Ukiona picha hizi zinakukumbusha nini

Ukiona picha hizi zinakukumbusha nini

Wapishi wenyewe ni hawa KUCHI? micro wave na azam gas nazi inaungwa kama kitunguu halafu hakuna kufunikiwa hupati ukoko wala matandu/mahaba...wallah huo ukinukia labda uumwagie pafyume ya kichina yenye harufu ya wali nazi ....unamwambia kimwana leo nataka wali wa nazi unakuta bokoboko la ubwabwa tepetepe limewekwa nazi ya azam ile ya pakiti....! Ukiwekwa kwenye sahani vinajitenga azam nazi juu bokoboko la mpunga chini utafikiri vinafanya igizo la sarakasi
Ukweli mtupu ndugu. Hizi teknolojia zimekuja na hasara pia kwa upande mwingine
 
Japo mama na dada zetu watanimind kishenzi leo..hasa yule aliyenialika Pasaka
Na hii ndio imesababisha leo hii kila kitu kipo tayari, hukuni nazi unanunua dukani, hupalui samaki ashapaluliwa sokoni, hadi kisamvu kimeshatwangwa na kuchemshwa jamaniiiiiii hadi ndizii zinamenywa sokoni hiki kizazi jama!!!
 
New_Picture_16.png

hii kitu mwisho kutumia saa mbili na nusu usimalize mafuta, lkn watu walikuwa wanapata A
Sema tu kwa sababu ya mazingira lakini moshi na hata kusoma kwa stahili hiyo haipaswi iwe ni kuua bundi manake...................
 
New_Picture_16.png

hii kitu mwisho kutumia saa mbili na nusu usimalize mafuta, lkn watu walikuwa wanapata A

Halafu Mtoto anatoka Ikulu anaenda shule anapata four. Refer Charles Makongoro Julius Nyerere, Abbas Ally Hassan Mwinyi na Mwana Asha Jakaya Kikwete.
 
Nilikuwa najifanya msongo kusoma kwa chemli NAAMBIWA WE JIFANYE KUSOMA ukimaliza mafuta utanunua mwenyewe
 
Dada yangu katunywesha sana klorokwini kwenye mtungi kama huo.. yaani alikuwa akiumwa anasimamiwa kumeza dawa sasa yeye anasimama karibu na mtungi na anaziachia zitumbukie humo na kuyeyukia humo. Maji yanakuwa ya uchachu flani hivi
 
Dada yangu katunywesha sana klorokwini kwenye mtungi kama huo.. yaani alikuwa akiumwa anasimamiwa kumeza dawa sasa yeye anasimama karibu na mtungi na anaziachia zitumbukie humo na kuyeyukia humo. Maji yanakuwa ya uchachu flani hivi
Kwann klorikwini iliwasha mwili?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom