Ukiona Picha hii Unajisikiaje?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
141,433
Reaction score
283,714
Hebu itazame kwa makini halafu tuambie.


Miongoni mwa watu hawa unaowaona hapo hakuna ambaye hajawahi kukamatwa, kufungwa jela au kulogwa, lakini kwa nguvu ya Mungu leo wanadunda.

Utukufu wa Mungu ni wa Ajabu sana.

Je, yale ya Hichilema wa Zambia yatajirudia 2025 nchini Tanzania?
 
Mama ashukuriwe sana kwa kuirejesha na kuimarisha demokrasia ya vyama vingi nchini.

Sasa kinacho takiwa kwa wanasiasa ni kutumia uhuru vyema kwa kuiweka Tanzania mbele sio kupandikiza chuki na kuchochea vurugu.

Wananchi tunataka kusikia siasa za maendeleo sio matusi na kejeli.
 
Hapo simuoni Dr. Slaa,
Maana upende usipende Dr. Slaa ndio nguzo ya chadema,
Dr. ndiye aliye jitolea kwa jasho na damu kukipigania chama.
 
Wananchi gani hawa waliyolaaniwa?(bodaboda)
 
Kama wameweza kutembea kwa uhuru kiasi hiki bila kuhofia watu wasiojulikana inatakiwa tumshukuru sana Mungu kwa kutuletea Rais Samia Suluhu maana amerejesha amani iliyokua imepotea kwa zaidi ya miaka 5 kwa hili jambo kubwa la kurejesha democrasia aisee tutafika na Mama hadi 2030
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…