Ukweli kuhusu tukio la tuhuma za rushwa monduli dhidi ya Masyaga Matinyi

Kinachonishangaza mimi ktk hili swala ni pale nilitumiwa sms ktk mail yangu kuwa nami nimeshiriki kusambaza habari ya waandishi waliokamtwa na rushwa huko arusha na sasa wamediriki hata kutoa habari ktk wanabidii na mabadiliko kuwa nipo kizimbani kwa swala la uchochezi na uongo nimeshangaa sana, kwanini wahusika wasiwaweke kizimbani TBC1 waliotangaza habari hiyo mara 2 na sisi kama wananchi kuzileta habari hizo JF na mitandao mingine kwani tunaelewa kuwa TBC1 ni chombo cha umma na habari zake huwa ni za uhakika na ukweli kwa hiyo mwana mtandao ana haki ya kuchukua habari toka TBC1 na kuwahabarisha wengine.

Mimi natumia jina halisi niletapo habari huwa naweka chanzo, muda na siku, ili kama kuna mtu anadhani habari ni ya uongo ama ni ya uchochezi basi anaweza fuata chanzo ili kujiridhisha, lakini kilichotokea ni kwamba muhusika hakutaka kufuata hilo na kuweka habari kuwa Eng Ibrahim Mtolera kizimbani kwa habari za uongo na uchochezi. Inasikitisha sana kiukweli.

Nimejiandaa na najipanga sasa ili niweze kuona wanasheria wanasema vipi juu ya hili

Kwa upande wangu nawapa pole wahusika lakini tuache tabia ya kutishana na kuombeana mabaya
 
Kinachonishangaza mimi ktk hili swala ni pale nilitumiwa sms ktk mail yangu kuwa nami nimeshiriki kusambaza habari ya waandishi waliokamtwa na rushwa huko arusha na sasa wamediriki hata kutoa habari ktk wanabidii na mabadiliko kuwa nipo kizimbani kwa swala la uchochezi na uongo nimeshangaa sana, kwanini wahusika wasiwaweke kizimbani TBC1 waliotangaza habari hiyo mara 2 na sisi kama wananchi kuzileta habari hizo JF na mitandao mingine kwani tunaelewa kuwa TBC1 ni chombo cha umma na habari zake huwa ni za uhakika na ukweli kwa hiyo mwana mtandao ana haki ya kuchukua habari toka TBC1 na kuwahabarisha wengine.

Mimi natumia jina halisi niletapo habari huwa naweka chanzo, muda na siku, ili kama kuna mtu anadhani habari ni ya uongo ama ni ya uchochezi basi anaweza fuata chanzo ili kujiridhisha, lakini kilichotokea ni kwamba muhusika hakutaka kufuata hilo na kuweka habari kuwa Eng Ibrahim Mtolera kizimbani kwa habari za uongo na uchochezi. Inasikitisha sana kiukweli.

Nimejiandaa na najipanga sasa ili niweze kuona wanasheria wanasema vipi juu ya hili

Kwa upande wangu nawapa pole wahusika lakini tuache tabia ya kutishana na kuombeana mabaya

Pole sana ndugu yangu kwa kutuhumiwa lakin ukweli tunao sisi tuliofikwa na haya ni vyema ukachukua hatua lakin pia co kweli tbc 1 ni chombo ambacho kinaweza toa habari ambazo zina ukweli siku zote juu ya hii habari wamepotoshwa na wao wameichukua kama ukweli na ndo maana wameirusha pasipokuwa na uhakika na ndo maana tumeelezea hapa jf kilichotokea monduli
 
Pole sana ndugu yangu kwa kutuhumiwa lakin ukweli tunao sisi tuliofikwa na haya ni vyema ukachukua hatua lakin pia co kweli tbc 1 ni chombo ambacho kinaweza toa habari ambazo zina ukweli siku zote juu ya hii habari wamepotoshwa na wao wameichukua kama ukweli na ndo maana wameirusha pasipokuwa na uhakika na ndo maana tumeelezea hapa jf kilichotokea monduli

kwanza nikupe pole kwa yote yaliyotokea na hii inatokana na mfumo mzima wa uendeshaji wa mambo hapa tanzania,tunahitaji mabadiliko ya hali ya juu,tuliona kesi ya muro walitumia hadi CCTV CAMERA lakini mwisho wa siku ukweli ukajulikana.

Kinachonishangaza mimi ni pale mtu ninae mheshimu kumtumia mtu mwingine na kutengeza habari na kuiweka ktk mitandao kuwa mimi ndie niliye sambaza habari za uongo na uchochezi juu ya waandishi kukamatwa na rushwa,sikai tanzania,sikuwepo siku hiyo,nimesikiliza TBC1 na kuipeleka habari mabadiriko na wanabidii kwa kile nilicho kiona ndani ya TBC1,sasa leo imetolewa habari hiyo silioni jina langu naona la TBC na JF,lakini ukienda wanabidii wameweka kichwa cha habari kabisa kuwa mimi ndio msema uongo na mchochezo,imenisikitisha sana,namheshimu huyo anayewatumia hao kuweka habari hizo na kamwe mpaka naenda kaburini sitakuja lipiza kisasi na mwachia mungu ndie atakae weza kujibu maombi yangu

tupo pamoja mkuu ni mategemeo yetu kuwa mahakama itatenda haki
 
engmtolera habari ya wewe kuambiwa umepelekwa kizimbani kwa uchochezi zilikuwa wapi, humu JF ama kwenye forum zingine?
 
Last edited by a moderator:
engmtolera habari ya wewe kuambiwa umepelekwa kizimbani kwa uchochezi zilikuwa wapi, humu JF ama kwenye forum zingine?

hazipo humu,zipo wanabidii

mwandishi wake ni
Abdalah Hamis ✆ hamisznz@gmail.com

Mwanachama maarufu wa Mitandao ya Kijamii Nchini Tanzania anayeishi
Japan Eng Ibrahim Mtolera AKA Ilham Solar amefunguliwa kesi ya
kusambaza habari za uwongo na uzushi kwa njia ya mtandao kwa kutumia
Mitandao ya Kijamii
.
 
Ingawa Mobhare anaheshimika ila naona naye hakuwa makini katika taarifa hii.

i) Anamlaumu mtu wa Japan (nafkr EngMtolera) kusambaza habari wakati yeye (Mtolera) yuko mbali kana kwamba yeye yuko Bongo.
ii) Analaumu JF kwa watu kutupasha habari wakati huohuo naye akitumia uhuru huohuo kuleta habari, kunya anye kuku akinya bata...

Nafkr hisia ilitawala taarifa yako Mobhare ila hoja ya msingi tumeielewa.

Kwa kuzingatia habari na taarifa tulizopata mpaka sasa humu jamvini nami nitoe pole kwa waandishi hawa.

Uprising
 
  • Thanks
Reactions: Paw
mhandisi usiogope watalaamu wa ICT law wapo
so long uliweka source ulishajiexclude kuwa wewe sio chanzo cha habari
na pia ulitumia forum huru kutoa hiyo habari
aliekuishtaki hawezi kuwa na cause of action against you.
we relax usitishwe na vitisho panya vya na uzuri kesi iko mahakamani ukweli utajulikana mapema
 
chomete

Nimeisoma story yote na naomba kutoa yaliyo moyoni mwangu (sio lazima yawe sahihi). Hili suala ni kama ile kesi ya Muro.

Kama lilivyokuwa suala la Muro, inaonekana ni kweli kulikuwepo na uombaji wa rushwa kutoka upande wa media lakini kukurupuka kwa TAKUKURU kukaharibu kila kitu. Kama ilivyokuwa kwa Muro, kuna vitu vingi sana kwenye maelezo aliyotoa Matinyi mkubwa ambavyo havijakaa sawasawa kuni-convince kuwa TAKUKURU walimbambikia jamaa. Inaonekana rushwa iliombwa lakini mtego ukategwa vibaya.

Huu ni mtizamo wangu!

na ni mtazamo wangu pia, hapa rushwa iliombwa lakini tatizo mtego uliwekwa vibaya kwa sababu hiyo wanaweza kushinda hii kesi sio kwamba hawakuomba bali ni kukosekana ushahidi tokana na uzembe wa Takukuru.

Na Mobhare yeye kama mwandishi anajua kwamba mbwa akimuuma binadamu sio habari lakini binadamu akiuma mbwa hiyo ni habari inayostahili kuandikwa. Kwa mwandishi mahiri tena mhariri wa gazeti kama alivyo mdogo wake kutuhumiwa kwa rushwa hiyo ni habari inayostahili kuandikwa sio tu na TBC bali na magazeti na mitandao makini ya ya jamii JF ikiwa mojawapo.

Haitamsaidia mdogo wake kuandika maelezo mengi kwenye vyombo vya habari, hivi sasa kesi iko mahakamani, njia pekee ni kumafutia wakili mzuri atakaeweza kuishawishi mahakama kwa hoja iridhie kwamba hana hatia-ukizingatia uzembe wa Takukuru hilo linawezekana
 
Mobhare Matinyi anailalamikia TBC1, JF pia anamlalamikia mtanzania aishie Japan bila shaka engmtolera kwa kusambaza habari za uongo na uzushi wakati yeye mwenyewe yuko mbali sana na bongo-USA!

Kumbukumbu yangu ni kwamba Eng. Mtolera aliiripoti hapa na kuweka chanzo cha habari ambacho kilikuwa tbc1, sasa hapa sioni hoja ya Mobhare Matinyi. Kichekesho kikubwa ni kwamba anatumia mtandao wa JF kuelezea ya moyoni mwake.

Kama amezoea kule wanabidii labda wanamuonea aibu hapa JF ni tofauti kabisa. Raisi JK anapewa vidonge vyake hapa JF sembuse Mobhare ambaye ame ''stolowei''!

Hapa ni kumkoma nyani giledi. Kila member anaandika ama kuripoti kile alichokiona ama kukisikia ama anachokifahamu.
 
Hii story kali kwelikweli kanya kuku akinya bata aaa...

Poleni wanandugu mnalitetea Taifa lakini cha juu mnaweka sasa TBC1, JF na Eng Mtolera wamekosea nini? Badwel mimi ndugu yangu alipokea na akagawa mbona kakamatwa peke yake na kawataja wenzake kwenye kamati na bado kuna mambo ya Uranium na siasa za visa za jimbo lakini Mahakama itachambua kama Muro ambaye leo yupo tena TBC1.

Acheni kufanya kazi za kipelelezi au kuwatisha kina Seche. Kongola MUNGU atawasaidia kama sio makanjanja maana suala ni rushwa lakini kufuatilia cheo au elimu sio mliompa kazi
 
Maelezo yako yaweza kuwa yanathibitisha uhusika wa kuomba na kupokea rushwa, Naichukia RUSHWA na Na WACHUKIA SANA WATOA RUSHWA NA WAPOKEA RUSHWA.

Waandishi wa habari asilimia kubwa wanaomba RUSHWA na huu ndo ukweli na huyo mdogo wako aliomba rushwa ulichokifanya hapa unaleta siasa kwenye issue ya msingi unachanganya maneno kuondoa hatia, wenye akili wanajua waliomba RUSHWA mi naomba TAKUKURU walete ushahidi mzito na mwishowe AFUNGWE huyo Mwomba RUSHWA
 
Mwenye kumfahamu vizuri Masyaga, hawezi kushangazwa na alichokifanya. Mwaka juzi alisimamishwa kazi kwa kumtishia jamaa mmoja mwanajeshi mstaafu kumuandika madhambi yake gazetini. Huyo mwanajeshi alikuja pale NH kulalamika.

CEO - wakati ule alikuwa Bobby alimuagiza Mhariri Mkuu Muhingo Rweyemamu aunde tume ya uchunguzi chini ya Balinagwe Mwambungu (aliyekuwa Ombudsman wa NH) na baada ya uchunguzi tume ilipendekeza kwamba Masyga alikuwa na hatia na achukuliwe hatua ya kufukuzwa kazi.


Muhingo alikasirika sana kwa uamuzi huo wa Mwambungu kwani Mwambungu hakuagizwa kutoa pendekezo lolote, bali ni kuchunguza tu na baadaye kusema tu iwapo Masyaga alikuwa na hatia au la.

Baada ya miezi kadha in suspension, Muhingo alimrudisha kazi kinyemela kwa mstuko wa wengi pale NH.

Namchallenge aje hapa Masyaga akanushe kwamba hili halikutokea.

Nitajitahidi kuweka hapa JF ile finding ya ombudsman Mwambungu.
 
Mwenye kumfahamu vizuri Masyaga, hawezi kushangazwa na alichokifanya. Mwaka juzi alisimamishwa kazi kwa kumtishia jamaa mmoja mwanajeshi mstaafu kumuandika madhambi yake gazetini. Huyo mwanajeshi alikuja pale NH kulalamika.

CEO - wakati ule alikuwa Bobby alimuagiza Mhariri Mkuu Muhingo Rweyemamu aunde tume ya uchunguzi chini ya Balinagwe Mwambungu (aliyekuwa Ombudsman wa NH) na baada ya uchunguzi tume ilipendekeza kwamba Masyga alikuwa na hatia na achukuliwe hatua ya kufukuzwa kazi.


Muhingo alikasirika sana kwa uamuzi huo wa Mwambungu kwani Mwambungu hakuagizwa kutoa pendekezo lolote, bali ni kuchunguza tu na baadaye kusema tu iwapo Masyaga alikuwa na hatia au la.

