Ukimya wa viongozi wa dini, mtasema lini?

Ukimya wa viongozi wa dini, mtasema lini?

Haijawahi tokea katika taifa letu kupata Rais jembe kama Magufuli nafikiri 2020 kura ni za NDIYO zote nafikiri atapata ushindi wa 98%
 
Walibweka walivyoambiwa Taasisi za Dini zitaanza kutozwa ushuru kwa bidhaa zinazoingiz nchini.Pale waliungana kuanzia Askofu Gwajima mpaka Mwadhama Cardinal P,hadi Muhashamu Ruwa'ichi akatoka kusema.

Ili kuwatia Pressure TEC na CCT akasema Taasisi za Afya za Dini kama BMC na KCMC ndio zinaongoza kwa wafanyakazi hewa,halafu madaktari wanaofanya hospitali hizo wanalipwa kama wale wa Muhimbili,akasema anapiga panga salary 30% na uhakiki wa wafanyakazi hewa uakondoa madaktari kadhaa walioanza kazi BMC mpaka wahakikiwe.Hapa TEC na CCT chini ya viongozi wao wakatuma ujumbe kimya kimya kuyaweka sawa,Maana ile MoU aliyosaini Edward Lowassa miaka ya 90 akiwa Waziri Ofisi ya Rais ilikuwa inaenda kufaa kifo cha mende.Hizi zote ni mbinu za kutikisa kiberiti ili watu wote hawa wakae kimya.

BAKWATA wakapigwa biti kwenye baraza la Idd,akasema atarudisha mali za Waislam,hapo hapo akatoa pesa za Hijja na kuwapa BAKWATA.Wazee wa BAKWATA waliposikia anakuja "kuwatumbua" kwa kuuza mali za waislamu,matumbo yakawa jotoooo.Nao wakakaa kimyaa,na sasa wameunda Tume ya Kuchunguza Mali za Waislam kwa "uwoga" wa Rais.Hawa nao huwezi sikia wanakosoa maana yeye alianza kuwakosoa moja kwa moja mbele ya Waislam na ukosoaji huu umetishia wengi ndani ya BAKWATA,hawawezi mkosoa.

Hii ndio njia aliyotumia yule jamaa wa Italy ambaye sijui mnumuita "Fascist" hili neno nimelisikia akilitumia sana yule Mwanasheria wa CHADEMA.Mussolin alivyoona atapingwa sana na kanisa katoliki kwa aina ya Utawala wake pale Italy,akaamua kutumia mtego kulitega kanisa...kwa sbb lilikuwa limepokwa maeneo yake,basi Mussolini akayarudisha...Wakasaini na kanisa kitu kinaitwa "LATERAN TREATIES",hapa ndio chanzo cha Vatican kuwa nchi ndani ya nchi,hapa ndio chanzo cha Mapadre na Maaskofu wa Rome kutambuliwa kama "wafanyakazi wa serikali" na kulipwa mishahara na serikali.Hii ikafanya kanisa likae kimyaaa juu ya mambo yote ya Mussolini....Jisomee hapa chini kama sio mvivu wa kusom upate uhondo.Haya mambo hayajaanza leo,historia hujirudia

Once leader, Mussolini had to decide on whether to take on the power of the Roman Catholic Church in Italy or to work with it. He chose the latter. In this way, Italians did not have to have divided loyalties. Therefore, Mussolini worked to get the Roman Catholic Church to accept a Fascist state while he planned to offer the Roman Catholic Church what it wanted.

To gain credibility with the Roman Catholic Church, Mussolini had his children baptised in 1923. In 1926, he had a religious marriage ceremony to his wife Rachele. Their first marriage in 1915 had been a civil ceremony. Mussolini closed down many wine shops and night clubs. He also made swearing in public a crime.

One of the reasons why Mussolini pushed the idea that women should stay at home and look after the family while their husbands worked, was because this was an idea pushed by the Roman Catholic Church. Mussolini voiced his disapproval at the use of contraception – an identical stance to the Roman Catholic Church. Like the Roman Catholic Church, Mussolini also wanted divorce banned in Italy. By doing all of this, Mussolini was trying to bring the Roman Catholic Church onto his side to get its support and give added credibility to his government. However, the relationship was not always harmonious.

In particular, Mussolini and the Roman Catholic Church clashed over who should control education. To ensure that children grew up as good Fascists, Mussolini wanted the state to control this – as it did. However, the Roman Catholic Church felt that it should have this power. Both sides worked for a compromise. The attempt to settle this dispute started in 1926 and it took until 1929 for agreements to be signed. These were the Lateran Treaties. They covered areas other than education.

The Papal States (the name given to land previously owned by the Roman Catholic Church in Italy) had lost all its land in the 1870 unification of Italy. The Roman Catholic Church received £30 million in compensation in 1929 and the Church was given 109 acres in Rome to create a new papal state – the Vatican. The pope was allowed a small army, police force, post office and rail station. The pope was also given a country retreat called Castel Gandolfo.

