Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Baba jayaron

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2015
Posts
4,580
Reaction score
6,279
Habari wana jamvi,

Kama kichwa kisemavyo,

Huu ukuta wa Mererani ulioagizwa na Mh Magufuli umezua utata kwa namna ulivyopokelewa hasa na washikadau wa shughuli husika za madini.

Kwanza wameshangaa kutolewa maamuzi ya namna ile ambayo kwayo wamesikitika kwamba kwanini nguvu hio na gharama hizo wasingejenga barabara sehemu zenye uhitaji.

Wakaenda mbali zaaidi juu ya washauri wa mh. Magufuli kana kwamba elimu yao ni yakinadharia tuu imewanyima ujuzi wa uhalisia kufikia maamuzi yasiyo na tija au wanaamua kumpotisha tuu mh. Magufuli.

Wanasema kama mh. Magufuli hawajui wachimba madini na wadau wake atakuja shtuka shimo linachimbwa mererani wanapolo wanatokea Arusha au hata chumbani kwa mtu na hapo ndo hasara ya kamera itakapo onekana, pia patakua na njia nyingi tuu za kufanikisha wizi kwa serikali kama serikali haitokuja na sera rafiki, shirikishi katika ukusanyaji kodi.

Mimi ni mzalando!!
 
Ukuta utazuiaje uchimbaji na utoroshaji wa madini?

Kikawaida, wanapolo safari zao ni chini kwa chini. Ndo maana wengi tulitaka more details kuhusiana na huo ukuta.

Kama ni kuzuia wauzaji wasitoroshe, ukuta peke yake hautasaidia.
 
Habari wana jamvi,

Kama kichwa kisemavyo,

Huu ukuta wa mererani ulioagizwa na mh Magu umezua utata kwa namna ulivgopokelewa hasa na washikadau wa shughuli usika za madini,

Kwanza wameshangaa kutolewa maamuzi ya namna ile ambayo kwayo wamesikitika kwamba kwann nguvu hio na gharama hizo wasingejenga barabara sehemu zenye uhitaji.

Wakaenda mbali zaaidi juu ya washauri wa mh. Magu kana kwamba elimu yao ni yakinadharia tuu imewanyima ujuzi wa uhalisia kufikia maamuzi yasiyo na tija au wanaamua kumpotisha tuu mh. Magu.

Wanasema kama mh. Magu hawajui wachimba madini na wadau wake atakuja shtuka shimo linachimbwa mererani wanapolo wanatokea Arusha au hata chumbani kwa mtu na hapo ndo hasara ya kamera itakapo onekana, pia patakua na njia nyingi tuu za kufanikisha wizi kwa serikali kama serikali haitokuja na sera rafiki, shirikishi katika ukusanyaji kodi.

Mimi ni mzalando!!

Walitakiwa kujenga Ukuta wa sheria za kuhakikisha madini yanafuata proper channels,siyo ukitaka wa Cement ya wazo.Hahahhahaha
 
Hii inanikumbusha wapalestina walivyochimba mahandaki chini kwa chini katika mpaka wake na Egypt. Hawa wachimbaji wadogo watachimba chini ya huo ukuta kutafuta Tanzanite.
Mradi huu ni upotevu wa pesa. Cha msingi serikali ingeanza kuwatoza kodi wachimbaji wote kutokana na eneo la vitalu vyao
 
Bado anasimuliwa kuhusu Arusha kuwa imebadilika, ila kibwagizo natumai alikiona siku aliyotokwa matusi, sasa picha kamili subirini hilo la mererani, hasipotukana ya nguoni na viungo vya siri sijui.
 
Hamna binadam mwenye mbinu za kjanja kama mTz hasa upande wa pesa ...yaani mchimbaji huwezi kumzuia kwa kutumia camera na ukuta hasa kweny madini yenye thamani kama tanzanite ambayo hayana process kubwa zaidi ya sorting tu huwez linganisha na dhahabu,hvyo itakuwa ngumu sana...tupunguze mawazo ya kukurupuka tujaribu kwenda na uhalisia
 
Habari wana jamvi,

Kama kichwa kisemavyo,

Huu ukuta wa mererani ulioagizwa na mh Magu umezua utata kwa namna ulivgopokelewa hasa na washikadau wa shughuli usika za madini,

Kwanza wameshangaa kutolewa maamuzi ya namna ile ambayo kwayo wamesikitika kwamba kwann nguvu hio na gharama hizo wasingejenga barabara sehemu zenye uhitaji.

Wakaenda mbali zaaidi juu ya washauri wa mh. Magu kana kwamba elimu yao ni yakinadharia tuu imewanyima ujuzi wa uhalisia kufikia maamuzi yasiyo na tija au wanaamua kumpotisha tuu mh. Magu.

Wanasema kama mh. Magu hawajui wachimba madini na wadau wake atakuja shtuka shimo linachimbwa mererani wanapolo wanatokea Arusha au hata chumbani kwa mtu na hapo ndo hasara ya kamera itakapo onekana, pia patakua na njia nyingi tuu za kufanikisha wizi kwa serikali kama serikali haitokuja na sera rafiki, shirikishi katika ukusanyaji kodi.

Mimi ni mzalando!!
Duu kweli we "mzalando "!!
 
Mimi niliwahi kuchimba madini huko mererani, nilikuwa najaribu kujiuliza ukuta utasaidiaje? nikawa sipati picha. Labda kama huo ukuta unaweza kupunguza wizi. Sikushangaa sana kwani rais wetu anapenda kudhibiti au kulinda kwa mtazamo wake. Lakini anakosa mbinu sahihi au wanaomshauri wanamshauri anachowashauri wao.

Nilishangaa ili siku aliposema kesho jeshi likaingia na mkwara mkubwa utafakiri ni jambo lenye tija sana. Nimewahi kushauri mara nyingi humu, badala ya jeshi kukaa tu bila kuzalisha mali wakati huu wa amani, ni bora lipewe mashamba makubwa ya kulima kwa kupewa pembejeo kama tractors, combine harvestors, mbolea nk. wazalishe kwa wingi kisha wananchi tunaolima kwa nguvu zetu tuachwe tuuze tunapotaka. Hayo ya jeshi ndio yakajazwe kwenye maghala ya serekali kwa ajili ya njaa na kutunza bei elekezi. Lakini nimeona jeshi limeenda kama roketi kujenga ukuta wakati kama ni madini ndio yako ukingoni. Usishangae ndani ya mwaka huo ukuta ukaanza kuweka ufa kwani sidhani hata kama feasibility study imefanyika. Anyway ndio rais wetu huyo nia njema lakini hana mbinu.
 
Msubiri ujengwe kwanza.. mengine baadae hayo ya kirafiki waandikieni barua mueleze yenu. Endelea kuandika mnafikiria kufanya nini ukuta ukisimama.. inapendeza sana sana na msifikiri nao hawajui maujanja.
 
mkuu cha kwanza ni kulinda raslimali zetu kwanza.....kejeli na kelele hizo zipo tuu.
Nia ni nzuri laki madini si kama kuangua nazi kwamba mkwezi anaonekana tangia anavyo panda hadi kushuka ,kwa hili imetumika akili ndogo niwe mkweli tu
 
Back
Top Bottom