Makene Bilali ni Baba yako au Babu yako,sasa serengeti si alienda kutalii unakataa nini,na USA si alenda kwani uwongo????mimi si mzanzibar na sipajui huko lakini alienda,kwan jk alipobembea jamaika watz tulisemaje??na tunasemaje????hadi sasa hapa jf anaitwa mtalii,
UTETEZI WA MASLAHI YA KICHAMA AU MASLAH BINAFSI NI ALAMA YA UBINAFSI AMBAO UNAWEZA KULITENGA TAIFA HILI AU KULIACHA KTK UJINGA KUTOKANA NA HUO UBINAFS.UTAIFA KWANZA KAMA KUNA UKWELI JUU YA ALICHOSEMA ARAFAT BASI ASHUKURIWE KIKWETE! LAKINI UONGO KTK HOJA HYO NI CHANGAMOTO INAYOTAKIWA KUCHOMWA MOTO! Labda hapo 2najifunza nini kutoka dr bilali principal alyepta wa udom zaid ya siasa chafu!
Wakati wazanzibari wanaendelea kukejeliwa wanapotaka kujitenga....wabara wako bize na kusapoti mambo haya
Hapo kwenye red, ndugu yangu jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Dk Bilal si kiongozi mbabaishaji ama mwenye kujenga chuki, ni kiongozi mwenye mapenzi mema na watu na ndio sababu amebaki kuwa kipenzi cha wengi si tu katika Zanzibar, Tanzania bali popote alipopata kuishi. Kwa msingi huo, utofauti wa yeye na Maalim Seif unabaki katika vyama vyao vya siasa tu lakini wanaunganishwa kwanza na Uzanziba na pia Utanzania. Si vema sana kutangaza chuki kwa watu ambao hawajakutuma kuwatangaza kuwa wanachukiana. Labda wewe ndiye unaowachukia hao wote wawili na unataka kuweka chuki zako kwa kutumia majina ya viongozi hawa.
Ndugu yangu nadhani hoja hii mmejipanga kutafuta jambo, kwanza mlianza na Makamu kwenda USA kutalii sasa mnabadilika. Kama ingekuwa ni kwenda USA nisingeingia kukujibu nimetoa majibu pale mlipopotosha safari ile ya kuiwakilisha Tanzania UNAIDS na utalii. Pili nimezungumzia safari ya Dk mbugani Serengeti, hivi ulitaka aende Bahama, ama yeye kama kiongozi wa kitaifa anayemsaidia Rais unataka kumjengea mipaka ya yeye aende wapi ndani ya Tanzania. Akili yako inakutuma kuwa kila mtu akienda mbugani kazi yake ni kutalii? Tambua kiongozi wa kitaifa aina ya Dk Bilal si mtu anayesubiri majibu ya hoja mezani, kiongozi huyu alienda huko kwa lengo la kutafuta ukweli kuhusu barabara inayotakiwa kujengwa ambayo imekuwa kwa kipindi sasa na taarifa za wanaharakati wanaotumiwa kwa maslahi ya mataifa ya nje na sio ya Tanzania. Sikushangaa kusikia alikwenda kutalii huko Serengeti kwa kuwa katika zama hizi za siasa zisizotathmini namna njema ya kuendeleza nchi yetu kila jambo linageuzwa siasa kwa makusudi ili kutoa taswira hasi kwa viongozi wa wananchi dhidi ya wananchi wao. Bado naamini kama huu muelewa nimekujibu lakini kama una agenda nyingine ambayo naamini unayo ni bora uilete hapa ili tuijadili hiyo.
wa jina, Makamu alienda serengeti kula bata baada ya uchaguzi siyo uzushi, tena alienda na wake zake wote wawili. Ngoja nizitafute zile picha nikubandikie.Ndugu yangu nadhani hoja hii mmejipanga kutafuta jambo, kwanza mlianza na Makamu kwenda USA kutalii sasa mnabadilika. Kama ingekuwa ni kwenda USA nisingeingia kukujibu nimetoa majibu pale mlipopotosha safari ile ya kuiwakilisha Tanzania UNAIDS na utalii. Pili nimezungumzia safari ya Dk mbugani Serengeti, hivi ulitaka aende Bahama, ama yeye kama kiongozi wa kitaifa anayemsaidia Rais unataka kumjengea mipaka ya yeye aende wapi ndani ya Tanzania. Akili yako inakutuma kuwa kila mtu akienda mbugani kazi yake ni kutalii? Tambua kiongozi wa kitaifa aina ya Dk Bilal si mtu anayesubiri majibu ya hoja mezani, kiongozi huyu alienda huko kwa lengo la kutafuta ukweli kuhusu barabara inayotakiwa kujengwa ambayo imekuwa kwa kipindi sasa na taarifa za wanaharakati wanaotumiwa kwa maslahi ya mataifa ya nje na sio ya Tanzania. Sikushangaa kusikia alikwenda kutalii huko Serengeti kwa kuwa katika zama hizi za siasa zisizotathmini namna njema ya kuendeleza nchi yetu kila jambo linageuzwa siasa kwa makusudi ili kutoa taswira hasi kwa viongozi wa wananchi dhidi ya wananchi wao. Bado naamini kama huu muelewa nimekujibu lakini kama una agenda nyingine ambayo naamini unayo ni bora uilete hapa ili tuijadili hiyo.
