Ukiona picha hizi zinakukumbusha nini

Ukiona picha hizi zinakukumbusha nini

Pale unapokuwa umedoea msosi kwa jirani, au umetoka kwenye boli/soccer kucheza mtaani umezamia harusi/kipaimara/hitms katikati
Ya msosi unamuona mama anakukata jicho flani hivi, wewe na yeye tu ndio mnaelewana yaaani ondoka fasta nisikuone hapo.
 

Attachments

  • NAM_090308_644_xw_bigthumb.jpg
    NAM_090308_644_xw_bigthumb.jpg
    11.9 KB · Views: 331
Wapishi wenyewe ni hawa KUCHI? micro wave na azam gas nazi inaungwa kama kitunguu halafu hakuna kufunikiwa hupati ukoko wala matandu/mahaba...wallah huo ukinukia labda uumwagie pafyume ya kichina yenye harufu ya wali nazi ....unamwambia kimwana leo nataka wali wa nazi unakuta bokoboko la ubwabwa tepetepe limewekwa nazi ya azam ile ya pakiti....! Ukiwekwa kwenye sahani vinajitenga azam nazi juu bokoboko la mpunga chini utafikiri vinafanya igizo la sarakasi
Duh! Huwa napitaga kimya kimya,lakini wewe umenichekesha
 
Bi mkubwa alikuwa fundi sana wa kufinyanga vyungu.
Ndani unakuta kuna mitungi miwili ya maji.Mwingine upo nje.
Uwani/chooni chungu kubwa la kuogea.
 
Kata ni chombo kinachotumika kuchotea Maji au Pombe kutoka Mtungini au Pipani au kwenye Ndoo au Kisimani,kilichotengenezwa kwa kifuu cha nazi au kibuyu au kopo pamoja na kipande cha mti/mti mwembamba.
Huo mti hutumika kama mshikio(handle).

Mwenye picha atuwekee.
Asante kwa jibu lako, nami nilihisi ni kitu hicho ila sikuwa na uhakika kama ni chenyewe.
 
hii kitu madam nyamchele ilikuwa ni raw material ya kutengenezea Magari ya bati pia(watoto na vijana). Huwezi kukuta hili kopo jalalani kirahisi.
382b0a5ab325086884f5f89ed43357fe.jpg

la pili kushoto
hii mambo nimecheza mpaka darasa la saba, binti yangu sasa hawezi hata kutengeneza mwanasesere wa vitambaa, kwa maana akitaka anampata wa dukani. watoto wakimujini sikuhizi hata mira ya kuchezea mpaka dukani.
ball.jpg
home made soccer ball.jpg
Stephano Charles na Sahani Richard wakifuma mpira..JPG
 
Maji ya kwenye mtungi ya baridi sana wakati wote. Siku hizi kuna freezers watu wamesahau mambo ya kale.
 
Wapishi wenyewe ni hawa KUCHI? micro wave na azam gas nazi inaungwa kama kitunguu halafu hakuna kufunikiwa hupati ukoko wala matandu/mahaba...wallah huo ukinukia labda uumwagie pafyume ya kichina yenye harufu ya wali nazi ....unamwambia kimwana leo nataka wali wa nazi unakuta bokoboko la ubwabwa tepetepe limewekwa nazi ya azam ile ya pakiti....! Ukiwekwa kwenye sahani vinajitenga azam nazi juu bokoboko la mpunga chini utafikiri vinafanya igizo la sarakasi
Nimejikuta nachekaaaaa
 
Enzi hizo apple na blackberry yalikuwa ni matunda tu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom