Ukweli ni kwamba, mkuu wa wilaya ya Kinondoni hafiti kabisa kuongoza wilaya yetu

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,293
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Wakubwa leo sina mengi ya kuelezea, ila ukweli ni kwamba mkuu wa wilaya yetu ya Kinondoni aliepo ofisini sasa hafai hata robo kuongoza wilaya yetu.

Kila mtu anafahamu kwamba wilaya ya Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kuwa na wasomi wengi nchini, ndio wilaya inayoishi viongozi wengi nchini, ndio wilaya inayoongoza kuwa na matajiri wengi nchini na ndio wilaya iliyoendelea kimakazi kuliko wilaya yoyote ile nchini.

Hivyo nilitarajia kutokana na sifa hizo nilizotaja hapo juu, pengine serikali ingekuletea kiongozi au mkuu wa wilaya ambae atakuwa na elimu pamoja na ujuzi wa ku deal na watu wenye sifa nilizozitaja hapo juu, na badala yake naona tumeletewa mtu ambae ni kama vile hajui ni nini alichotakiwa au anachotakiwa kukifanya katika wilaya hii.

Maeneo mengi ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi yeye hana maono wala muda nayo, hashirikiani na mamlaka kubwa za serikali kutatua kero za sisi anaotuongoza kama vile kupigania na kusimamia miundo mbinu ya ujenzi wa barabara mbali mbali ambazo zinatakiwa kujengwa, utatuaji wa migogoro ya ardhi, changamoto za usafiri katika maeneo ambayo hayafikiki, upatikanaji wa maji nk.

Najua kuna watu watasema kwamba ooh toka lini mkuu wa wilaya akajenga barabara, lkn ukweli ni kwamba juhudi zake na uambanaji wake vinaweza kubusti na kuchangia ujengaji huo.

Yani jamaa anashindwa kupambania wilaya yake hata na wakuu wa wilaya wenzake kina DC Komba (Ubungo) , DC Matinyi (Temeke) , DC Bulembo (Kigamboni) nk ambao kila siku hukutana na wananchi wao kwa ajili ya kuwasikiliza kero zao na baadae kuangalia njia ya kuzitatua kero hizo.

Yeyote ambae yupo karibu na DC huyo hapa JF, naomba amfikishie ujumbe na kumwambia mh DC ajitafakari vizuri kama yeye kwa elimu yake na uwezo wake anao uwezo wa kweli wa kuongoza wilaya yetu, au ameamua tu kukaa ofisini kutafuna kodi za wavuja jasho bila tija yoyote.

Bora DC Godwin Gondwe alijitahidi kushirikiana na wananchi kwa namna moja au nyingine, lkn huyu wa sasa hamna kitu na ni kama vile kaletwa mahala asipopajua au kupapenda.

Wana Kinondoni safari hii tumeamua kuwa kitu kimoja katika kufuatilia na kusimamia maendeleo yetu. Kamwe hatutokubali kuona vichelema mbali mbali vinaletwa katika wilaya zetu kuja tu kupiga picha na kukaa ofisini kusubiri mshahara wa mwezi bila kupigania maendeleo yetu na haki zetu.

Asanteni wakuu.
 
Vp kuusu ule uzi wako wa Gwajima mkuu. Mlimalizana nae?
Gwajima nafikiri sisi wananchi ndo tuta deal nae vizuri mwaka 2025.
Hivyo kama ana lengo la kuendelea kuwa mbunge wetu basi afanyie kazi yale niliyomwambia uzini.
 
Wewe itakuwa CCM tena wale wanaojifanya bila wao.. mambo hayaendi.... Akija mtumishi yeyote wa serikali mnajifanya kumwambia eti "tusikilize sisi utakaa sana hapa" mkibanwa kwenye mbavu mnaanza kutafuta huruma kwenye mitandao ya kijamii... Fanyeni Kazi bana... Achane hizo bana mtawarithisha watoto wenu domo au?

NB: huko china au japani, wanawafundisha watoto wao kilimo, ujenzi, nidhamu, kupenda Kazi na ubunifu... Nyie mmekaza na umbea tu...
Nimeandika hii baada ya kusoma huo umbea wako... Maana imeniuma sana kwakuwa naelewa kinacho endelea....
 
Huyo DC wa Kinondoni alitokea wapi? Utendaji wake ulikuwaje ukiacha kufanyia faulu upinzani katika 2020 uchaguzi?
 
Huyo DC wa Kinondoni alitokea wapi? Utendaji wake ulikuwaje ukiacha kufanyia faulu upinzani katika 2020 uchaguzi?
Ninaemzungumzia hapa ni mpya , hivyo mwaka 2020 hakuwepo Kinondoni.

Jamaa hana anachokifanya kuleta maendeleo jimboni wakati wenzake maeneo mengine wanapambana usiku na mchana.
 
Kati ya teuzi bora kabisa za Mheshimiwa Rais ni huyu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ni Mtu makini,Msikivu na anajua kuishi na Kila mtu yuko Vizuri sana yaani kwa lugha ya Ndg yetu humu jukwaani Pascal Mayalla anasema yuko Humble down to Earth.!
Mkuu hivi toka Gondwe alipohamishwa na kumuachia ofisi huyu wa Sasa, ni kitu gani cha maana ambacho ameshakisimamia kikafanikiwa?
 
Wasalaam Mkuu,
Binafsi naona post yako imejaa majungu. Mimi kama mkazi wa Kinondoni nampongeza sana Mkuu wa Wilaya Mh. Saad kwa namna anavyoongoza. Tangu amehamia hapa ame-perfom vizuri sana tena bila mbwembwe tofauti na watangulizi wake.

Mh. Saad amejitengea siku ya Alhamisi kusikiliza kero mbalimbali hususani migogoro ya Ardhi na kuzitatua hapohapo. Ni kiongozi mwenye hofu na Mungu ni ngumu kuingilika kifisadi. Mungu mbariki Mh. Saad, Mungu wabariki wakazi wa Kinondoni.
 
Wasalaam Mkuu,
Binafsi naona post yako imejaa majungu. Mimi kama mkazi wa Kinondoni nampongeza sana Mkuu wa Wilaya Mh. Saad kwa namna anavyoongoza. Tangu amehamia hapa ame-perfom vizuri sana tena bila mbwembwe tofauti na watangulizi wake.

Mh. Saad amejitengea siku ya Alhamisi kusikiliza kero mbalimbali hususani migogoro ya Ardhi na kuzitatua hapohapo. Ni kiongozi mwenye hofu na Mungu ni ngumu kuingilika kifisadi. Mungu mbariki Mh. Saad, Mungu wabariki wakazi wa Kinondoni.
Naunga mkono ulichoandika mkuu.
 
Back
Top Bottom