Naunga mkono hoja. Ukisoma vema kisa cha rais wa Zanzibar kutolewa kilazima mwaka 1984 utagundua kisa ni Seif. Ukisoma kisa cha Wazanzibari wengi kufa 2001 kisa ni Seif. Ukisoma vema juu ya watu hawa wawili wala hupati taabu kukubaliana na mwandishi wa makala hii. Ila kuna wengine lazima wataipinga sana kwa kuwa wao ni wachumia tumbo. Watu walianza kuajiriwa na makampuni ya mafisadi ili watumie kalamu zao kuwatetea. Kisha wamepewa nafasi serikalini kuendelea kutumia nafasi zao. Watu hawa kamwe hawawezi kuusimamia ukweli. Daima watasimamia maslahi yao. Ndivyo tulivyo wanadamu.
Ukweli utabaki kuwa ukweli hata kama utachukiwa kwa kiasi gani. Seif na Bilal ni zaidi ya wanafiki. Wanawahadaa Wazanzibari kwa maslahi yao binafsi.
Sikuwahi kufikiri kama huyu ndugu Bilal anatabia kama za bwana Seif.
Wewe ndio humjui Bilali.
Kama kuna kiongozi mbaguzi mwenye kuweka mbele undugu na ubaguzi kama huyu jamaa. Kila anapoenda anaweka jamaa zake na ndugu zake wa karibu. Huyu ndio kiongozi wa wale waliokuwa wakipinga SUK kwa kigezo eti itaharibu dhana ya mapinduzi daima. Yeye na Shamhuna ndio waliokuwa viongozi wa waasi wa kupinga SUK kwa kuhofia maslahi yao yataharibika.
Mkuu wangu siku zote nimekuwa nikiwaambia kwamba hawa viongozi wote ni wanafiki lakini hamkunielewa mkidhani sipendi maendeleo ya Wazanzibar. Hakuna kiongozi hata mmoja Zanzibar asiyekuwa mnafiki hilo ndilo nilojifunza isipokuwa wale waliokimbia toka wakati wa Karume. Na ktk swala hili wala usimseme Bilal peke yake kwa sababu anajulikana kuwa tapeli, majisifa, mroho na asiyetosheka na utajiri bali pia kisiasa lazima pia umwongezee Karume ambaye alichukua madaraka ya uongozi wa Zanzibar kwa kufuata maagizo ya CCM bara ili Zanzibar isijiunge na OIC. Na sii hivyo tu hata kukawepo na uadui wa kiana usiohusiana kabisa na maslahi ya Wazanzibar bali nani atashika madaraka gani na nani kakosa! Mbali na yote hayo angalia jinsi walivyojilimbikiza mali na yasemekana karibu kila hotel za kitalii beach wana 10%!...Dr Mohammed Ghalib Bilal aliteuliwa kuwa CM wa Zanzibar 1995 na kushika madaraka hadi 2000 akiwa na Rais wake Salmin Almour a.k.a Komandoo. Kabla ya hapo alikuwa PS-Wizara ya Sayansi na Teknologia kuanzia 1990.
Mwaka 2000 Bilal akiwa CM na Komandoo akiwa Rais wake walianzisha mpango kabambe wa kuitikisha serikali ya Mzee Ben, hadi Komandoo kujitokeza adharani na kutamka kuwa mtu yeyote anayedhani na kufikiria kuizua Zanzibar kujiunga na OIC anatikisa kiberiti, maneno na mienendo ya Komandoo na Bilal iliwa tia hamasa nakuwaadaha sana Wazanzibar walio wengi kiasi cha kujenga matumaini makubwa sana kwa Komandoo mwenyewe na msaidizi wake Dr. Bilal! Ni wakati huo ambapo Bilal na Komandoo pia waliwai kuota ndoto ya kupinda katiba ya Zanzibar hili kumuongezea Komandoo muda.
Wakidai muda zaidi kwa ajili ya Zanziabar huru zaidi wakijifanya miaka kumi haikuwa tosha na pia walifikia hatua ya kujidai kuwa wakipata nafasi watabadili mfumo wa Muungano hili Zanzibar iwe huru zaidi hisiingiliwe na Serikali ya Muungano wanapotaka kufanya mambo yao ya kimataifa, Komandoo na Bilal waliendelea kujinasibu na hata pale mkakati wa kubadili katiba ulipo kwama Komandoo alitamka dhahiri kuwa Rais wa Zanzibar atakuwa Dr. Bilal iwe hisiwe na kuwa lengo kuu ni kubadili aina ya muungano ili Zanzibar ielekee OIC, hayo maneno yalifurahisha sana wengi wa Wazanzibari na kuendelea kuweka matumaini yao yote juu ya Dr. Bilal; Katika ile inayoitwa Zanzibar special CCM committe mchuano wa kura za Urais wa zanzibar ulikuwa ni kama ifuatavyo (Komandoo akiwa ndio Mwenyekiti): -Jumla ya kura zilikuwa 74. Ni baada ya CC-CCM kubadili hayo matumaini makubwa ya Wazanzibar hasa Wapemba juu ya Dr. Bilal na kumrejesha Karume kama mgombe wa Urais wa Zanzibar kwa ticket ya CCM ndipo Dr. Bilal na Maalimu Seif walipofanya muungano husio rasmi na kuperekea Wapemba kupiga kura za pamoja kumpinga Amani Karume wakimnadi kuwa hawezi kuleta mabadiliko ambayo Wazanzibar wanayataka na kuwa ni kibaraka wa Wabara, huu ndio uchaguzi ulioleta kinachoitwa na wapemba kama machafuko ya Zanzibar, ni vurugu zilizo asisiwa na matumani ya Bilal na Maalimu Seif wakiwadanganya Wazanzibar kuwa ama Seif au Bilal mmoja wao ndio lulu na matumaini ya Zanzibar na kuwa watakapo ingia madarakani OIC ni dakika chache tu! Dr. Bilal na Seif tokea hapo mwaka 2000 walipo chochea kuuwawa kwa Wazanzibari wenzao waliendele kuingia katika chaguzi bila kufua dafu; Dr. Bilal akiomba Urais wa zanzibar kupitia CCM na kuchujwa na Seif akiomba kwa CUF na kushindwa katika Uchaguzi kwa kile ambacho wengi tuna amini kuwa mara zote alikuwa anaibiwa kura.
- Dr. Mohammed Ghalibu Bilal kura 44 (60%)
- Abdisalaam Issa Khatibu kura 13 (18%)
- Amani Abeid Karume kura 9 (12%)
- Kura zilizo aribika 8 (10%)
Maskini Wazanzibar kumbe Seif na Bilal si lolote walikuwa wanatafuta madaraka na shibe ya tumbo zao! Tuliamini wakipata nafasi kuna jipya! Wapo leo na mbona wamefunga midomo yao, wote wamepewa nafasi na Kikwete kwa makusudi kabisa! Mbona Dr. Bilal alipoapishwa tu alikimbia kula raha Mbuga za serengeti na kusaka na rumba USA? hayo ndio matumaini makubwa aliyowajengea wazanzibar juu yake?
Kumbe muda wote Wazanzibar waliweka matumaini yao juu ya watu wawili wanafki na wenyewe tamaa ya madaraka kiasi cha kuperekea kuuwawa kwa vijana wengi tu wakipemba na wengine mpaka leo wamezamia UK.
Tokea kupata nafasi ya Makamu wa Rais wa Muungano sijamsikia akiongelea tena OIC wala kubadili aina ya mfumo wa Muungano amefunga mdomo maana kishapata madaraka na hicho ndio kilikuwa shida yake.
Ukitaja wanafki waliowai kuiadaha Zanzibar, wenye tamaa na uchu wa madaraka, ukimtaja Maalimu seif husimsahau na Dr. Mohammed Ghalib Bilal.
Mkuu wangu siku zote nimekuwa nikiwaambia kwamba hawa viongozi wote ni wanafiki lakini hamkunielewa mkidhani sipendi maendeleo ya Wazanzibar. Hakuna kiongozi hata mmoja Zanzibar asiyekuwa mnafiki hilo ndilo nilojifunza isipokuwa wale waliokimbia toka wakati wa Karume. Na ktk swala hili wala usimseme Bilal peke yake kwa sababu anajulikana kuwa tapeli, majisifa, mroho na asiyetosheka na utajiri bali pia kisiasa lazima pia umwongezee Karume ambaye alichukua madaraka ya uongozi wa Zanzibar kwa kufuata maagizo ya CCM bara ili Zanzibar isijiunge na OIC. Na sii hivyo tu hata kukawepo na uadui wa kiana usiohusiana kabisa na maslahi ya Wazanzibar bali nani atashika madaraka gani na nani kakosa! Mbali na yote hayo angalia jinsi walivyojilimbikiza mali na yasemekana karibu kila hotel za kitalii beach wana 10%!...