Baada ya miezi kadha in suspension, Muhingo alimrudisha kazi kinyemela kwa mstuko wa wengi pale NH.

Namchallenge aje hapa Masyaga akanushe kwamba hili halikutokea.

Nitajitahidi kuweka hapa JF ile finding ya ombudsman Mwambungu.
kwanza unatumia jina ambalo halifanani na hoja yako, unajiita marksman wakati umeshindwa hata kulenga ukweli wa unalolisema. hakika ukubwa wa mwili si hoja.

Go back to Mwambungu, get his report. Kama kuna mapendekezo unayoyasema yaweke hewani. Pia namfahamu Masyaga sana sana, huyo mwanajeshi mstaafu ni nani.

Kazi njema mpiganaji a.k.a. Marksman.
 
Haya mapambano dhidi ya udhalimu wa rasilimali zetu yana safari ndefu sana. Hata kama mtu ana mapungufu yake lakini kwa hili Takukuru wamechemka na wametumika na wakatumika vibaya bila kufanya kazi kitaaluma.

Wakiendelea hivi watapoteza imani kwa umma na kwa kweli wanawaacha wezi na mafisadi wakubwa wanahangaika na kuwalinda wezi na wahujumu uchumi. Ziko wapi kesi za twiga, kesi za meremeta, kagoda, Rada, Richmond, Kiwira, na kadhalika?

Takukuru wanatia aibu sasa.

Hivi Mhariri mzima atoke Dar kufuatilia mtumishi wa Tanesco ngazi ya wilaya hii inaingia akilini kweli?
 
Ni kweli na swala hapa tusimshambulie mobhare kwa kuteleza kuiandika jf vibaya.

cha msingi hapa tueleze kwa nn takukulu wanatetea mafisadi wezi wa mali za nchii hii alafu wanakuja kupambana na watu duni kama mimi ambaye sina hata sauti kwenye nchi hii hata sifahamiki.
Na pasipo wao kufikili juu hili kuwa ni uzembe na kutokuwa makini ndo wa kwanza kusema wamefanya kazi nzuri sana.

Nikikumbuka kauli alizokuwa anatoa Shirima ambaye ni afisa TAKUKURU hakika nashanga sana
chomete unaweza kutueleza kwa maneno yako wewe uliingiaje katika skata hilo hadi ukawepo katika eneo husika, uhusiano wako na Matinyi n.k ili tpate kupima vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Mobhare ulicho kielezea hapa ni ukweli mtu na mimi ndo mmoja wapo na mimi ndiye niliye lazimishwa kupokea hiyo rushwa hakika nilipambana sana ingawa nilipokea kipigo kikali sana mpaka nikafikia hatua ya kusema kwa nini mnaniua kwa kunipiga kwa kitu ambacho mnanibambikizia.

Hawa waajiriwa wa TAKUKURU wengi walikuwa waalimu waliokosa kazi au vijana waliomaliza shule/chuo, wengi wao hawajui kazi yao na huishia kulazimisha watu wapokee pesa kwa kuwapiga na wakienda mahakamani huishia kushindwa kesi.

Niliwahi ona kesi yao moja kichekesho, wao walidanganywa na mzee mmoja kuwa daktari anataka rushwa ili amjazie fomu zake za ajali (Kugongwa na gari), wakachukua pesa wakampa huyo mzee ili akampe huyo daktari kiasi alichoomba, bahati mzuri wakaenda naye na kuweka mtego wao njiani mahali palipokuwa na watu wengi tu, yule daktari alipofika kabla ya kuingia ofisini akadakwa na yule mzee kuwa nimekuja na kile kiasi ulichosema, Daktari akajibu kwa sauti kubwa tu nenda kalipie Dirishani,(ilikuwa asubuhi lakini Dr alitoka kuzimua nje ya geti) mzee akakataa katakata kuwa yeye ni mgonjwa wa miguu hivyo akaendelea kuomba msaada wa Daktari aende akamlipie, baada ya mabishano marefu mbele za watu yule daktari akawa na huruma akachukua ile pesa ili aende kumkatia receipt, kooooosa wakamkamata, bila kuangalia na kuweka maanani kuwa kuna watu ambao walisikia jinsi daktari alivyotoa maelekezo mazuri tu ambayo wao nao walipashwa wajue mapema kuwa kumbe pesa iliyoombwa ni haki na sio rushwa.

Kwa ujumla TAKUKURU wengi hawajui kazi yao ukijumlisha na Bosi wao aliyetudanganya ya RICHMOND/RADA... etc
 
pole sana chomete vp lakini unaendeleaje kiafya? Ripoti yako ya Dr. umeitunza ili ikusaidie mahakamani
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom