Wanasema na makato ni makubwa 18% ya kile uuzacho
punguzo umekuja na wazo zuri. Mimi najiuliza swali moja. Je nisababu zipi za msingi zinaziwafanya wafanya biashara wagome kutumia hizo mchine. Je ni kwasababu ya bei zake (initial cost) au kwavile wanajua kuwa utaratibu huu utawafanya wajulikane kipato chao basi hawataki kuzitumia. Je ni kwavile hawaoni faida ya wao kulipa kodi na hivyo kutafuta mwanya wa kuendelea kukwepa kulipa kodi?
Kuna vitu viko wazi ambavyo mimi naviona. Ukusanyaji wa kodi kwa TRA bado upo kwa kiwango cha chini, cha kusikitisha hata hicho kidogo kinachokusanya ni kiwango kidogo kinachofanya kazi za maana/kinachotumiwa kwa maendeleo. Kiasi kikubwa kinaishia mikononi mwa wachache kwa njia za deal deal. Na hiyo inawafanya watu wasione umuhimu wa kulipa kodi.
Pili hata wale wenye EFD tayari bado hawazitumii inavyotakiwa. Utakuta bado wanatumia risti zao za zamani au hatoi risti kabisa. Na mara nyingi sana na hii imenitokea mara kibao wafanya biashara anakwambia bei ya kifaa hiki ni mfano laki 7 ukitaka risti au laki 5.5 bila risti. Mteja yoyote atakimbilia kuchukua bidhaa bila risti na mwisho wa siku mfanya biashara ananufaika kwa kukwepa kodi. Lakini ki u-halisia huwa wanaongeza bei kumtisha mteja na hivyo kusababisha mteja akubali kutochukua risti. TRA needs to workout that, vinginevyo mtakuwa na hizo EFD lakini bado efficiency yenu ya kukusanya kodi itakuwa ndogo. Usahauri wangu kama zipo machine zinazoweza kupatikana kwa bei ndogo kama ulivyo pendekeza itakuwa ni jambo zuri. Lakini pia wanaweza kuwakopesha wafanya biashara na wakawa wanawakata hela yao kidogo kidogo hadi itakapo isha. Tusilazimishe kununua machine hizo kwa hela ndefu hivyo. Si kila mfanya biashara anahela ya kutoa kwa haraka na hasa anapogundua kuwa hicho kifaa hakimsaidi kama wanavyoelezwa eti kutunza kumbukumbu. Ingekuwa kweli wao wanaona kitawasaidia basi wangekimbilia, kumbukumbu zao wanazo ila huwa wanajaribu kuzificha na kwasababu TRA hawanauwezo wa kuzipata hujikuta wakiwakadilia malipo kidogo ya kodi licha ya kwamba utaona wengi wanalalamika kama vile wamekadiliwa kwa kiwango cha juu.
Wito wangu: Serikali ijitahidi kutumia vizuri kodi za wananchi, hii itawafanya wananchi ambao ndo walipa kodi waone kwamba kodi yao inatumika vizuri. Binafsi huwa nasikitika naposikia watu wamepiga hela za miradi flani, au wanafanya ubadhilifu, au wanatumia vibaya magari ya serikali. Wanafanya uchakachuzi katika sekta mbalimbali huwa nasikitika sana. Najua mwisho wa siku sisi ndo tunaumia maana hizo ni kodi zetu. Ukweli ni kwamba kama wafanyakazi wa nchi hii nao wangekuwa na option ya kukwepa kulipa kodi ya mapato (pay as you earn) watu wasingelipa. Hakuna mtu anayegoma kulipia huduma na hasa anapoona huduma zinzotolewa ananufaika nazo.
Watu hawana hospitali, viongozi wanakimbizwa nje wanapougua, shule zetu zinakwisha watoto wa viongozi wanasomeshwa nje au shule private nzuri. Barabara mbovu, tembelea maeneo wanapokaa wao. Huduma za maji na umeme mbovu kwao wanapata masaa yote. Sasa mtu anajiuliza kwanini nilipe kodi. Kwanini nami nisifanye saving itakayo nisaidia baadaye nitakapo ihitaji.
Hivi wewe ni mwanaume au mwanamke!!!!!
Hebu weka wazi ujulikane nia yako maana kila unapokuja mjadala wa EFD lazima ulete mada ya ku divert attention kuwa kuna ajenda ya siri,au wafanya biashara hawataki kulipa au kuwa wafanyakazi wanakatwa na mambo kama hayo!!!!!!
Jua kitu kimoja kuwa hawaTRA ndio wanajukumu la kuondoa ambiguities zote hizo unakurupuka nazo kwa kuwekeza wao katika muundombinu huu ili tumalize hili suala tufuate ajenda nyingine za manufaa ya nchi!!!!!!
Umeagizwa na nani na.unalipwa shilingi ngapi,if I may buy you out madam!!!!!!
So that we(without you) can pave the way for a more brighter and sustainable means to build this Nation!!!!!
Mkuu issue sio bei coz bei TRA inakuja kufanya setoff kwenye kodi,,so hakuna mfanyabiashara hata mmoja atakayelipa kutoka hela yako mfukoni,,tusifuate mkumbi wakubwa na wala kulishwa sumu na hawa wakwepa kodi,,,issue hapa ni kuthibiti wakwepa kodi,,,they are damn rich kwa sababu ya kukwepa kodi na gap la masikini na tajiri linazidi kuongeza kwa sababu hiyo.issue sio tulia kodi mkuu, issue ni bei ya efds kuwa juu. umeelewa?
Kwa hizo mashine zimefungwa kamera ili kujua ni kitugani kimetok na kipi kimeingia? Kama jibu ni hapana wizi utakuwa palepale watauza na hawatatoa risti.
Hii issue kweli wafanyabiashara wameamua kuipotosha...issue sio bei za machine coz hizo bei ni TRA wenyewe ndio wanaolipia kupitia makato ya kodi...hakuna mfanyabiashara anae nunua ile mashine kwa hela yake mkononi....ni TRA ndio itakayofanya setoff kwenye kodi....wakubwa msirukie mada kabla ya kuielewa vzr na kuanza kulaumu...huu ukwepaji kodi hauvumiliki....its time kila mtu alipe kodi sasa.
Ndo manake mkuuKwahiyo wanapewa Bure?
Jamani ndio maana mijadala mingi inakosa lengo kuu.Hapa tuache kujadili tatizo la wafanyabiashara kutolipa kodi maana ni mjadala mpana sana.Mada kuu ni gharama za EFD na sijasikia popote wafanyabiashara wakigoma kulipa kodi zaidi ya uzembe wa TRA tu na mfano mimi nayafahamu makampuni tena makubwa ambayo hata assessment ya kodi haijawahi kufanyika yaani kampuni inajilipia tu kodi itakavyo!
Mjadala ni bei za machine za EFD na sio ukwepaji kulipa kodi. Tusipoteze uelekeo wa mjadala huu.
issue sio tulia kodi mkuu, issue ni bei ya efds kuwa juu. umeelewa?
Something is behind this mgomo...but the bottom line is TRA ikicheka na wafanyabiashara hakuna kodi itakayokusanywa....hawa sio watu wa kuwachekea kabsa...pamoja na vipato vyetu vya chini wafanyakazi tumelipa kodi sana....tuanze kugawana maumivu sasa na kuongezwa tax base kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii.
Wabongo tumezoea sana wizi na kukwepa, wafanya biashara wamezoea super profit, kwa vile sasa mashine zitaonyesha kila kitu, nanataka kuzigomea!. Mbona wahindi wanazitumia na hawagomi?!.
Anayelipa kodi ni end user, hivyo anayepaswa kugoma ni mteja baada ya kupandishiwa bei kufuatia wafanya biashara kulipa kodi!, na sio wafanya biashara wagome kuuza, kisa kodi iko juu!. Huu sasa ni mwanzo mzuri wa hivi vibiashara mchoro mchoro vifungwe zibaki biashara halali tuu!.
Kwa upande wa EFD, nako ni wizi mtupu!, mashine inauzwa dola 100, hapa unauziwa dola 1000!.
Ukiamua kununua mwenywe, wale maajent wa TRA hawakubali ku install!.
Mijimashine yenyewe approved kwa Tanzania yote inatumia windows only kwa sisi tunaotumia mac, tunalazomika kununua computer ya window kwa ajili ya EFD tuu!.
Huu pia ni nyanyasaji!.
Pasco.