Yaani Linchi letu lote limeoza kwa UNAFIKI ambao nadhani yawezekana inaingia ktk Uasili wa tamaduni zetu kwani haiwezekani unafiki huu wa kuuzana uwe wa bahati mbaya (coincidence) Upo ushahidi wa kihistoria unaoturudisha toka enzi za Utumwa kwamba sisi wenyewe tuliwauza ndugu zetu kwa kubadilishana na shanga!..Mambo mengi yanajirudia toka kuuzwa kwa nchi, mikataba na kadhalika yote haya yana historia ya Uasilia wa Mtanzania kwa Unafiki.. ndugu marafiki tunazikana kila siku yaani kwa Mbogo usikosee ukamwamini atakuweka mjini!
Kisha tunajiuliza ati sisi tumemkosea nini Mungu!
Makene wewe unamjuwa sana Dr. Bilal na umekuwa ukizunguka naye sana katika ziara zake na hata Serengeti ulikuwa naye; Twambie Dr. Bilal tokea mwaka 2000 matumaini makubwa ambayo Wazanzibari walijenga juu yake ilikuwa ni ya nini? waitegemea nini kutoka kwake kama ikiwa akipata nafasi ya uongozi kama huu aliopewa sasa?
Maneno yako kweli kabisa na una kila haki ya kutomwamini mtu yeyote kutokana na utamaduni wa Mtanzania (Unafiki) hilo halina shida kabisa isipokuwa nitayarudia maneno ya Lowassa ya kwamba ni bora kuchukua maamuzi magumu ukalaumiwa kuliko kutofanya kabisa! na pia ile ya JK kuhusu akili za mbayuwayu kwamba - Unapoambiwa kitu lazima usiamini moja kwa moja lazima uchanganye na za kwako!..
Mkandara! GOOD there you are;
Niliwai kusema kuwa unaweza kukuta hata hawa tunaowapa matumaini makubwa sana leo kesho wakaturudi, huwa nasema na sita ogopa kusema hadi kifo changu kwa CDM hadi leo ninayemwamini ni Dr. Slaa tu! Nina wasiwasi mkubwa sana na Zitto kabwe na Mbowe! Sijui kwanini imani yangu inawakataa kwa kweli siwa amini hata kidogo wanatumia ujinga wetu kutu adahaa na amini hivyo na nitaendelea kuamini hivyo mpaka watakavyo onyesha tofauti na kuni-prove wrong.
Tangu nianze kusoma post hii uliyoileta hapa nilipata maswali kadhaa na kisha kugundua yafuatayo:
1. Ninakufahamu na hukutegemea nijitokeze kukujibu hapa, nakufahamisha tu kuwa sina uoga katika kuzungumzia ukweli hata kama utakuchoma na hata kama utatoa tafsiri kama ambazo umeweka hapo
2.Umemuweka Seif Sharif katika mada hii kimtindo tu ili kurahisha kufikisha lengo lako ambalo kubwa ni kupinga Muungano, hoja ambayo ina mashiko katika vyama vinavyoshabikia serikali tatu.
3. Huna taarifa za kutosha juu ya mada hii kwa kuwa unatoa taarifa nyingi za kuhisia tu
4.Uwezo wako wa kuchambua hoja bila kuingiza mambo binafsi unaashiria kuwa hufai kupewa nafasi ya kuweka post hapa JF
5.Huna taarifa ya Katiba ya nchi hivyo hutambui hata majukumu ya viongozi wako wa kitaifa nafasi zao na kazi zao
6.Dk Bilal ni kiongozi wa Tanzania nzima ikiwemo Zanzibar kwa hiyo anafanya kazi kwa maslahi ya watu wa Rukwa, Kigoma, Singida Mjini Maghribiu, Kaskazini Pemba na kwa kiapo chake ni jukumu lake kufanya kazi kwa maslahi ya watanzania
7. Hoja ya uadilifu na mapenzi ya nchi yake sambamba na kutokuwa na tamaa ya mali ni sifa anuai alizonazo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo fanya tafiti kabla hujakimbilia kutoa hoja zinazoonyesha kuwa una chuki binafsi na viongozi wa nchi yetu ya Tanzania
Hapa Mkuu umechanganya madawa. Unazungumzia Wapemba gani waloweka matumaini kwa Dk. Bilal?Ni baada ya CC-CCM kubadili hayo matumaini makubwa ya Wazanzibar hasa Wapemba juu ya Dr. Bilal na kumrejesha Karume kama mgombe wa Urais wa Zanzibar kwa ticket ya CCM ndipo Dr. Bilal na Maalimu Seif walipofanya muungano husio rasmi na kuperekea Wapemba kupiga kura za pamoja kumpinga Amani Karume wakimnadi kuwa hawezi kuleta mabadiliko ambayo Wazanzibar wanayataka na kuwa ni kibaraka wa Wabara, huu ndio uchaguzi ulioleta kinachoitwa na wapemba kama machafuko ya Zanzibar, ni vurugu zilizo asisiwa na matumani ya Bilal na Maalimu Seif wakiwadanganya Wazanzibar kuwa ama Seif au Bilal mmoja wao ndio lulu na matumaini ya Zanzibar na kuwa watakapo ingia madarakani OIC ni dakika chache tu! Dr. Bilal na Seif tokea hapo mwaka 2000 walipo chochea kuuwawa kwa Wazanzibari wenzao waliendele kuingia katika chaguzi bila kufua dafu; Dr. Bilal akiomba Urais wa zanzibar kupitia CCM na kuchujwa na Seif akiomba kwa CUF na kushindwa katika Uchaguzi kwa kile ambacho wengi tuna amini kuwa mara zote alikuwa anaibiwa kura.
Hapo kwenye red, ndugu yangu jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Dk Bilal si kiongozi mbabaishaji ama mwenye kujenga chuki, ni kiongozi mwenye mapenzi mema na watu na ndio sababu amebaki kuwa kipenzi cha wengi si tu katika Zanzibar, Tanzania bali popote alipopata kuishi. Kwa msingi huo, utofauti wa yeye na Maalim Seif unabaki katika vyama vyao vya siasa tu lakini wanaunganishwa kwanza na Uzanziba na pia Utanzania. Si vema sana kutangaza chuki kwa watu ambao hawajakutuma kuwatangaza kuwa wanachukiana. Labda wewe ndiye unaowachukia hao wote wawili na unataka kuweka chuki zako kwa kutumia majina ya viongozi hawa.
Maneno yako kweli kabisa na una kila haki ya kutomwamini mtu yeyote kutokana na utamaduni wa Mtanzania (Unafiki) hilo halina shida kabisa isipokuwa nitayarudia maneno ya Lowassa ya kwamba ni bora kuchukua maamuzi magumu ukalaumiwa kuliko kutofanya kabisa! na pia ile ya JK kuhusu akili za mbayuwayu kwamba - Unapoambiwa kitu lazima usiamini moja kwa moja lazima uchanganye na za kwako!..
Haya yote ni mawazo yanayozingatia Uasilia wa watu na mazingira tuliyopo kwani sisi ni wavivu wa kufikiri, kutenda na kikubwa zaidi ni wanafiki. Tahadhali ni muhimu sana.
Mbowe na Zitto ni vijana wadogo sana ambao kiuhakika hawajafikia kujijenga kisiasa na kuwa na mtandao unaotisha.......Lakini sii kazi rahisi kabisa kumwondoa kiongozi yeyote aliyewekwa na CCM na wala sii rahisi kumpata kiongozi bora atakayetokana na CCM kwa sababu hii ni cartel ambayo inamweka mtu kwa maslahi ya chama kama walivyowekwa wote wale waliotangulia. Haiwezekani kiongozi bora atoke CCM ikiwa CC ya cartel ndiyo inamchagua mgombea - Haiwezekani atapigwa chini kwa hali na mali.
...Mipango yote ya ASP ktk chaguzi za Zanzibar, TANU walikuwa nyuma yake na hata Mapinduzi yaliyofanywa na Umma Party yalidumu miezi miwili tu kabla TANU na ASP hawajayateka na kuwa yao, kisha leo hii watu tunashangaa na kujiuliza kuhusiana na Muungano while sote tunaamini Nyerere na Karume wakishirikiana na CIA kunyapua Mapinduzi!.kweli tuna akili timamu kama tunaijua historia ya mapinduzi vizuri?
Binafsi ndani ya CCM visiwani pengine naweza kumwamini Salim A. Salim pekee kwa sababu ya msimamo kama ule wa marehemu waliotangulia kina kina Dr Omar, Jaji Omar, Prof. Haroub Othman waliokuwa na msimamo dhidi ya system kwa maslahi ya wananchi..