Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
wandugu mwenye kujua ukweli wa hii kampuni ya CA TRADE CAR VIEW ya japan inayohusika na kuuza used car kutoka japan naomba unipe uhakika wa hii kampuni isije ikawa ni matapeli wa nigeria wanatumia mtandao kutaka kutapeli pesa . nia yangu ni kuagiza gari kupitia kampuni yao. kama yupo aliyewahi kuitumia hii kampuni tafadhali naomba anipe uhakika
Ni kampuni nzuri ya kutangaza magari yanayouzwa kama yalivyo mengi na malipo hupitia kwao, na magari yao huuzwa "As Is." Kama gari ikifika utaona matatizo yanaanza kukusumbua kichwa hawahusiki maana biashra ukishalipa mnaachana we shughulia na tolori lako kulitengeneza kama hukufanya uhakiki kabla ya kununua.
Note:
Nilipotaka kununua gari kupitia kwao nilishangaa kuona kuna nyongeza ambazo awali hazikuainishwa kwenye bei ya kununulia na kusafirisha
Picha ya gari inapendeza lakini hakuna uhakika na ubora wa gari kwa vile mfanya biashara anachotaka ni gari yake iuzike apate chake.
Kuna gharama za kawaida ambazo ni shipping, inspection, bima, lakini kuna makampuni utashangaa yanakuongezea gharama zaidi ambazo hazikuainishwa awali katika matangazo yao.
Nilichofanya:
Kupata kampuni inayojitangaza huko Trade car view ambayo mtu atafanya uhakiki wa ubora wa gari ninayokusuda kuuza, kwa kuwa magari mengi ni used na yanauzwa as is.
Kwa bahari rafiki yangu mmoja anafanyia kazi moja ya makampuni hayo ni mtanzania, tumesoma pamoja na kuwa friends muda mrefu aliyeko huko huko Japan ndiye aliyenisaida kupata gari bora sana ambalo wengi walishangaa kwa bei niliyonunua na linavyoonekana moto wa kuotea mbali.
Watanzania wengi huangalia mradi kuwa na gari bila kuangalia ubora, ni jambo ambalo nawaangalisha wengi, maana mimi jasho langu huwa sipendi lipotee kwa uzembe, maana mtu kufikia kukusanya za kununua gari ujue amejifunga ukanda na kupangua yasiyo lazima ili kujaza kibaba.
Jambo la msingi bora uwe na mtu ambaye anafanya inspection kwa ajili ya kukuhakikishia ubora, maana kutumiwa gari tu kesho ukishatumia wiki moja matatizo mengi yanaanza kukumiza kichwa kama transmission nk. nini sababu ulitazama mvuto wa umbile na rangi bila kuangalia mambo ya ndani kama ina ubora huenda imechakachuliwa katika kutangaza biashara.
Wenye bahati wanabahatika kupata magari mazuri na wengine inakula kwao, na hata pengine kusihia pesa kuota mbawa kwani ninayo mifano ya uhakika katika hilo, hapa tusiongope tuwe wakweli, maana pesa kama umeitokea jasho unahitaji kupata chambo kitakachokusaidia muda wa kutosha vinginevyo litakuwa pambo nyumbani una gari usiloweza kutoka nalo hata mita moja.
Kama uko Tanzania, na kabisa jiji la Dar es Salaam, nenda Mikocheni pale Shoppers Center kuna kampuni tanzu ya LUCUS Japan ambao hutumia pia mtandao huo huo wa Trade Car View, watakusaidia kuchagua gari na mambo mengine na hata pesa utailipia pale kwao. Lakini wanataka uachie kitu wakati mwingine kama posho ya uagizaji. Ukitaka nikupe anayeweza kukufanyia ukaguzi wa kupata gari moja zuri ambaye anafanya kampuni hiyo hiyo aliyeko Japan, please PM me nitakuunganisha. Note mimi sifanyi biashara hiyo, itakuwa kukusaidia mdau wa JF.
Uwe mwangalifu, humu kuna wafanyabiashara wa magari, wanakuvutia lakini uwe makini na kuwa na jicho la ziada kusoma comments za watu.