Ukosefu wa Usawa katika Mikopo ya Kibiashara

Ukosefu wa Usawa katika Mikopo ya Kibiashara

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Ni jambo la kushangaza na lenye kuibua maswali makubwa kuhusu usawa katika mazingira ya biashara kati ya Tanzania na China. Mfanyabiashara wa China anapokopa katika benki za kibiashara nchini kwao hulipa riba ya takribani asilimia 3 pekee.
images (64).jpeg

Lakini mfanyabiashara wa kitanzania anapokopa katika benki za kibiashara za Tanzania, anakabiliana na riba ya wastani wa asilimia 17. Hii ni tofauti kubwa ya asilimia 14.
images (63).jpeg

Je, katika mazingira haya, mfanyabiashara wa Tanzania anawezaje kushindana na Mchina ambaye mara nyingi hujificha nyuma ya mgongo wa Mtanzania kuendesha biashara zake? Ni wazi kuwa mfumo huu unawaweka wafanyabiashara wetu katika wakati mgumu, ukipunguza uwezo wao wa kushindana na kuendelea kibiashara. Swali la msingi linabaki: ipo wapi sera ya usawa na ulinzi kwa wafanyabiashara wa ndani?
 
Boss wangu watu wanavyopinga huu uchaguzi nyuma yake kuna mengi yanayotuumiza, hii nchi ni ngumu sana kwa maskini kutoboa vikwazo ni vingi sana mkuu sio Kodi TU na riba
 
Then who cares????

Tupambane tu tutakavyoweza tutoboe
Hizi bank za kwetu hazipo kwa aliji ya kukusaidia Bali kutimiza ndoto zao maana na wao ni biashara
 
Hebu tutajie hizo bank na mikopo ilikuwa ni ya kiasi gani?
 
Ni jambo la kushangaza na lenye kuibua maswali makubwa kuhusu usawa katika mazingira ya biashara kati ya Tanzania na China. Mfanyabiashara wa China anapokopa katika benki za kibiashara nchini kwao hulipa riba ya takribani asilimia 3 pekee.
View attachment 3470612
Lakini mfanyabiashara wa kitanzania anapokopa katika benki za kibiashara za Tanzania, anakabiliana na riba ya wastani wa asilimia 17. Hii ni tofauti kubwa ya asilimia 14.
View attachment 3470613
Je, katika mazingira haya, mfanyabiashara wa Tanzania anawezaje kushindana na Mchina ambaye mara nyingi hujificha nyuma ya mgongo wa Mtanzania kuendesha biashara zake? Ni wazi kuwa mfumo huu unawaweka wafanyabiashara wetu katika wakati mgumu, ukipunguza uwezo wao wa kushindana na kuendelea kibiashara. Swali la msingi linabaki: ipo wapi sera ya usawa na ulinzi kwa wafanyabiashara wa ndani?
Na hapo bado hujaongelea gharama za viambatanisho na kuprocess huo mkopo! Sijui barua ya mtendaji wa Kata, barua kutoka serikali ya Mtaa, viapo vya Mwanasheria, pasport size, Bima ya jengo, bado hujabambikw madeni feki ya nyuma ya mitandao ya simu! Kote huko unatakiwa utoe hela!
Kichekesho kwenye huo mkopo utashangaa na hela ya Afisa Mikopo nayo inakatwa! Na wakati huyo mtu ameajiriwa na benki na analipwa mshahara kila mwezi!

Ukigusa mikopo ya wafanyakazi! Huko ndiyo kuna wizi mkubwa mpaka basi! Riba kandamizi! Makato yasiyokiwa na kichwa wala miguu!

Kwa kweli inahuzunisha sana. Mabenki yanafilisi wafanyakazi, wafanyabiashara na wajasiriamali kwenye hii nchi mpaka inakatisha tamaa. I wish ningekuwa Rais.
 
Then who cares????

Tupambane tu tutakavyoweza tutoboe
Hizi bank za kwetu hazipo kwa aliji ya kukusaidia Bali kutimiza ndoto zao maana na wao ni biashara
Yaani umeanza na statement kwamba then who cares? halafu ukaendelea kusema tupambane tutoboe! Inaonesha kuwa kuna party inafanya ku-care bila hata kuonesha kujali?
 
Hebu tutajie hizo bank na mikopo ilikuwa ni ya kiasi gani?
Nikishaweka uje na swali jingine? Kama umepata uraia wa Tanzania jana ni sawa ila kama unafahamu mfumo wa mikopo ya wafanyabiashara ndani ya Tanzania sidhani kama majibu huyafahamu mkuu!
 
Na hapo bado hujaongelea gharama za viambatanisho na kuprocess huo mkopo! Sijui barua ya mtendaji wa Kata, barua kutoka serikali ya Mtaa, viapo vya Mwanasheria, pasport size, Bima ya jengo, bado hujabambikw madeni feki ya nyuma ya mitandao ya simu! Kote huko unatakiwa utoe hela!
Kichekesho kwenye huo mkopo utashangaa na hela ya Afisa Mikopo nayo inakatwa! Na wakati huyo mtu ameajiriwa na benki na analipwa mshahara kila mwezi!

Ukigusa mikopo ya wafanyakazi! Huko ndiyo kuna wizi mkubwa mpaka basi! Riba kandamizi! Makato yasiyokiwa na kichwa wala miguu!

Kwa kweli inahuzunisha sana. Mabenki yanafilisi wafanyakazi, wafanyabiashara na wajasiriamali kwenye hii nchi mpaka inakatisha tamaa. I wish ningekuwa Rais.
Well said mkuu
 
Ni jambo la kushangaza na lenye kuibua maswali makubwa kuhusu usawa katika mazingira ya biashara kati ya Tanzania na China. Mfanyabiashara wa China anapokopa katika benki za kibiashara nchini kwao hulipa riba ya takribani asilimia 3 pekee.
View attachment 3470612
Lakini mfanyabiashara wa kitanzania anapokopa katika benki za kibiashara za Tanzania, anakabiliana na riba ya wastani wa asilimia 17. Hii ni tofauti kubwa ya asilimia 14.
View attachment 3470613
Je, katika mazingira haya, mfanyabiashara wa Tanzania anawezaje kushindana na Mchina ambaye mara nyingi hujificha nyuma ya mgongo wa Mtanzania kuendesha biashara zake? Ni wazi kuwa mfumo huu unawaweka wafanyabiashara wetu katika wakati mgumu, ukipunguza uwezo wao wa kushindana na kuendelea kibiashara. Swali la msingi linabaki: ipo wapi sera ya usawa na ulinzi kwa wafanyabiashara wa ndani?
Kiuchumi bado Tz hawawez kushusha rate iyo nchi yetu bado inahitajii riba kubwa kuilinda shilingi
 
Back
Top Bottom