Uko wapi uzalendo wa Tundu Lissu kwa Nchi yake?

Mimi ninaamini Mh Rais anastahili kuungwa mkono kwani ameonyesha kwa dhati anatetea wanyonge.

Na wale wasiokuwa wanyonge, nani anawatetea? Katiba ya nchi inaruhusu jambo hili la mkuu wa nchi kutetea wanyonge tu? Na imekuwaje baadhi ya watanzania ni wanyonge? Ingekuwa sahihi kama angekuwa anatetea haki ya kila mtanzania kwa mujibu wa katiba, sheria, kanuni na taratibu kama alivyoapa kuilinda na kuitetea katiba na hiki kiapo ndio kulinda na kutetea haki ya kila mtanzania na sio kundi moja la wanyonge tu.
 
Mpendazoe kwa umri wako hoja hii unajidhalilisha sana. Hujielewi umesimamia wapi zaidi ya kuonyesha unafiki na uchumia tumbo tuu.

Lissu ametoa hoja ambazo zilihitaji majibu na sio kusema katukana, kamtukana nani? ona hata Polisi wamechoka ndio maana wanatoa majibu kuwa NI AMRI TOKA JUU.

Hiyo kauli ukiiangalia kwa jicho la tatu ni kama kusema sisi hatuoni kosa la huyu lakini aliyeko juu ndio katoa amri.

Jambo ambalo ni kinyume na katiba na haki za kiraia. Wewe kaa kimya tuu, umejichujia na huna hoja yeyote zaidi ya njaa.
Akili ya Watanzania ni ya ajabu sana, ndiyo maana kila siku Rais anauliza hivi sisi tuna nini? Yeye hana jibu na hawa akina Mpendazoe wanaojifanya wajuaji hawana majibu!!

Mpandazoe inaelekea anataka akumbukwe kwenye huu Ufalme ............ Kila kukicha anajipitisha pitisha ili aonekane!!

Hii Propaganda kuwa Lissu na wapinzania wanatumia lugha ya matusi, kejeli na dharau sijui ana maana gani. Mbona hataji hata tusi moaja lililotamkwa na Lissu au hao Wapinzani. May be kejeli na dharau maana haya maneno yako subjective na inategemea jinsi mtu binafsi anvyopokea ujumbe.

Mpendazoe ataje hayo matusi anayotukanwa Mkuu!!
 
Mheshmiwa Mpendazoe, shikamoo!! Kwa sasa nitajikita katika maana ya uzalendo.

Pengine baadae nitarudi kujibu hoja zako zingine. Nimeona msingi wa hoja yako ipo kwenye neno "uzalendo" hadi umehoji uzalendo wa Tundu Lissu (TL) uko wapi.

Nijuavyo mimi uzalendo ni mapenzi ya kujitoa, kuunga mkono na kuilinda nchi yako;utii kwa taifa lako (i.e devoted love, support, and defense of one's country; national loyalty). Hapa hakuna maneno mawili "rais" na "chama cha siasa".

Kwa sababu binfasi, sababu za kisiasa, sababu za kutetea maslahi binafsi, watanzania wengi tena wengi wao ni wasomi wamekuwa wakipotosha maana ya neno "uzalendo". Wao kwenye neon "taifa" au "nchi" wanaweka neon "rais" kwenye definition ya neon uzalendo.

Mark Twain alipata kusema "patriotism is supporting your country all the time, and your government when it deserves it". Pia Edward Abbey alipata kusema "A patriot must always be ready to defend his country against his government".

Hapa utaona utofauti kati ya nini mzalendo anapaswa kutetea; Je ni serikali (including rais) au Je ni nchi/taifa?

Serikali ni watu ambao wapo wema na wabaya lakini nchi/taifa lina misingi na miiko yake ikiwemo demokrasia, utawala wa sheria, umoja, huduma bora za kijamii, amani nk. Je, anayoyafanya TL hata kuhoji uzalendo wake ana-defend nini? Unachofanya wewe Mpendazoe, JPM nk mna-defend nini?

Uzalendo ni "NDIYOOOOO" kwa kila afanyalo Rais hata kama linavunja msingi na mwiko wa taifa letu?

Uzalendo ni kuunga mkono chochote kilicho chema kwa taifa regardless kimefamywa na nani? Kinachopaswa kuungwa mkono ni MTU au KITENDO?

Umeongea vizuri sana lakini jambo moja tu limeharibu uzi wako nalo ni '' USHABIKI''. yaani umepindisha maana halisi ya andiko lako ili kumtetea Lissu against Uzalendo. unapomreffer Mark Twain "patriotism is supporting your country all the time, and your government when it deserves it".

Nadhani ulielewa maana halisi ya msemo huu unless hukuelewa. alichokisema Lissu kwamba 'Nchi' inyimwe misaada, maana yake aliongelea Tanzania as country inyimwe misaada na siyo Serikali au Rais Magufuli. sasa kwa mujibu wa kauli hiyo ya Mark Twain uzalendo wa Lissu uko wapi hapo? maana he is not support his country nor the government, therefore he is not a patriotic.