Pasco.
punguzo umekuja na wazo zuri. Mimi najiuliza swali moja. Je nisababu zipi za msingi zinaziwafanya wafanya biashara wagome kutumia hizo mchine. Je ni kwasababu ya bei zake (initial cost) au kwavile wanajua kuwa utaratibu huu utawafanya wajulikane kipato chao basi hawataki kuzitumia. Je ni kwavile hawaoni faida ya wao kulipa kodi na hivyo kutafuta mwanya wa kuendelea kukwepa kulipa kodi?
Kuna vitu viko wazi ambavyo mimi naviona. Ukusanyaji wa kodi kwa TRA bado upo kwa kiwango cha chini, cha kusikitisha hata hicho kidogo kinachokusanya ni kiwango kidogo kinachofanya kazi za maana/kinachotumiwa kwa maendeleo. Kiasi kikubwa kinaishia mikononi mwa wachache kwa njia za deal deal. Na hiyo inawafanya watu wasione umuhimu wa kulipa kodi.
Pili hata wale wenye EFD tayari bado hawazitumii inavyotakiwa. Utakuta bado wanatumia risti zao za zamani au hatoi risti kabisa. Na mara nyingi sana na hii imenitokea mara kibao wafanya biashara anakwambia bei ya kifaa hiki ni mfano laki 7 ukitaka risti au laki 5.5 bila risti. Mteja yoyote atakimbilia kuchukua bidhaa bila risti na mwisho wa siku mfanya biashara ananufaika kwa kukwepa kodi. Lakini ki u-halisia huwa wanaongeza bei kumtisha mteja na hivyo kusababisha mteja akubali kutochukua risti. TRA needs to workout that, vinginevyo mtakuwa na hizo EFD lakini bado efficiency yenu ya kukusanya kodi itakuwa ndogo. Usahauri wangu kama zipo machine zinazoweza kupatikana kwa bei ndogo kama ulivyo pendekeza itakuwa ni jambo zuri. Lakini pia wanaweza kuwakopesha wafanya biashara na wakawa wanawakata hela yao kidogo kidogo hadi itakapo isha. Tusilazimishe kununua machine hizo kwa hela ndefu hivyo. Si kila mfanya biashara anahela ya kutoa kwa haraka na hasa anapogundua kuwa hicho kifaa hakimsaidi kama wanavyoelezwa eti kutunza kumbukumbu. Ingekuwa kweli wao wanaona kitawasaidia basi wangekimbilia, kumbukumbu zao wanazo ila huwa wanajaribu kuzificha na kwasababu TRA hawanauwezo wa kuzipata hujikuta wakiwakadilia malipo kidogo ya kodi licha ya kwamba utaona wengi wanalalamika kama vile wamekadiliwa kwa kiwango cha juu.
Wito wangu: Serikali ijitahidi kutumia vizuri kodi za wananchi, hii itawafanya wananchi ambao ndo walipa kodi waone kwamba kodi yao inatumika vizuri. Binafsi huwa nasikitika naposikia watu wamepiga hela za miradi flani, au wanafanya ubadhilifu, au wanatumia vibaya magari ya serikali. Wanafanya uchakachuzi katika sekta mbalimbali huwa nasikitika sana. Najua mwisho wa siku sisi ndo tunaumia maana hizo ni kodi zetu. Ukweli ni kwamba kama wafanyakazi wa nchi hii nao wangekuwa na option ya kukwepa kulipa kodi ya mapato (pay as you earn) watu wasingelipa. Hakuna mtu anayegoma kulipia huduma na hasa anapoona huduma zinzotolewa ananufaika nazo.
Watu hawana hospitali, viongozi wanakimbizwa nje wanapougua, shule zetu zinakwisha watoto wa viongozi wanasomeshwa nje au shule private nzuri. Barabara mbovu, tembelea maeneo wanapokaa wao. Huduma za maji na umeme mbovu kwao wanapata masaa yote. Sasa mtu anajiuliza kwanini nilipe kodi. Kwanini nami nisifanye saving itakayo nisaidia baadaye nitakapo ihitaji.
Something is behind this mgomo...but the bottom line is TRA ikicheka na wafanyabiashara hakuna kodi itakayokusanywa....hawa sio watu wa kuwachekea kabsa...pamoja na vipato vyetu vya chini wafanyakazi tumelipa kodi sana....tuanze kugawana maumivu sasa na kuongezwa tax base kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii.