Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Kama unazo na nafasi ya hela ipo na umemsoma Vizuri shughuli anayoenda kufanya mkopeshe tu Ndio urafiki wenyewe maana Hamna Formula kuwa lazima Hatalipa na utapoteza rafiki wewe mwenyewe huna mkataba kuwa hamma siku hutahitaji msaada kwa marafiki na sio kwamba lazima kuwa utasaidiwa na huyo huyo uliye mkopesha

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli mkuu,kuliko kutoa ahadi za uongo;mi nadhani ni bora mtu kuwa muwazi...kwamba sina,kuliko kumpa mtu matumaini,matokeo yake hamna kitu.
 
Mimi:Inakuaje kiongozi uko poa?
Rafiki:Fresh mwanangu,niambie kaka.
Mimi:Vipi michakato?
Rafiki:dah michakato iko poa mambo yako vizuri.
Mimi:aisee na hali hii kaka?
Rafiki:kaka pesa ukiitafuta mbona itakufuata,now mtaji umekua si unaona mwenyewe.
Mimi😛oa kaka hongera na jambo la kumshukuru Mungu,sasa Mkuu nimekwama hapa na huu mguu wako ,nina shida na elfu 10 hebu naomba unisaidie kesho kutwa jioni nitakupa sina hata mia ukicheki familia inahitaji kula.
Rafiki:Aisee pole sana ndugu yangu najisikia vibaya sana ,sasa umechelewa kidogo yaani nimetoa sasa hivi laki 8 kununua mzigo hapa nimebakiwa na elfu 5 kama nauli ila usijali kuna mtu hapa analeta pesa yangu laki 4 saa 11 jioni kama vipi pitia.
Mimi:sawa kaka nitashukuru

Saa 11 jioni

Mimi:Kaka umeshindaje?
Rafiki😀ah acha tu ndugu yangu.
Mimi:kuna usalama kweli?
Rafiki😀ah utoke wapi si unakumbuka nilikuambia kuna mtu ana pesa yangu laki 4 ana ileta leo ndo nikakwambia uje?
Mimi:Ndio nakumbuka kaka
Rafiki:Sasa yule mtu kafariki dah roho inaniuma kweli peaa yangu nishaikosa na hapa biashara leo ngumu sijui itakuaje ndugu yangu nilitamani kukusaidia ila nimekwama pia.

Hapo giza lishaingia ushafeli huna pa kwenda maana alikupa matumaini ukaweka kwake hukutaka kutafuta kwingine.

Watu wa namna hii ni hovyo sana mfano hai wiki mbili zilizopita tulikua na kikao cha harusi sista anataka kuolewa february 23 tukakubaliana tufanye sherehe ndogo kila mtu atoe laki moja,lakini Kaka yetu wa pili akagoma akasema tutoe laki mbili kila mmoja tulimgomea kwa kua uchumi mgumu lakini akashinda kwa kua aliungwa mkono na mama .Leo ndo siku ya kuwasilisha mchango tangu jana kazima simu zote hapatikani aliahidi kitu kisichotekelezeka tena kwa mbwembwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa nao wapo wengi tu mkuu,, ukweli humuweka mtu huru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo mtu hakuambii kama anazo ama hana...mbaya zaidi hapokei simu yako na alikuahidi.
Hakuna tabia inaboa kama hiyo. Kheri mtu apokee simu na akupe hata maelezo. Kutokupokea simu ni dharau kubwa sana
 
Hakuna tabia inaboa kama hiyo. Kheri mtu apokee simu na akupe hata maelezo. Kutokupokea simu ni dharau kubwa sana
Kweli mkuu,ilibidi nifute namba tu...sasa kama mtu hapokei simu yako kuna umuhimu gani
 
Back
Top Bottom