Sasa hapo nimeelewa tatizo kubwa la ndani ulilo nalo. Dr Stephen Ulimboka ni daktari kitaaluma na anafanya kazi yake ya kutibu wagonjwa lakini pia ni MWENYEKITI wa jumuia ya madaktari. Wewe kazi unayoifanya ya afisa habari ni ya KITAALUMA, ila unaweza kuwa Mwenyekiti wa UVCCM kwa mfano kwa sio kazi ya kitaaluma.
Pia sasa nimeelewa kuwa hata majukumu yako inawezekana huyajui. Kuwa fair kwa wanaCCM wenzio ingekuwa vizuri ungeweka na JOB DESCRIPTION yako hapa ili wajiridhishe na kuona ni aina gani ya kazi utakuwa unazifanya. Ila zingatia sana ushauri wangu bwana mdogo, kwa umri wako itafikia kuwa na familia, utapata watoto ambao watahitaji kusoma, tena katika shule nzuri tu. Lazima uwaze kuhusu maisha yako ya baadaye kwa kuwa na Job Security, hizi kazi za kupeana zawadi ni mbaya. Kwa mfano siku inatokema Mwigulu aliyekupa hiyo kazi anakuomba JICHO kwa mfano, na ukimpa jicho lako hutaona tena, lakini ukimnyima unarisk nafasi yako, utabaki njia panda na kujutia maisha yako. Njia nzuri ya maisha yako mdogo wangu ni kumuomba akusaidie upate shule ya kufundisha hapa Dar, piga kazi ya ualimu huku ukifanya siasa kama Party time. Kuna leo na kesho mdogo wangu.