Ukimya wa viongozi wa dini, mtasema lini?

Ukimya wa viongozi wa dini, mtasema lini?

Wanaifanya kazi yao. Hawapo kwa ajili ya kuhakikisha demokrasia ipo, wapo kutuongoza kiroho kwa ajili ya maisha yajayo ambayo hayapo bayana. Nisaidie andiko la kitabu chochote linalosema bila demokrasia hakuna kwenda mbinguni.

Do not be myopic, mtu hataishi kwa mkate peke yake
 
Wao kiingialia dissatisfied na wanna lisu,makamba,mlema wao wafanye nn???
 
Do not be myopic, mtu hataishi kwa mkate peke yake
Mbona hujamalizia hilo neno & by the way who is myopic kati yangu mimi na wewe ambaye hujalielewa neno hilo? Mtu hataishi kwa mkate pekee bali kwa siasa si ndiyo?
 
Sasa hivi matamko ya kichungaji yameenda likizo mpaka rais aje muislam...sasa kila kitu oyeee
 
Kipindi wakina-Kakobe wakileta ujumbe kutoka kwa Mungu mliwakebehi sasa mnawatafuta mambo yanapoenda mrama,Wakati wa heri shiriki na wenzako ili shari ikukutapo wakusaidie
 
Ukiona watu unaowategemea wakusaidie wako kimya kwa muda mrefu, lazima wewe ujiulize kama unachofanya kiko sahihi badala ya kuanza kuwalaumu.

Ukimya wao unatoa ujumbe kuwa hicho unachotakifanya hawakiafiki.

Your analysis is too myopic, suppose they are afraid of after effects of their interests?
 
Ukimya wenu unatia mashaka uumini wenu kwa Mungu mnayemtumikia wakati kondoo wanahitaji kauli yenu. Tutawasikia siku ikitangazwa kuwa Tanzania ni nchi ya kiislamu, au inajiunga OIC, hapo maaskofu mtalipuka , maana linahusu maslahi yenu. Hivyo hivyo Masheikh ikisemwa sheria ya ndoa ni mke mmoja mtalipuka kwa vile imegusa imani yenu.
Nyote Kuminywa kwa democrasia hakuwahusu, mko kimya
Kama askofu agustino ramadhan alikuwa mgombea wa urais wa ccm unategemea nini ?
 
Umeona TUCTA, CWT NA TUGHE wana payuka tena? HATA wao hawajui hii ngoma wataichezaje, mdundiko unapigwa, kwaya inapigwa, bongo fleva IPO, viduku vipo, rege IPO, Taarabu IPO, nachi zipo NA..... Sasa wafuate lipi? Kumbuka NJAA haina BAUNSA
Kama sadaka tunazowachangia haziwatoshi bora waachie ngazi wakale ruzuku ya ccm.
 
Vingozi wa dini wanajitambua, hawafati upuuzi wa chadema. Hawa sio kama yule mpuuzi wenu wa ufufuo.
 
Hapa tupate majibu. Baraza LA maaskofu (TEC) na Jumuia ya Kikristo (CCT) ni makundi yanayoheshimika sana.
Kwenye mitandao kumekuwa na tuhuma kuwa pamoja na utawala wa awamu ya tano kuja na speed kubwa ya kusigina katiba na sheria kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi kuliko kipindi chochote toka uhuru hawaja kemea hali hiyo kwa vile muhusika ni muumini wao tofauti na JK ambaye walikuwa wanamkomalia hata masuala madogo madogo.
Taarifa hizo binafsi zimenifedhehesha na kujiuliza jee kuna ukweli? Kama ni hivyo hamuoni mna tuondolea imani tuliyokuwa nayo na taasisi hizo?
 
Mtabweka sana.Wenyewe wanamwelewa Raisi kama mchapa kazi anayechapa kazi kwa maslahi mapana ya walio wengi.MMEBAKI NYIE MSIOJIELEWA
 
Hapa tupate majibu. Baraza LA maaskofu (TEC) na Jumuia ya Kikristo (CCT) ni makundi yanayoheshimika sana.
Kwenye mitandao kumekuwa na tuhuma kuwa pamoja na utawala wa awamu ya tano kuja na speed kubwa ya kusigina katiba na sheria kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi kuliko kipindi chochote toka uhuru hawaja kemea hali hiyo kwa vile muhusika ni muumini wao tofauti na JK ambaye walikuwa wanamkomalia hata masuala madogo madogo.
Taarifa hizo binafsi zimenifedhehesha na kujiuliza jee kuna ukweli? Kama ni hivyo hamuoni mna tuondolea imani tuliyokuwa nayo na taasisi hizo?
Siamini katika udini wa kumkomalia JK na kumnyamazia JPM kwa vile ni mkristu, no! NI WAOGA, WANAOGOPA KUFA MSALABANI KAMA WANAYEJINADI NAYE (YESU) ALIVYOWAFIA WATU WAKE. WANAFIKI WAKUBWA NA MAKANZU MAREFU KUWAAMINISHA/KUWATISHA WAUMI WAO HISIA ZA UYESU WALIOJIVIKA! Hawa niwachumia tumbo tu, machinga walio advanced!
 
Siku hizi hakuna viongozi wa dini kuna wachumia matumbo yao tu ambo wamekuwa sehemu ya watawala, wamekuwa marafiki wa wezi, mafisadi n.k, labda yakiguswa maslahi yao ya misamaha ya kodi ndio utaona matàmko uchwara kibao yanatolewa
 
Hata mimi hili linanipa shida. Inaleta hisia mbaya sana kwamba Kikwete alisakamwa kwa kuwa alikuwa wa upande mwingine na makanisani mara nyingi tulikuwa tunaambiwa Kikwete anataka kuifanya hii nchi ya kiislamu na kuingiza serikalini upendeleo kwa waislam.
Ule msisitizo wao wa Amani ni tunda la Haki hausikiki siku hizi!
Wanashindwa kutekeleza ile kazi yao ya kinabii, ya kuonya, kutahadharisha n.k.
 
Hapa tupate majibu. Baraza LA maaskofu (TEC) na Jumuia ya Kikristo (CCT) ni makundi yanayoheshimika sana.
Kwenye mitandao kumekuwa na tuhuma kuwa pamoja na utawala wa awamu ya tano kuja na speed kubwa ya kusigina katiba na sheria kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi kuliko kipindi chochote toka uhuru hawaja kemea hali hiyo kwa vile muhusika ni muumini wao tofauti na JK ambaye walikuwa wanamkomalia hata masuala madogo madogo.
Taarifa hizo binafsi zimenifedhehesha na kujiuliza jee kuna ukweli? Kama ni hivyo hamuoni mna tuondolea imani tuliyokuwa nayo na taasisi hizo?
waruhusu maandamano eti?
 
Back
Top Bottom