ABEDNEGO CHARLES
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 567
- 104
Ndiyo kawaida ya Historia. Kuna nadharia ya Historia kuwa na aina 2 za watu. Commoners na noble heroes. Commoners hutumika kuwainua ma noble heroes
Ndugu zake wawili, waliwekwa kizuizini bila ya kufikishwa mahakamani na kufungwa kwa zaidi ya miaka kumi.
Katika mwaka 1982 ndugu zake Kambona na Otini Kambona walifunguliwa kutoka kizuizini baada ya juhudi za waziri mkuu wa New Zealand Robert Muldoon.
'IN POLITICS, THERE ARE NO PERMANENT FRIENDS NOR ARE THERE PERMANENT ENEMIES'Gagnija,
Kweli kuna maswali mengi ambayo hatuna majibu yake ya uhakika. Kambona aliwahi kuwa waziri wa ulinzi. Alichofanya wakati huo aliweka watu wake katika nafasi muhimu jeshini na vile vile katika Usalama wa Taifa. Mzee ES, wakati wa harakati za kupigania uhuru, Mwalimu alikuwa anahitaji msaada wa kila mtu. Kambona, Kawawa, Shaba, Bomani, Eliufoo, you name them. Kuunda huu utanzania usio na misingi ya kikabila ilikuwa kazi kweli kweli. Na hapo ndio tunapaswa kuwashukuru wazee wetu wa TANU.
Kambona alikuwa na personal ambitions, na nina hakika kama Mwalimu angemwachia madaraka aliyomwachia Kawawa ya uwaziri mkuu kwa mwaka mzima, Mwalimu asingerudi kama rais mwaka 1962. Hiyo ya kumwachia aende London nadhani Mwalimu alimwona less a threat outside the country than inside. Kumbuka this was only 3 years after the 1964 mutiny. With him outside it would be easy to root out his supporters within the army and the intelligence. Na kweli time came to prove Mwalimu right.
Kwani ana undugu nae?bonge ya stori
ni vizuri kujua hao wapigania uhuru kama hivi, umekuwa neutral hujahusianisha maisha yake ya kupigania uhuru na udini wala ukabila, wala hujasema alikuwa baba ako mdogo, na wala hujatumia article hii ku diminish role mwalimu Nyerere au kumdis kwa namna yyte.
hivo ndio historia hupaswa kuandikwa big up, tukitaka kufichua historia zilizo fichwa tuwe impartial tutoe facts kama hivi.
RIP Waziri Kambona
Iceman,bonge ya stori
ni vizuri kujua hao wapigania uhuru kama hivi, umekuwa neutral hujahusianisha maisha yake ya kupigania uhuru na udini wala ukabila, wala hujasema alikuwa baba ako mdogo, na wala hujatumia article hii ku diminish role mwalimu Nyerere au kumdis kwa namna yyte.
hivo ndio historia hupaswa kuandikwa big up, tukitaka kufichua historia zilizo fichwa tuwe impartial tutoe facts kama hivi.
RIP Waziri Kambona
Mkuu Maalimkatika historia ya uhuru wa Tanganyika.
Vipi utaikwepa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na uifikie historia ya TANU?
...kwa nini iwe Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...
Waliothubutu kuikwepa historia hiyo matokeo yake hii leo yanakutisha.
Utawajua vipi walioasisi TANU ikiwa huitaki historia ya Al Jamiatul Islamiyya?
Na akiacha kuweka wazi, pia nae ni mmojawapo wa wanaoficha hiyo historiaMkuu Maalim
Mohamed Said
Tufahamishe uhusiano wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...na historia ya TANU?.
...kwa nini iwe Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...?
Tueleze hao waliothubutu kuikwepa historia hiyo matokeo yake hii leo ni yapi na yanatisha kivipi?.
Pia sio vibaya tukiwajua Waasisi wa TANU na uhusiano wao na . Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...
Paskali
Kleist Sykes alikuwa mmoja wa waasisi wa African Association mwaka wa 1929 na mwaka wa 1933 akawa pia mmoja wa waasisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.Mkuu Maalim
Mohamed Said
Tufahamishe uhusiano wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...na historia ya TANU?.
...kwa nini iwe Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...?
Tueleze hao waliothubutu kuikwepa historia hiyo matokeo yake hii leo ni yapi na yanatisha kivipi?.
Pia sio vibaya tukiwajua Waasisi wa TANU na uhusiano wao na . Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika...
Paskali
Asante kwa taarifa hii, where is the interlinking?.Kleist Sykes alikuwa mmoja wa waasisi wa African Association mwaka wa 1929 na mwaka wa 1933 akawa pia mmoja wa waasisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Viongozi hawa walioasisi African Association ndiyo kundi hili hili lililoasisi Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Watoto wa Kleist wote watatu Abdul, Ally na Abbas walikuwa katika TAA na hawa ndiyo pamoja na vijana wenzao wa 1950s waliokuja kuunda TANU 1954.