Wakati mwingine tuwe waungwana kukubali pale watu wanapokosea hata kama tunawapenda au tunaunga mkono mlengo wa itikadi zao za kisiasa. vile vile, badala ya kufanya personal attack kwa mpendazoe hebu tujaribu kuzielewa hoja zake hususan demokrasia ndani ya vyama vyetu kama inaendana na kile tunachokikosoa kwa wengine.
 
Aiseee siamini macho yangu...Kumbe ndo uwezo wako ulipofikia hapo Mpendazoe..nilikuona kichwa kumbe sikuwa nimekufahamu vyeme kabla...

Nimejaribu kusoma maelezo yako yoote yaani hayana uhusiano na kichwa cha habari bali ni muendelezo ule ule wa wale viongozi wasiokuwa na dira kujaribu kujipendekeza kwa Rais..Unapoamua kupoteza mda na kuandika mambo yoooote kama haya 'next time' jaribu kuwa 'more critica'l na ujibu hoja kwa hoja sio kufanya majumuisho yasiyoeleweka..kwa mfano ulitakiwa kutwambia kwamba sio kweli...

Uteuzi wa wasaidizi wake haufanywi kiukabila kwa kutoa mifano a, b,c...au ungesema vyama vya upinzani sio pekee vinavyozuiwa kufanya mikutano ya ndani na CCM wanazuiwa mfano a,b,c...

Au Polisi hawapewi amri kutoka juu kwa sababu a,b,c...n.k......lakini kwa upupu huu ulioandika nachelea wakati mwingine kusoma makala yako yoyote utakayoandika kwani itakuwanikunipotezea mda wangu bure..
 
Labda tuwasaidie namna ya kumjibu Lissu,fuateni hii hapa;

1.Tanzania hakuna ukandamizaji wa demokrasia...Toeni uthibitisho kuwa katiba na sheria inafuatwa kuhusu demokrasia

2.Rais Magufuli sio dikteta uchwara....Toeni maana ya dikteta uchwara na mlinganishe na matendo ya rais ili kuthibitisha kuwa sio dikteta uchwara

3.Bunge linaendeshwa haliko huru,linaendeshwa kwa uhuru---Toeni maelezo kuwa bunge liko huru na haliendeshwi na serikali.

4.Mahakama inaingiliwa---Pingeni hoja hii kwa uthibitisho

5.Polisi inanyanyasa wapinzani kulinda ccm-----Kanusheni kwa uthibitisho

6.CCM pekee ndio kinafanya siasa,vyama vingine vimezuiliwa,.---Kaneni hii hoja kwa kutolea maelezo upokeaji wa wapinzani kwenye mikutano ya rais na ziara za Polepole na Shaka.

Mpendazoe na wenzako,jibuni hoja acheni kuzungukazunguka!!
 
Huyu mwanachama mwenzangu japo kuwa aangalii umri wake ikabidi nimjibu kiuchama. Hivi yanayifanyika ktk hii nchi yenye amani ni sawa yaani Lissu anaelezea yanayifanyika kwa huu uongozi ulioko anatamatwa na kuitwa Mchochezi.Kwa uchochezi upi huu wa kusema ukweli ndiyo najua ukweli unauma lakini ndo hivyo sisi ndo yote aliyoyasema ni ya kweli.

Mzee tunapigana na Mpinzani wetu wakati tumemfunga mikono hapa nani Mchochezi

Uzalendo wa Lissu ni kwamba ndo mtetezi wa wananchi Tanzania ambao akili zao sio tegemezi kwani mtegemezi ni mtu mvivu na mtu mvivu hawezi kuwa na hoja zenye mashiko ktk jamii


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lissu ndio icon ya demokrasia hapa nchini kwa sasa na ndiye mwanasiasa pekee anayethubutu kuongea fact zinazomuhusu sizonje na serikali yaan najuta kuipoteza kura yangu kumpigia mpendazoe sikutegemea km kuna siku ataota mkia na kuwa kiumbe chenye madhara kwa demokrasia ya nchi yetu najua hii yote anajipendekeza ili sizonje ampe kanafasi hata cha afisa mtendaji wa kijiji ok ngoja tusubiri na yeye si wa kanda ya kulekule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo sasa, tena nashukuru Chademakwanza hawakuchukuwa nchi, hawa jamaa hawangekuwa madikteta, wangekuwa kama kina Museveni kama siyo kina Mugabe, wakibisha wewe angalia wanavyoendesha chama chao, kuanzia mwenyekiti wa kudumu, jinsi wanavyochaguwa wabunge wa kuteuliwa uendeshaji wa chama, mapato na matumizi n.k. n.k.
jibu kwanza hoja za Lisu, sio kutupa mateke kule na kule..............
 
Kupingana na serikali sio kupingana na wananchi, kuomba serikali izomewe sio kuomba wananchi wazomewe. Raisi na serikali yake sio nchi nzima.