Another part of the treaty was called the Concordat. This made the Roman Catholic faith the state religion – this was a fait accompli anyway. The pope appointed his bishops, though they had to receive the government’s blessing. Religion had to be taught in both primary and secondary schools. The Roman Catholic Church was given full control of marriage.

When these agreements were signed in 1929, Mussolini’s popularity was at its highest. He had got what he wanted – the support from the members of the public who may not have supported the Fascists but who saw the Roman Catholic Church working with the Fascist government, and that by itself created a tacit acceptance of Mussolini’s government.
 
Hili lina ukweli sana kuwa jk alishambuliwa si kwakuwa alikuwa raisi mbaya, no! Ni kwakuwa alikuwa upande wa pili?? Hata shule za kata aliambiwa anawajengea waislam wenzake! In short ilikuwa ni vurugu tu kila siku! Ni uvumilivu wake tu ndo akamaliza muda wake salama, na kama sio vurugu za makanisa jk angetufikisha mbali sana kimaendeleo kuliko alipotuacha
 
Katiba ipi imesiginwa kwahiyo ulitaka mafisadi yanavyoshughulikiwa TEC wayatete bado hilo mlilo nalo humu CDM limamvii.lazima mjue kuna serikali serious
 
Kuiteta Chadema ni kutetea mafisadi.
Viongozi wa dini hawawezi kutetea ufisadi kamwe.
Acha ife kifo cha asili.


Bora udikteta wa CCM kuliko ufisadi wa chadema.
 
Hata mimi hili linanipa shida. Inaleta hisia mbaya sana kwamba Kikwete alisakamwa kwa kuwa alikuwa wa upande mwingine na makanisani mara nyingi tulikuwa tunaambiwa Kikwete anataka kuifanya hii nchi ya kiislamu na kuingiza serikalini upendeleo kwa waislam.
Ule msisitizo wao wa Amani ni tunda la Haki hausikiki siku hizi!
Wanashindwa kutekeleza ile kazi yao ya kinabii, ya kuonya, kutahadharisha n.k.

Jamani, mapungufu ya JPM yasifanye tuone kuwa JKM hakuwa na mapungufu au alikuwa afadhali 'NO', alikuwa nayo sana tu, wala tusiweke udini hapa, maana huyu wa sasa mkisema udini maana yuko anapendelea wakristu, swali anawapendelea wakristu wote au wale wa dhehebu lake? ukabila je? ukanda je? Kwa kifupi nionavyo mimi ni kuwa ni next to imposible kumpata kiongozi mkweli kutoka CCM, kila mtu ana style yake tu ya kutafuta kik mwanzoni au mida fulani aonekane bora (au kwa kifupi basi kama sio unafiki kila mtu ana mazuri na mabaya yake), mi bado sijamwona ninayemtrust walao hata iwe 50% kuluko wengine waliopita, naona watanzania tunakorogwa tu.
 
Siamini katika udini wa kumkomalia JK na kumnyamazia JPM kwa vile ni mkristu, no! NI WAOGA, WANAOGOPA KUFA MSALABANI KAMA WANAYEJINADI NAYE (YESU) ALIVYOWAFIA WATU WAKE. WANAFIKI WAKUBWA NA MAKANZU MAREFU KUWAAMINISHA/KUWATISHA WAUMI WAO HISIA ZA UYESU WALIOJIVIKA! Hawa niwachumia tumbo tu, machinga walio advanced!

Yaalaaaa sheitwaaaaan wewe,as unataka wahoji nini wakati walichokuwa wanahoji enz za jk ndicho anachoshughulia jpm,enzi za jk nchi ilioza utadhani kulikuwa na mdudu ktk ubongo,taratiibu mtamjua jpm
 
Mtabweka sana.Wenyewe wanamwelewa Raisi kama mchapa kazi anayechapa kazi kwa maslahi mapana ya walio wengi.MMEBAKI NYIE MSIOJIELEWA
Kutumia herufi kubwa ni alama ya ukali, unamkaripia nani?
 
Kuiteta Chadema ni kutetea mafisadi.
Viongozi wa dini hawawezi kutetea ufisadi kamwe.
Acha ife kifo cha asili.


Bora udikteta wa CCM kuliko ufisadi wa chadema.
Kuna mahali mleta mada ametaka CDM watetewe? ndio tatizo la kumeza majibu unayafyatua hata pasipo
 
Katiba ipi imesiginwa kwahiyo ulitaka mafisadi yanavyoshughulikiwa TEC wayatete bado hilo mlilo nalo humu CDM limamvii.lazima mjue kuna serikali serious
Kushikilia kipengele kimoja na kujivika upofu wa mengine ni kipimo tosha cha umbumbumbu. Nano kasema yote mabaya? Hapa tunazungumzia yale mabovu tena ya hatari kwa nini hayakemewi?
Hongera sana mkuu barafu kwa post #11
 
Chakaza unashadadia udini wewe kwann TEC na CCT tu, shauri hata BAKWATA watoe maoni yao. hoja yangu hapa suala la kukosoa na kushauru ni la kila mtu na taasisi pale ionapo mambo yanakwenda ndivo sivyo.
 
Hapa tupate majibu. Baraza LA maaskofu (TEC) na Jumuia ya Kikristo (CCT) ni makundi yanayoheshimika sana.
Kwenye mitandao kumekuwa na tuhuma kuwa pamoja na utawala wa awamu ya tano kuja na speed kubwa ya kusigina katiba na sheria kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi kuliko kipindi chochote toka uhuru hawaja kemea hali hiyo kwa vile muhusika ni muumini wao tofauti na JK ambaye walikuwa wanamkomalia hata masuala madogo madogo.
Taarifa hizo binafsi zimenifedhehesha na kujiuliza jee kuna ukweli? Kama ni hivyo hamuoni mna tuondolea imani tuliyokuwa nayo na taasisi hizo?
Mkuu hao nao wamekuwa kama BAKWATA.
 
Siamini katika udini wa kumkomalia JK na kumnyamazia JPM kwa vile ni mkristu, no! NI WAOGA, WANAOGOPA KUFA MSALABANI KAMA WANAYEJINADI NAYE (YESU) ALIVYOWAFIA WATU WAKE. WANAFIKI WAKUBWA NA MAKANZU MAREFU KUWAAMINISHA/KUWATISHA WAUMI WAO HISIA ZA UYESU WALIOJIVIKA! Hawa niwachumia tumbo tu, machinga walio advanced!
Mzee kwa yule ni rais wa wakristo peke yake na hii nchi ni ya wakrito peke yake je nchi imearibika tanzania peke yake kwani mbona idadi ya waisilamu c mnasema mko wengi kuliko wakristo coz mnazaana sana sasa amuoni ni wakati wa nyie kutumia wingi wenu kupaza sauti kutumia viongozi wenu na mnataka viongozi wa kikristo wafanye ili nyie mjione na muonekane ni wema kwanza toka lini shughuli za dini ziingilie shughuli za serikali kwanza hata nyie si mlimuombea juzi tena akawapa milioni tano au ndo umesaau tayari
 
Hata mimi hili linanipa shida. Inaleta hisia mbaya sana kwamba Kikwete alisakamwa kwa kuwa alikuwa wa upande mwingine na makanisani mara nyingi tulikuwa tunaambiwa Kikwete anataka kuifanya hii nchi ya kiislamu na kuingiza serikalini upendeleo kwa waislam.
Ule msisitizo wao wa Amani ni tunda la Haki hausikiki siku hizi!
Wanashindwa kutekeleza ile kazi yao ya kinabii, ya kuonya, kutahadharisha n.k.
Viongozi wa dini siyo TEC na CCT peke yao hata BAKWATA wanatakiwa kukemea.

Hapo ndiyo ujue viongozi wa dini nao wapo kimaslahi zaidi. Nilitegemea saivi wawe wametoa matamko ya kutetea taifa na kwakuwa hawataki kwa sababu ya woga wao, unafiki na kujipendekeza, watakuja kukumbuka shuka asubuhi na wakati huo watakuwa wamechelewa
 
Kuna mahali mleta mada ametaka CDM watetewe? ndio tatizo la kumeza majibu unayafyatua hata pasipo
Mkuu umeona ee! Hoja nyingi humu hazijibiwi kwa kushirikisha akili bali moyo. Na moyo ukiwa na chuki na jambo fulani basi hilo halina maana kabisa.
Tunazungumzia taasisi hizo kukemea uvunjaji katiba na viashiria vya hali ya hatari wao wanadhani tunasema wabunge mkono Chadema
 
Hili lina ukweli sana kuwa jk alishambuliwa si kwakuwa alikuwa raisi mbaya, no! Ni kwakuwa alikuwa upande wa pili?? Hata shule za kata aliambiwa anawajengea waislam wenzake! In short ilikuwa ni vurugu tu kila siku! Ni uvumilivu wake tu ndo akamaliza muda wake salama, na kama sio vurugu za makanisa jk angetufikisha mbali sana kimaendeleo kuliko alipotuacha

Jakaya alizidi upole kiasi kuwa kuna wakorofi walikuwa wanajifanyia tu mambo yao kama vile kuchoma moto makanisa, kuua viongozi wa dini, kumwagiana tindikali...
katka hali kama hiyo lazima viongozi was dini waseme kitu.

Huyu JPM ameshasema hajaribiwi. Na kuna kila uwezekano kuwa ukimjaribu unaweza uka-RIP. Hakuna cha maandamano ya wanafunzi, sijui ya wanasiasa, au ya akina Ponda kuelekea kidongo chekundu. Hata mihadhara ya kukashifiana dini haipo. Kimya! Reign of terror!
Nani sasa atatoa tamko na kwa sababu gani?
 
Haijawahi tokea katika taifa letu kupata Rais jembe kama Magufuli nafikiri 2020 kura ni za NDIYO zote nafikiri atapata ushindi wa 98%
Kwa wizi ni sawa, lakini kwa haki hawezi kutoboa
 
Back
Top Bottom