Ukiwa na miaka 60 - 67 unaweza kuwa na ndoto za miaka 20 mbele?

Leverage

JF-Expert Member
Jan 25, 2021
2,125
3,130
Nimekutana na mzee mmoja mstaafu katika kuongea nae nikagundua ana mipangilio ya miaka mingi mbele.

Mosi: Ana eneo ekari 5-6 Kongowe ya Mbagala hapa ana ndoto ya kujenga shule.

Pili: Ana eneo ekari moja Mabwepande hapa ana mpango wa kujenga nyumba za kupangisha.

Tatu: Ana eneo ekari moja na nusu Fukayosi, hapa ana mpango wa kulima mananasi.

Nimeangalia mipango yake na umri wake kwa akili yangu imegoma hasa hapo kwenye shule na ukizingatia ni miaka 13 sasa tangia astaafu. Naamini jamii forum kuna watu wenye umri tofauti na uzoefu tofauti.

Je, mstaafu wa JWTZ anaweza kutekeleza hayo? Kuuza eneo hataki kusikia kabisa tena ukimshauri mnaweza kugombana.
 
Tusiwe tunachagua rais aliyezidi miaka 50. Wazee hawana mipango ya muda mrefu.
Umri wa mtu kuchaguliwa uanzie miaka 21.
 
Samuel Doe aliingia madarakani kwa mapinduzi kule Liberia akiwa na 35. Aliwachezesha singeli wananchi mpaka wakashangaa. Kupata madaraka ukiwa kijana sometimes sio poa.
Ghaddafi aliingia na 27. Alexander mkuu alitawala dunia akiwa na mika 32, alianza kuteka na miaka 20 hivi. Yesu hadi anakufa ana miaka 33. Pablo Escobar alianzisha Medellin Cartel akiwa na miaka 26 tu.

Upande wa pili unamkuta Zuma na Mugabe wanaiba wakiwa na miaka zaidi ya 70. Bado wakina Biya, Bongo na wazee wengine wengi wajingawajinga
 
Miaka 21 bado mtoto
Anaruhusiwa kuwa mbunge na waziri huyo. Maana yake anaweza kuwa waziri mkuu. Tena iwe kumi na nane kabisa. Sababu kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Iweje huyu wa miaka 21 awe na vigezo vya kuchagua Rais lakini asiwe na vigezo vya kuchaguliwa kuwa Rais?

Kipengele cha miaka kinavunja katiba ya nchi.
 
Alhamdullilah yuko 73..
Mungu mkubwa huwezi jua kakupangiaje
Plan atleast 85-90 yrs of age unaweza fika...
 
Japo kwa umri huo inabd uwekeze kwenye vipato visivyo hitaji nguvu
Suala la ujenzi shule kwelii?
Ana hicho kipato kwanza?
Heri akanunue bonds BoT atulie ale hela kdg kdg
 
Kwa umri huo ajikite zaidi kwenye kuplani ni namna gani atazikwa na mgawanyo wa mali zake kwa wanae utakuwaje.

Mkumbushe kua bible imeandika hvii

Siku za mwanadamu zahesabika nazo si nyingi, jumla yake ni miaka sabini😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Achukue 70 atoe umri alio nao saiv alafu aende bar akagambike akisubiri kufa😂😂😂😂😂😂
 
Japo kwa umri huo inabd uwekeze kwenye vipato visivyo hitaji nguvu
Suala la ujenzi shule kwelii?
Ana hicho kipato kwanza?
Heri akanunue bonds BoT atulie ale hela kdg kdg
Watoto wake wanasema pension yake aliyopata wakati anastaafu miaka 10 iliyopita ni milioni 96
Je itakuwepo hadi sasa?
 
Kwa umri huo ajikite zaidi kwenye kuplani ni namna gani atazikwa na mgawanyo wa mali zake kwa wanae utakuwaje.

Mkumbushe kua bible imeandika hvii

Siku za mwanadamu zahesabika nazo si nyingi, jumla yake ni miaka sabini😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Achukue 70 atoe umri alio nao saiv alafu aende bar akagambike akisubiri kufa😂😂😂😂😂😂
Ukiwa kazini unaishi kwa dhiki na ukistaafu unaishi kwa tabu
 
Nimekutana na mzee mmoja mstaafu katika kuongea nae nikagundua ana mipangilio ya miaka mingi mbele.

Mosi: Ana eneo ekari 5-6 Kongowe ya Mbagala hapa ana ndoto ya kujenga shule.

Pili: Ana eneo ekari moja Mabwepande hapa ana mpango wa kujenga nyumba za kupangisha.

Tatu: Ana eneo ekari moja na nusu Fukayosi, hapa ana mpango wa kulima mananasi.

Nimeangalia mipango yake na umri wake kwa akili yangu imegoma hasa hapo kwenye shule na ukizingatia ni miaka 13 sasa tangia astaafu. Naamini jamii forum kuna watu wenye umri tofauti na uzoefu tofauti.

Je, mstaafu wa JWTZ anaweza kutekeleza hayo? Kuuza eneo hataki kusikia kabisa tena ukimshauri mnaweza kugombana.
Dah.... nina 79yrs natafuta mchumba...nikimpata nanunua shamba Bagamoyo....nalima mananasi.....halafu nafuga kuku..na pia nitapanda miti.....:D

 
Nimekutana na mzee mmoja mstaafu katika kuongea nae nikagundua ana mipangilio ya miaka mingi mbele.

Mosi: Ana eneo ekari 5-6 Kongowe ya Mbagala hapa ana ndoto ya kujenga shule.

Pili: Ana eneo ekari moja Mabwepande hapa ana mpango wa kujenga nyumba za kupangisha.

Tatu: Ana eneo ekari moja na nusu Fukayosi, hapa ana mpango wa kulima mananasi.

Nimeangalia mipango yake na umri wake kwa akili yangu imegoma hasa hapo kwenye shule na ukizingatia ni miaka 13 sasa tangia astaafu. Naamini jamii forum kuna watu wenye umri tofauti na uzoefu tofauti.

Je, mstaafu wa JWTZ anaweza kutekeleza hayo? Kuuza eneo hataki kusikia kabisa tena ukimshauri mnaweza kugombana.
Inawezekana kabisa kutimiza ndoto pasipo kujali umri.Nuhu alijenga safina akiwa na miaka 600 Sara alizaa akiwa na miaka 60.Tajiri wa KFC alipata utajiri akiwa 60s.Maisha hayana formula
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom