Binti wa zamani
Platinum Member
- Nov 19, 2011
- 11,763
- 27,149
Acha nianze:
- Maisha hayana huruma - unaweza kufanya kila kitu kwa ubora na kama inavyotakiwa na bado ukafeli.
- Ukimya ni jibu - jifunze kunyamaza na kucontrol hisia zako, itakupunguzia matatizo mengi ambayo si ya lazima.
- Watu watakuja na kuondoka kwenye maisha yako, ni mzunguko wa asili. Usije kufanya kosa la kung’ang’ania mtu ambaye muda wake kwenye maisha yako umekwisha.
- Vifo vya watu unaowapenda, vitakuumiza kwa muda mrefu kuliko utakavyorajia.
- Pesa haitakupa furaha ila itakuheshimisha na kukurahisishia maisha.
- Ukiwa mtoto wa kwanza kwenye familia kubwa, maisha yako hayatokua na mapumziko, utategemewa na kila mtu anayekuzunguka mpaka kifo chako.
- Familia ambazo wazazi wetu wanatokea (wajomba, mababa wakubwa, mama wadogo, mashangazi etc.) ni watu wa kuishi nao kwa busara sana au kukaa nao mbali.
Endelea ....................