M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Tangu mh Tundu Lissu arejee nchini mwezi Agosti, amekuwa akitoa matamko mbalimbali ambayo kwa kiasi kikubwa yameweza ku reshape approach ya serekali ya awamu ya 5 katika utekelezaji wa mambo yake kadhaa.
Hii imepelekea makundi mbalimbali katika jamii ya Watanzania kunufaika kwa namna moja ama nyingine. Tafsiri ya hili ni kwamba bila ya intervention ya Lissu serekali isingeweza kuchukua hatua stahiki kwa manufaa ya makundi haya.
Makundi haya lazima yatakuwa yameshatambua mchango wa Lissu katika ufanikishwaji wa yale waliyokuwa wanayahitaji kutoka serekalini bila mafanikio kwa miaka yote 5 iliyopita.
Nina uhakika akilini mwao watakuwa wanajiuliza "Kama Tundu Lissu amewezesha haya ilihali hayuko madarakani, je haitakuwa zaidi pale atakapokuwa madarakani? Kwa nini tusimpe nchi kabisa tunufaike pakubwa zaidi?"
1. Walimu 13'000 ambao serekali imetangaza kuwapa ajira mpya - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
2. Wafanyabiashara waliopewa msaada wa sh milioni 100 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
3. Wananchi walioahidiwa kujengewa barabara ya km 46 (Sengerema - Nyehunge) - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
4. Wananchi wa Itigi walioahdiwa kujengewa barabara ya km 16 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
5. Wamachinga ambao Magufuli kawaambia si lazima tena kulipia elfu 20 kupata kitambulisho - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
6. Askofu Niwemugizi aliyerejeshewa passport yake baada ya Lissu kupiga spana - huyu pamoja na waumini wake na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
7. Kuanzia mwezi huu mshahara kima cha chini serekalini umepanda kutoka 170,000 hadi 270,000 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
8. Kwa mara ya kwanza (baada ya kuwa anawafokea tu kwa miaka 5) Watanzania wamemwona mgombea urais wa CCM akiongea nao kwa kuwabembeleza - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
9. Ni makundi hayo tu kwa uchache, lakini yapo mengi unaweza kuongeza mengine.
Hii imepelekea makundi mbalimbali katika jamii ya Watanzania kunufaika kwa namna moja ama nyingine. Tafsiri ya hili ni kwamba bila ya intervention ya Lissu serekali isingeweza kuchukua hatua stahiki kwa manufaa ya makundi haya.
Makundi haya lazima yatakuwa yameshatambua mchango wa Lissu katika ufanikishwaji wa yale waliyokuwa wanayahitaji kutoka serekalini bila mafanikio kwa miaka yote 5 iliyopita.
Nina uhakika akilini mwao watakuwa wanajiuliza "Kama Tundu Lissu amewezesha haya ilihali hayuko madarakani, je haitakuwa zaidi pale atakapokuwa madarakani? Kwa nini tusimpe nchi kabisa tunufaike pakubwa zaidi?"
1. Walimu 13'000 ambao serekali imetangaza kuwapa ajira mpya - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
2. Wafanyabiashara waliopewa msaada wa sh milioni 100 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
3. Wananchi walioahidiwa kujengewa barabara ya km 46 (Sengerema - Nyehunge) - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
4. Wananchi wa Itigi walioahdiwa kujengewa barabara ya km 16 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
5. Wamachinga ambao Magufuli kawaambia si lazima tena kulipia elfu 20 kupata kitambulisho - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
6. Askofu Niwemugizi aliyerejeshewa passport yake baada ya Lissu kupiga spana - huyu pamoja na waumini wake na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
7. Kuanzia mwezi huu mshahara kima cha chini serekalini umepanda kutoka 170,000 hadi 270,000 - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu
8. Kwa mara ya kwanza (baada ya kuwa anawafokea tu kwa miaka 5) Watanzania wamemwona mgombea urais wa CCM akiongea nao kwa kuwabembeleza - hawa na wategemezi wao wote watampigia kura Tundu Lissu.
9. Ni makundi hayo tu kwa uchache, lakini yapo mengi unaweza kuongeza mengine.