Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,860
- 12,293
Habari zenu wanaJF wenzangu,
Wakubwa leo sina mengi ya kuelezea, ila ukweli ni kwamba mkuu wa wilaya yetu ya Kinondoni aliepo ofisini sasa hafai hata robo kuongoza wilaya yetu.
Kila mtu anafahamu kwamba wilaya ya Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kuwa na wasomi wengi nchini, ndio wilaya inayoishi viongozi wengi nchini, ndio wilaya inayoongoza kuwa na matajiri wengi nchini na ndio wilaya iliyoendelea kimakazi kuliko wilaya yoyote ile nchini.
Hivyo nilitarajia kutokana na sifa hizo nilizotaja hapo juu, pengine serikali ingekuletea kiongozi au mkuu wa wilaya ambae atakuwa na elimu pamoja na ujuzi wa ku deal na watu wenye sifa nilizozitaja hapo juu, na badala yake naona tumeletewa mtu ambae ni kama vile hajui ni nini alichotakiwa au anachotakiwa kukifanya katika wilaya hii.
Maeneo mengi ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi yeye hana maono wala muda nayo, hashirikiani na mamlaka kubwa za serikali kutatua kero za sisi anaotuongoza kama vile kupigania na kusimamia miundo mbinu ya ujenzi wa barabara mbali mbali ambazo zinatakiwa kujengwa, utatuaji wa migogoro ya ardhi, changamoto za usafiri katika maeneo ambayo hayafikiki, upatikanaji wa maji nk.
Najua kuna watu watasema kwamba ooh toka lini mkuu wa wilaya akajenga barabara, lkn ukweli ni kwamba juhudi zake na uambanaji wake vinaweza kubusti na kuchangia ujengaji huo.
Yani jamaa anashindwa kupambania wilaya yake hata na wakuu wa wilaya wenzake kina DC Komba (Ubungo) , DC Matinyi (Temeke) , DC Bulembo (Kigamboni) nk ambao kila siku hukutana na wananchi wao kwa ajili ya kuwasikiliza kero zao na baadae kuangalia njia ya kuzitatua kero hizo.
Yeyote ambae yupo karibu na DC huyo hapa JF, naomba amfikishie ujumbe na kumwambia mh DC ajitafakari vizuri kama yeye kwa elimu yake na uwezo wake anao uwezo wa kweli wa kuongoza wilaya yetu, au ameamua tu kukaa ofisini kutafuna kodi za wavuja jasho bila tija yoyote.
Bora DC Godwin Gondwe alijitahidi kushirikiana na wananchi kwa namna moja au nyingine, lkn huyu wa sasa hamna kitu na ni kama vile kaletwa mahala asipopajua au kupapenda.
Wana Kinondoni safari hii tumeamua kuwa kitu kimoja katika kufuatilia na kusimamia maendeleo yetu. Kamwe hatutokubali kuona vichelema mbali mbali vinaletwa katika wilaya zetu kuja tu kupiga picha na kukaa ofisini kusubiri mshahara wa mwezi bila kupigania maendeleo yetu na haki zetu.
Asanteni wakuu.
Wakubwa leo sina mengi ya kuelezea, ila ukweli ni kwamba mkuu wa wilaya yetu ya Kinondoni aliepo ofisini sasa hafai hata robo kuongoza wilaya yetu.
Kila mtu anafahamu kwamba wilaya ya Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kuwa na wasomi wengi nchini, ndio wilaya inayoishi viongozi wengi nchini, ndio wilaya inayoongoza kuwa na matajiri wengi nchini na ndio wilaya iliyoendelea kimakazi kuliko wilaya yoyote ile nchini.
Hivyo nilitarajia kutokana na sifa hizo nilizotaja hapo juu, pengine serikali ingekuletea kiongozi au mkuu wa wilaya ambae atakuwa na elimu pamoja na ujuzi wa ku deal na watu wenye sifa nilizozitaja hapo juu, na badala yake naona tumeletewa mtu ambae ni kama vile hajui ni nini alichotakiwa au anachotakiwa kukifanya katika wilaya hii.
Maeneo mengi ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi yeye hana maono wala muda nayo, hashirikiani na mamlaka kubwa za serikali kutatua kero za sisi anaotuongoza kama vile kupigania na kusimamia miundo mbinu ya ujenzi wa barabara mbali mbali ambazo zinatakiwa kujengwa, utatuaji wa migogoro ya ardhi, changamoto za usafiri katika maeneo ambayo hayafikiki, upatikanaji wa maji nk.
Najua kuna watu watasema kwamba ooh toka lini mkuu wa wilaya akajenga barabara, lkn ukweli ni kwamba juhudi zake na uambanaji wake vinaweza kubusti na kuchangia ujengaji huo.
Yani jamaa anashindwa kupambania wilaya yake hata na wakuu wa wilaya wenzake kina DC Komba (Ubungo) , DC Matinyi (Temeke) , DC Bulembo (Kigamboni) nk ambao kila siku hukutana na wananchi wao kwa ajili ya kuwasikiliza kero zao na baadae kuangalia njia ya kuzitatua kero hizo.
Yeyote ambae yupo karibu na DC huyo hapa JF, naomba amfikishie ujumbe na kumwambia mh DC ajitafakari vizuri kama yeye kwa elimu yake na uwezo wake anao uwezo wa kweli wa kuongoza wilaya yetu, au ameamua tu kukaa ofisini kutafuna kodi za wavuja jasho bila tija yoyote.
Bora DC Godwin Gondwe alijitahidi kushirikiana na wananchi kwa namna moja au nyingine, lkn huyu wa sasa hamna kitu na ni kama vile kaletwa mahala asipopajua au kupapenda.
Wana Kinondoni safari hii tumeamua kuwa kitu kimoja katika kufuatilia na kusimamia maendeleo yetu. Kamwe hatutokubali kuona vichelema mbali mbali vinaletwa katika wilaya zetu kuja tu kupiga picha na kukaa ofisini kusubiri mshahara wa mwezi bila kupigania maendeleo yetu na haki zetu.
Asanteni wakuu.