Ukiwa Rais leo unaanzia wapi?

Ukiwa Rais leo unaanzia wapi?

Inkotanyi 94

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2013
Posts
2,244
Reaction score
4,030
Kila mtu ana ndoto. Kila mtu huamini ana suluhisho sahihi. Hata hivyo tukubariane hakuna mbinu moja katika kutafuta jawabu la changamoto za ustawi wa maisha. Ndo mana ubepari na ujamaa hakuna ajuaye fika ipi ni bora kufanya maisha yawe na maana.

Kutofautiana ndiko huleta matokeo chanya. Leo ukipewa nchi ya Tanzania utaanza na lipi? (Katika hili utani/mizaha haipokelewi). Bila kutamka ELIMU mana kila mtu ataanza nalo,
Mimi nitaanza;

1. Kufuta vyama vyote vya siasa wajisajiri upya na visizidi 4 na kuruhusu mgombea binafsi kuruhusu siasa zenye uwiano. Mali zote zilizoko mikonon mwa ccm na zilipatikana wakat wa mfumo wa chama kimoja kwa jasho la wote zinarudi serkalini.
2. Nitaondoa kero zote za muungano (kuweka win win union) hata zikigharimu kura ya kutengana mazima.
3. Nitaichambua upya mikataba mikubwa ya madini, gesi/mafuta, bandari na mbuga.
4. Nitaboresha sera ya mahusiano ya kimataifa kufanya biashara na taifa lolote.
5. Nitafuta makosa yote walio magereza isipokuwa walioua nawapa haki yao wote.
6. Nitajenga matajiri wazawa. Kila tenda kubwa na ndogo wazawa kwanza labda wakiri si level yao.
7. Nitafuta bidhaa zote zinazoweza kutengenezwa ndan kuwa imported. Uhitaji utazaa uwekezaji wa ndani.
8. Nitapunguza gharama za kuendesha serkali kwa 40%
9. Nitabadiri sheria kadhaa ikiwemo kutunga sheria ya kuua wahujum uchumi wakubwa.
Kila aliyefaidika na mifumo ya nyuma nitamruhusu aendeleze alichokwapua kuliko kutoroshea nje, hakuna makosa ya nyuma.
10. Nitaboresha mifumo ya kutawalana ianzie ngazi ya balozi na kuimarisha kamati ya maadili ya kila jamii husika. Kila mtu atajulikana ni nani, anafanya nini.

Pia nitaboresha mifumo na utendaji wa serkali (Serikali, Bunge na Mahakama) ikiwemo wabunge wawe na elimu kuanzia degree na uhuru wa mahakama. Mwisho kabisa, serkali itasimamia vyanzo vikubwa vya uzalishaji kupitia kampuni kwa ubia.

Lengo kuu ni ustawi wa watu ujidhihiri katika furaha ya kuishi (kama scandinavian states)
 
Nitafuta kifuta chama Cha kijani kisionekane Tena Duniani na chawa wake wote ntawachoma sindano za sumu

Nitapunguza idadi ya wabunge bungeni had kufikia wabunge 100..tu nakigezo Ili uwe mbuge at least uwe na masters..

Nitabadili mitaala ya elimu Ili kuendana na Dunia inataka nini

Nitabadili katiba na kupunguza madaraka ya rais

Nitaondoa ma DaS na wakurugenzi kweny kila wilaya nitaacha wakuu wa wilaya..

Nitafanya mapinduzi ya kijani kweny kilimo...Ili Tanzania iweze kuirisha Africa mzima
 
Nitafuta kifuta chama Cha kijani kisionekane Tena Duniani na chawa wake wote ntawachoma sindano za sumu

Nitapunguza idadi ya wabunge bungeni had kufikia wabunge 100..tu nakigezo Ili uwe mbuge at least uwe na masters..

Nitabadili mitaala ya elimu Ili kuendana na Dunia inataka nini

Nitabadili katiba na kupunguza madaraka ya rais

Nitaondoa ma DaS na wakurugenzi kweny kila wilaya nitaacha wakuu wa wilaya..

Nitafanya mapinduzi ya kijani kweny kilimo...Ili Tanzania iweze kuirisha Africa mzima
Kufuta chama kimoja ni kuzalisha tatizo kubwa zaid. Bora ufute vyote. Kila watu waamue kusajiri upya.
Hii ni kwa sabab kwa sasa hatuna mfumo wa vyama vya siasa bali tuna ccm na vyama vya siasa. Vyama hivi kiuwezo na ushindani ni kama watoto wa ccm watukutu na wadadisi.
Ndio maana ukiwa nje ya ccm unaonekana muasi na mtukutu na si mbadala. Ni kama museven na muhoozi.
 
Kila mtu ana ndoto.
Kila mtu huamini ana suluhisho sahihi.
Hata hivyo tukubariane hakuna mbinu moja katika kutafuta jawabu la changamoto za ustawi wa maisha. Ndo mana ubepari na ujamaa hakuna ajuaye fika ipi ni bora kufanya maisha yawe na maana.
Kutofautiana ndiko huleta matokeo chanya.
Leo ukipewa nchi ya Tanzania utaanza na lipi?
(Katika hili utani/mizaha haipokelewi)
Bila kutamka ELIMU mana kila mtu ataanza nalo,
Mi nitaanza
1. Kufuta vyama vyote vya siasa wajisajiri upya na visizidi 4 na kuruhusu mgombea binafs kuruhusu siasa zenye uwiano. Mali zote zilizoko mikonon mwa ccm na zilipatikana wakat wa mfumo wa chama kimoja kwa jasho la wote zinarudi serkalini.
2. Nitaondoa kero zote za muungano (kuweka win win union) hata zikigharim kura ya kutengana mazima.
3. Nitaichambua upya mikataba mikubwa ya madini, ges/mafuta, bandari na mbuga.
4. Nitaboresha sera ya mahusiano ya kimataifa kufanya biashara na taifa lolote.
5.Nitafuta makosa yote walio magereza isipokuwa walioua nawapa haki yao wote.
6.Nitajenga matajiri wazawa. Kila tenda kubwa na ndogo wazawa kwanza labda wakiri si level yao.
7. Nitafuta bidhaa zote zinazoweza kutengenezwa ndan kuwa imported. Uhitaji utazaa uwekezaji wa ndani.
8. Nitapunguza gharama za kuendesha serkali kwa 40%
9. Nitabadiri sheria kadhaa ikiwemo kutunga sheria ya kuua wahujum uchumi wakubwa.
Kila aliyefaidika na mifumo ya nyuma nitamruhusu aendeleze alichokwapua kuliko kutoroshea nje, hakuna makosa ya nyuma.
10. Nitaboresha mifumo ya kutawalana ianzie ngazi ya balozi na kuimarisha kamati ya maadili ya kila jamii husika. Kila mtu atajulikana ni nani, anafanya nini.
Pia nitaboresha mifumo na utendaji wa serkali (serkali, bunge na mahakama) ikiwemo wabunge wawe na elimu kuanzia degree na uhuru wa mahakama.
Mwisho kabsa, serkali itasimamia vyanzo vikubwa vya uzalishaji kupitia kampuni kwa ubia.
Lengo kuu ni ustawi wa watu ujidhihiri katika furaha ya kuishi(kama scandinavian states)
1. Nawapeleka mahakamani wote walioiba fedha za umma.
2. Mahakamani wote waliovunja katika na sheria kwa kiburi cha madaraka
3. Katiba mpya (hii inakwenda sambamba na hayo juu )
 
Naanza na kumpa Tundu Antipas Lissu Mwanasheria mkuu wa nchi.
Huyu ana dalili za ukisasi (vengeance). Awe mshauri tu kwanza. Sheria zikishakaa sawa kudhibiti madaraka ndo apewe meno.
Lisu na magufuri wanatofautiana majina tu. (Nadhan wana akili sana hawaamin katika makosa.)
Kumbuka nawaza umekuwa rais unajenga Tanzania mpya alafu uruhusu mifumo ijiendeshe sio ukae milele. Kwa sasa naona tunatawalana kama viumbe wa mbugani.
Survival of the fittest!
Ingawa kwa vinasaba vya kiafrika demokrasia inahitaji tafsiri ya kimazingira yetu. Tuna asili ya mfumo wa ufalme/uchifu/ukama (kama waarab). La sivyo inaweza kuwa chaos. Kenya wamethibitisha hivyo!
 
