Jamal Akbar
JF-Expert Member
- Oct 9, 2014
- 413
- 471
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya, Geofrey Sarakikya, amesema mfanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara Emmanuel Chacha, aliyefariki dunia Machi 11, mwaka huu hakupigwa risasi.
Aliyasema hayomkoani Mara, wakati akitoa ufafanuzi kuhusu kifo cha Chacha, ambapo alisema alifariki dunia baada ya kujirusha katika shimo lenye urefu wa mita 20.
"Hiyo ni kwa mujibu wa maelezo ya watu waliokuwepo eneo la tukio na majibu ya matokeo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu uliofanywa na daktari wa Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza, zimebainisha kifo chake kimetokana na majeraha yaliyotokana na kujirusha kwenye shimo lenye urefu wa mita 20,"alisema.
Kamanda Sarakikya alisema kabla ya kujirusha katika shimo hilo, kikosi kazi kilimkuta mfanyakazi huyo akiiba mawe yanayodhaniwa kuwa na dhahabu ndani ya mgodi huo.
Alisema kikosi kazi kilijumuisha ofisa madini wa mkoa, maofisa kutoka Jeshi la Polisi, kitengo cha ulinzi cha mgodi na kampuni ya ulinzi ya Nguvu Moja.
Aidha, Kamanda Sarakikya alisema taarifa zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii zikidai aliuawa kwa kupigwa risasi hazina ukweli.
"Kwa hali hiyo ni vyema ifahamike taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa kifo cha Emmanuel Chacha kilitokana na kupigwa risasi, siyo za kweli," alisema Kamanda Sarakikya
Kamanda Sarakikya alitoa ufafanuzi huo kutimiza ahadi aliyoitoa Machi 12, mwaka huu ambapo aliahidi angetoa taarifa kamili ya kifo hicho baada ya kupata majibu ya daktari kuhusu uchunguzi wa mwili wa marehemu.
Katika taarifa yake ya awali, alisema kifo hicho kilitokea Machi 11, mwaka huu katika eneo la Gokona ndani ya mgodi wa Barrick North Mara.
Aliyasema hayomkoani Mara, wakati akitoa ufafanuzi kuhusu kifo cha Chacha, ambapo alisema alifariki dunia baada ya kujirusha katika shimo lenye urefu wa mita 20.
"Hiyo ni kwa mujibu wa maelezo ya watu waliokuwepo eneo la tukio na majibu ya matokeo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu uliofanywa na daktari wa Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza, zimebainisha kifo chake kimetokana na majeraha yaliyotokana na kujirusha kwenye shimo lenye urefu wa mita 20,"alisema.
Kamanda Sarakikya alisema kabla ya kujirusha katika shimo hilo, kikosi kazi kilimkuta mfanyakazi huyo akiiba mawe yanayodhaniwa kuwa na dhahabu ndani ya mgodi huo.
Alisema kikosi kazi kilijumuisha ofisa madini wa mkoa, maofisa kutoka Jeshi la Polisi, kitengo cha ulinzi cha mgodi na kampuni ya ulinzi ya Nguvu Moja.
Aidha, Kamanda Sarakikya alisema taarifa zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii zikidai aliuawa kwa kupigwa risasi hazina ukweli.
"Kwa hali hiyo ni vyema ifahamike taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa kifo cha Emmanuel Chacha kilitokana na kupigwa risasi, siyo za kweli," alisema Kamanda Sarakikya
Kamanda Sarakikya alitoa ufafanuzi huo kutimiza ahadi aliyoitoa Machi 12, mwaka huu ambapo aliahidi angetoa taarifa kamili ya kifo hicho baada ya kupata majibu ya daktari kuhusu uchunguzi wa mwili wa marehemu.
Katika taarifa yake ya awali, alisema kifo hicho kilitokea Machi 11, mwaka huu katika eneo la Gokona ndani ya mgodi wa Barrick North Mara.