hearly
JF-Expert Member
- Jun 19, 2014
- 45,622
- 63,117
duuuuhhNdugu, hakuna Jini zuri au Jema hata moja.
Hebu nitajie wema wa Majini.
Jini likishirikiana na binadamu basi ni katika kufanya kazi mbaya tu za urozi, wizi uhalibifu, vifo, magonjwa nk.
Hao wanaopata pesa za majini zinaambatana na masharti mengi ya kuumiza, kama kutoa makafara ya watu au wanyama wa kula, kutumia hizo hela kwa kufanya uhalibifu, unakuta mtu tajiri lakini haruhusiwi kutumia hizo pesa kwa maendeleo yake, anakatazwa kulala kitandani, kula nyama, kuvaa vizuri nk.
Na mwisho wake anakuwa chizi au kufilisika kabisa.
Ni utajiri wa mauzauza tu ili yakuingize kingi kwenye himaya yao na yaishie kukutesa.
Huyo anayeyajua Majini utakuta hawezi kujinufaisha na hayo majini, na kama hana uwezo wa kutafuta pesa yeye mwenyewe basi anakuwa masikini wa kutupwa.
Ikisemekana Jini ni Jema tusisingizie huo wema yanamtendea Mungu kwani sisi hatuuoni.
Ili kujua wema wa Majini hebu tuweke hapa kama yanashirikiana na binadamu yanamnufaishaje huyo mwanadamu.
Siku moja kuna mtu alipandisha Majini eti yakawa yanadai yaletewe Ubani na Udi ili yafukiziwe moshi wake na pia yachinjiwe kuku ili yale damu yake,
Kuna jamaa mmoja akayaambia, "nyie majini kwanini msifuge hao kuku ili mkitaka damu mchinje na mnywe wenyewe "
Kwanini pia mnapenda kukaa kwa watu masikini ambao hawali sana kuku, badala ya kukaa kwa matajiri wanaokula kuku kila siku na nyinyi muambulie mchuzi " yakabaki nanachimba vimikwala tu
Jini ni kiumbe dhifu sana ukulinganisha na binadamu, Binadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu na kupewa mamlaka ya kuitawala dunia. Jina hana mamlaka hayo ndio maana dunia inajengwa na binadamu na sio Majini.
Kuna siku moja jamaa alipandisha Majini eti yanadai yaletewe Bia ya Safari ili yanywe, tulicheka hadi nusu tuzimie, Jini hana uwezo hata wa kugema Ulansi au Pingu au Mnazi.
Binadamu anapoenda kuomba msaada kwa Jini, Jini mwenyewe huwa kwanza anamshangaa sana huyo binadamu.
Ni sawa na mtu mzima mwenye afya bora anaenda kumwomba msaada mtoto mdogo abebe mzigo mzito ambao huyo mtoto hawezi hata kuunyanyua.
Jini ni viumbe dhifu mno vinaishi kwenye mazingira magumu sana hayawezi hata kujenga makazi mazuri ya kuishi, yanaishi kwenye mapango, baharini kwenye baridi kali, jangwani joto lao mvua yao baridi lao, kwenye vichaka, kwenye mahame, chooni, nk
Binadamu usiogope Jini hata siku moja, haliwezi kukufanya chochote zaidi ya kukutishatisha ukiliendea linakimbia ukiogopa linakucheka.
Jini ni sawa na uchafu tu.
A Shit Hole.