Naanza na kumpa Tundu Antipas Lissu Mwanasheria mkuu wa nchi.
lissu ni radical, acha awe vile vile,...... usimpe cheo kinachohitaji mtu rational,
lissu na jiwe wana character sawa, wanatofautiana matendo!
 
1. Nawapeleka mahakamani wote walioiba fedha za umma.
2. Mahakamani wote waliovunja katika na sheria kwa kiburi cha madaraka
3. Katiba mpya (hii inakwenda sambamba na hayo juu )
Kama unajenga Taifa upya, na orodha kubwa hivi ikiyotufikisha hapa, kufungana ni sawa na kutoanza upya. Kuna wakati kusamehe kunajenga.
Tatizo utafunga nusu ya raia hivi hivi. Na binadam ni kiumbe wa kujikomboa, atakusumbua. Kizuri zaid ni raia akiibia serkali naye kajiibiana. Walioibiwa wanaweza vumilia.
 
Natfuta katiba, nchi inaendeshwa kijeshi Kwa miaka kumi, Mimi ndio ntakuwa katiba, Sheria na Kanuni. Miaka miwili ya mwisho Katiba mpya itakuwa imepatikana, naifanyia majaribio kama imeziba myanya yote ya mafisadi na wazembe, imechajihisha uzalishaji na uwajibikaji. Mwaka wa 11 tunaenda kwenye uchaguzi wa kidemo, nikishindwa nakubari, nikishinda nauwasha moto kwenye maendeleo na kuhakikisha mentality za kifisadi zilizowajaa wadanganyika zinayeyuka na kupotea kabisa. Bila kusahahu navunja Muungano kabisa au serikali Moja.

NB. Pligozin na kundi lake la Wagner watahusika. Kuwazibiti wazalendo uchwala.
 
NItaruhusu kilimo cha Bangi haraka Sana yaani ndani ya wiki yangu ya Kwanza madarakani
Nitakuelewa kama unamaanisha kilimo cha bangi kwenye udhibiti maalum(hasa jeshi) ili tuuze extract concentrate kutengeneza madawa.
Lakin zaid ni kukarbisha kiwanda cha dawa kama za maumivu nchini. Maana hata leo ndo tunayatumia yenye bangi.
Lakin kwa wavutaji mtanisamehe nijiridhishe na utafiti. Unaweza kujikuta una watu hawatawaliki.
 
Anza na mabadiliko yako wewe mwenyewe kwenye eneo lako la kazi,uwe muaminifu,usile rushwa,usionee mtu,ujanja ujanja na uvivu iwe mwiko kwako,

Leo familia yako kwenye maadili mema ili kujenga taifa bora,

Mabadiliko huanza na wewe,huwezi kulea familia ya mke na watoto wawili kwenye maadili ya hovyo kisha eti uje kua kiongozi bora.
 
Kuna viongozi wastaafu watakuwa jela baada ya miezi sita ya uongozi wangu

Kwa kuliingiza taifa kwenye mikataba mibovu.
Hamna cha kinga ya kutokuishitakiwa wala nini ni jela na kufilisiwa.
 
1. Nitafungua kiwanda cha ugoro jijini Arusha, ugoro upo mtaani lakini cha ajabu haijulikani unatengenezwa wapi material zake ni nini na zikoje,

2. Nitafungua kiwanda cha Gongo kila mkoa wenye baridi kali kuhakikisha walevi wanapasha mwili joto kwa kitu chenye TBS:
 
Ukishakua raisi...nipe kitengo cha usafi wa mazingira kitaifa, hiki ntakimudu vzuri sana
Ntabadilisha mfumo mzima wa usafi kuanzia mtaa mpaka mkoa
 
Back
Top Bottom