#TIMEWILLTELL
Upo sahihi mkuu!
Bongo bado bongo zimelala na ndiyo maana hawa washenzi wanaweza kutujibu wanavyojisikia
Nimemsikia msigwa anasema wanaowaza kuandamana tarehe 29 wanajisumbua bure haiwezekani
Kwa nchi Ambazo wananchi wako na akili timamu hawezi kujibu hivyo
 
Wengi wenu mnajitahidi kuamini kuwa tarehe 29 watz wataandamana, ila kiuhalisia haiwezekani kwasababu zifuatazo.

1- Idadi ya wageni waliopo Tz ni kubwa mno, yaani wakongo, warundi, wamalawi n.k. Hili kundi haliwezi kuandamana maana wapo nchini kwa hisani ya CCM.

2- Bado asilimia kubwa ya watz wapo vijijini hivyo hawajui yanayoendelea na asilimia chache iliopo mjini ndio wanajua.

3- Wengi bado wanaamini siasa sio vitu vyao.

4- Kuskiliziana, yaani kila mmoja anamsikilizia mwenzake aone kama ataandamana. Yaani nani alianzishe kutokana na woga.

5- Hofu ya kubambikwa kodi au makesi.

6- Wengi wanaamini wakiandamana watauwawa au kuumizwa hivyo kuziathiri familia zao, umaskini utawafuata.

Kiuhalisia hakuna wakuandamana hiyo tarehe 29, kama tu mashabiki wa mpira walishindwa kuzomea wanasiasa siku ya matamasha ndio ije kuwa kutoka front.

Sina lengo lakuwakatisha tamaa, ila hata jana mahakamani wananchi walishindwa kuwa na umoja.
#TIMEWILLTELL
Israel ilianza kuiambia Iran itaishambulia miaka 40 kabla ya kufanya hivyo , Iran wakawa wanapuuza Kuwa Israel ni kanchi kadogo hakana uwezo

Siku waliyofanya hivyo Wairan wakashangaa imekuwaje watu wanajua kila nyumba kila chumba anachokaa kiongozi kumbe wenzao walikuwa wamemaanisha na wanajiandaa.

Hakuna kosa Serikali watafanya kama kuamini wanaweza kuwazuia watanzania wasiandamane.

Mimi niko mahali naona kabisa kama ikitokea Watu 100 pekee wakajaa sehemu Strategic au kwenda kwenye vituo vya kura kuvichoma au kufanya jambo lolote, basi nchi hii itaripuka ghafla bila kujiandaa.

Wazungu hawapuuzi kitu hata nukta ndio maana unaona kila siku wanagundua teknolojia mpya za kulinda nchi zao na uhuru wao
 
Vitu vingi vilianza kama utani hadi vilivyokuwa serious,watu wanalalamika mnawapuuza,watu wanapotea mnapuuza,kodi mnapuuza.Kumbuka wananchi wanatunza tu hasira na jinsi chama kinavyoendela kuwa madarakani na ndio watu wanazidi kukasirika.Hata ikishindikana tarehe 29 niamimi mimi miaka ijayo kutakuja kutokea balaa
 
Israel ilianza kuiambia Iran itaishambulia miaka 40 kabla ya kufanya hivyo , Iran wakawa wanapuuza Kuwa Israel ni kanchi kadogo hakana uwezo

Siku waliyofanya hivyo Wairan wakashangaa imekuwaje watu wanajua kila nyumba kila chumba anachokaa kiongozi kumbe wenzao walikuwa wamemaanisha na wanajiandaa.

Hakuna kosa Serikali watafanya kama kuamini wanaweza kuwazuia watanzania wasiandamane.

Mimi niko mahali naona kabisa kama ikitokea Watu 100 pekee wakajaa sehemu Strategic au kwenda kwenye vituo vya kura kuvichoma au kufanya jambo lolote, basi nchi hii itaripuka ghafla bila kujiandaa.

Wazungu hawapuuzi kitu hata nukta ndio maana unaona kila siku wanagundua teknolojia mpya za kulinda nchi zao na uhuru wao
😀 yaani kwa Tz bado sana. Imagine jana mahakamani, polisi wanamchangia mtu mmoja na wengine wote wamekaa wanarekodi huku wanalia.
 
Vitu vingi vilianza kama utani hadi vilivyokuwa serious,watu wanalalamika mnawapuuza,watu wanapotea mnapuuza,kodi mnapuuza.Kumbuka wananchi wanatunza tu hasira na jinsi chama kinavyoendela kuwa madarakani na ndio watu wanazidi kukasirika.Hata ikishindikana tarehe 29 niamimi mimi miaka ijayo kutakuja kutokea balaa
Makanisa ya Ngwaji yalifungiwa, kiko wapi? Lisu yuko ndani kwa makosa ya kubumba, kila mtu yupo busy na mambo yake. Mdude yuko wapi? Ikifika siku wewe MTz ukawa tayari kutenda haki bila kuombwa na mtu basi jua mabadiliko yako mbioni.
 
Israel ilianza kuiambia Iran itaishambulia miaka 40 kabla ya kufanya hivyo , Iran wakawa wanapuuza Kuwa Israel ni kanchi kadogo hakana uwezo

Siku waliyofanya hivyo Wairan wakashangaa imekuwaje watu wanajua kila nyumba kila chumba anachokaa kiongozi kumbe wenzao walikuwa wamemaanisha na wanajiandaa.

Hakuna kosa Serikali watafanya kama kuamini wanaweza kuwazuia watanzania wasiandamane.

Mimi niko mahali naona kabisa kama ikitokea Watu 100 pekee wakajaa sehemu Strategic au kwenda kwenye vituo vya kura kuvichoma au kufanya jambo lolote, basi nchi hii itaripuka ghafla bila kujiandaa.

Wazungu hawapuuzi kitu hata nukta ndio maana unaona kila siku wanagundua teknolojia mpya za kulinda nchi zao na uhuru wao
mjuba mbona kama unavitishia vyombo vya ulinzi na usalama viwe na tight security high pressure siku hiyo. Unaviathiri kisaikolojia vishindwe kuelewa wapiga kura na waandamanaji ni wapi hasa! Utawachanganya wachanganyikiwe
 
Una wasiwasi na hayo maandamano ambayo waandaaji wanasema yatakuwa siku ya uchaguzi na ndiyo maana umejitokeza kutafuta uhakika kama yatakupo kweli ama hayapo.

Police wakitisha watu - wananchi hawatatoka ndani kwenda kupiga kura vituo vitakuwa wazi hence uchaguzi utafeli 100%.

Wananchi wakiruhusiwa kutoka huwezi kujua huyu na yule ndo wanakwenda kituoni ama ndo wanajikusanya?

Unless tume inadili tarehe ya uchaguzi dk za mwisho ili kuiua hiyo hoja ya kuandamana 29th October ipo ki mtego.
 
Usisababishe majeshi yote ya ulinzi na usalama yatoke na kutapakaa mitaani kulinda vituo vya kupiga kura visihujumiwe na haohao wapiga kura watakaojigeuza kuwa waandamanaji kuhujumu uchuguzi mzima uvurugike. Bora uchaguzi upite tuendelee na maisha kama kawaida. Watanzania hawana hulka za kuandamana na mambo ya fujo si jadi yao
 
Back
Top Bottom