HAMUONI AIBU kulilia misaada? si mlisema sisi nchi tajiri hatutaki misaada? kimeishia wapi? mnaonaje mkapunguza matumizi ya anasa yasiyokwisha kila siku ili muishi ndani ya uwezo wenu? nyie mfakamie nusu ya bajeti kwenye recurring expenditures halafu mtie aibu nchi nzima kwa ulafi wenu na kutaka kutembelea mashangingi?

Tumefika hapa kama taifa kwa uroho, ulafi na upuuuzi wa CCM, hilo halikwepeki. mkiambiwa ukweli mtulie.

Alichokisema Lissu ndicho alichokisema mwenyekiti wenu, wametumia aina tofauti ya matamko tu. shida yenu ni unafki na kuropoka bila kutazama uhalisia. mnajidai nchi tajiri wakati mkimaliza hotuba mnakinga mabakuli ya misaada na kuomba hadi vinchi maskini kama ethiopia misaada.
 
Umeongea vizuri sana lakini jambo moja tu limeharibu uzi wako nalo ni '' USHABIKI''. yaani umepindisha maana halisi ya andiko lako ili kumtetea Lissu against Uzalendo. unapomreffer Mark Twain "patriotism is supporting your country all the time, and your government when it deserves it".

Nadhani ulielewa maana halisi ya msemo huu unless hukuelewa. alichokisema Lissu kwamba 'Nchi' inyimwe misaada, maana yake aliongelea Tanzania as country inyimwe misaada na siyo Serikali au Rais Magufuli. sasa kwa mujibu wa kauli hiyo ya Mark Twain uzalendo wa Lissu uko wapi hapo? maana he is not support his country nor the government, therefore he is not a patriotic.

Wakati mwingine tuwe waungwana kukubali pale watu wanapokosea hata kama tunawapenda au tunaunga mkono mlengo wa itikadi zao za kisiasa. vile vile, badala ya kufanya personal attack kwa mpendazoe hebu tujaribu kuzielewa hoja zake hususan demokrasia ndani ya vyama vyetu kama inaendana na kile tunachokikosoa kwa wengine.
Kipande, Africa hiyo democracy ndani ya vyama ni kiini macho!! Na kama kungekuwa na hiyo democracy mtu kama Maghufuli asingekuwa Rais wa nchi hii kupitia CCM !! Kwani hakuwa na uungwaji mkono ndani ya chama. Kwa hiyo hata kwa CDM walijuwa kinachowafaa ndani ya chama na si wengi wanatakaje !! Kwa hali hiyo hoja ya Mpendazoe haina mashiko.

Kuhusu uzalendo Tundu Lisu ni mzalendo kwa sababu hataki nchi irithishwe udikteta unaomea pole pole kupitia mikono ya JPM. Na Bahati mbaya kabisa siku hizi pro Maghufuli na government wote wanashabikia u dictator

Cairo's
 
ukiona mgonjwa analalamika ujue sindano imegusa penyewe !!! Lissu kaongea lumumba imekuwa vilio tupu na huu ndo uzalendo halisi kuwajulixha wa2 wasiyoyajuwa na kuwa mzalendl cyo kuwa mtiifu kwa serikali !!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fred Mpenda whatever your name is, Tundu Lissu ameeleza ukweli mnasifia hata uchawi? Watanzania tujitambue sio kusimamia kila jambo analosema kiongozi yule. Nendeni Kibiti mkarekebishe mambo acheni kupoteza muda. BBC wameitoa hiyo nenda kawajibu na wao kama ulivyojaza utumbo hapa.
 
Kipande, Africa hiyo democracy ndani ya vyama ni kiini macho!! Na kama kungekuwa na hiyo democracy mtu kama Maghufuli asingekuwa Rais wa nchi hii kupitia CCM !! Kwani hakuwa na uungwaji mkono ndani ya chama. Kwa hiyo hata kwa CDM walijuwa kinachowafaa ndani ya chama na si wengi wanatakaje !! Kwa hali hiyo hoja ya Mpendazoe haina mashiko.

Kuhusu uzalendo Tundu Lisu ni mzalendo kwa sababu hataki nchi irithishwe udikteta unaomea pole pole kupitia mikono ya JPM. Na Bahati mbaya kabisa siku hizi pro Maghufuli na government wote wanashabikia u dictator

Cairo's

Sijui kama ulifikiri vizuri Kuhusu kutolea mfano wa uteuzi wa magufuli CCM. Maana ukilinganisha na ule wa Lowassa CDM, angalau CCM walionekana waki exercise democracy katika uteuzi wao kwsbb magufuli alishindanishwa na watu wengine akiwemo huyo Lowassa katika hatua mbalimbali mpaka aliposhinda kwa kura.

Sasa tujiulize Lowassa CDM alishindanishwa na nani? Mchakato wa uteuzi wake ulifanywa na nani? Kwann Dk.slaa uteuzi ulitenguliwa akapewa Lowassa tena muda mfupi tu baada ya kuhamia. Yaani Maswali ni mengi kuliko majibu.

Kiufupi tukubali tu ukiongolea Demokrasia ndani ya vyama ni heri ya CCM kuliko CDM na hili tunalijua isipokua ushabiki ndo unatufanya tunyooshee kidole upande mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom