yvegenc prymacov
JF-Expert Member
- Jan 22, 2023
- 1,528
- 1,968
Ukweli ina maana kuu tatu,1, ni uhakika,2 kama ilivyo,3 ni kinyume cha uongo.
Ngumi Tena 😂😂😂🤣🤣🤣hapo sasakatika swala zima la ukweli ni umbo lenye pande Sita three dimension sasa hatuwezi kuwe sawa ingawa wote tutakua wakweli Aliyeona juu hatajua chini Kuna nn na aliuona chini hatajua mbele na vitu mfano Wa hivyo usishangae leo hii watu wanne walioshuhudia tukio moja kila mtu akija na stori yake na inawezekana wanabishana na ngumi zikapigwa
Kweli kinyume cha Uwongo. Biblia imesema Mungu ni Kweli na Shetani ni Baba wa Uwongo. Yesu alisema yatupaswa kumuabudu Mungu kwa Njia ya Roho na Kweli. Kuijua kweli lazima tupate picha halisi ya Uwongo kwani kinyume chake cha Uwongo ndio Kweli. Kwa mfano nikikuuliza jee unajua rangi ya Kinyonga? Hakuna anaeijua Rangi halisi ya Kinyonga kwani inabadilika kila inapotokea hali ya mabadiliko ya mazingira yanayo mzunguka.Ukweli ni Kujua na kutambua hali halisi na kutoa utata wa sintofahamu. Knowing, casying the shadow of doubt, replacing belief with knowledge.
Sent using Jamii Forums mobile app
Uongo ukirudiwa zaidi ya mara tatu inabadilika na kuwa UkweliMhnn..!!! Wakikutana waongo watupu watakubaliana na ùwongo
Hapana. Uongo siku zote utabaki kuwa uwongo, sema watu watahisi ndiyo ukweli kwa vile umesemwa sana, lakini wenyewe utabaki kuwa uwongoUongo ukirudiwa zaidi ya mara tatu inabadilika na kuwa Ukweli
#23ukweli ni uwazi na uthibithisho wa jambo,kauli isio na shaka ndani yake,inayo zungumzia uhakika wa jambo au wa kitu, je utaijuaje kua kauli hii haina pingamizi na ni sahihi!! jibu ,ufasaa na ushahidi halali ima kupitia vigezo au kwa kukileta kitu mbele ya mtaka ushahidi na kukihakikishaa!!!
Nimeperuzi uzi wote angalau wewe umefafanua vizuri sana mkuuUkweli ni uhalisia wa jambo jinsi lilivyo bila kuongeza wala kupunguza. Ni habari au taarifa ya kitu au jambo lilivyo tendeka.
Kila kitu au jambo uliloona, kusikia na hata kuadithiwa linaukwe halisi.
Ukweli halisi na ikiwa uhalisia wa jambo haupo, huo si ukweli ni uongo.
Kwa hali ya kusikitisha, wengi tunashindwa kuelewa tofauti kati ya UKWELI na IMANI.
UKWELI ni mambo ambayo tayari yamefanyika na kuthibitishwa.
IMANI ni mambo ambayo hutarajia kufanyika.
Lakini ikumbukwe kwamba Imani inajengwa na mambo ambayo tayari yamefanyika. Ni lazima mambo yaliyo fanyika na kuthibitishwa (UKWELI) yatangulie ili upate uhakika wa a mambo yajayo (IMANI).
Mkuu unachanganya IMANI na UKWELIKwa jini nilivyo ipitia michango ya hii thread na thread yenyewe I declare ukweli it's just an complicated things it depends na Imani ya watu Mila desturi na mazingira ya watu hao husika
Mfano kula kitimoto Kwa cristian ni halali na kwao huo ni ukweli to them you can't change that fact
But to Muslim ni Haram and to them you can't change that fact
So ukweli ni complicated things
Ukweli ni fiction shauri yako ,Mkuu unachanganya IMANI na UKWELI
Ukweli huwa ni mmoja tu kwa jambo mmoja
Imani ni kukubali jambo kuwa ni kweli bila uthibitisho……. Ndio maana kila imani inaamini kivyake vyake tofauti na imani nyingine kwa jambo hilo hilo moja
Futi moja ni futi moja dunia nzima lakini kitimoto ni halali au haramu itategemea na wewe umeamua kukubali kuamini lipi
Umeandika vizuri sana “unaweza ukaamini”Ukweli ni fiction shauri yako ,
Unaweza ukaamini kwamba huyo unaye mfahamu kuwa ni baba Yako kuwa ndiye baba Yako halisi na katika huo uliopo kwako ndio ukweli ukweli wenyewe
Lakini kumbe kiuhalisia sio baba Yako , so hauoni kwamba Hadi hapo ukweli ni issue ambayo ni complicated