johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 104,319
- 183,528
Baada ya Mwakyembe kusoma report ya Richmond pale bungeni baadae Lowasa aliondoka akiwa kimya, na inasemekana alikwenda nyumbani na hakutaka maongezi na yeyote. Keshoyake Edward akatinga bungeni na mkewe ambaye hadi wakati alikuwa anashangaa ukimya wa mzee,ndipo pale bungeni mzee akachukua maamuzi magumu yaliyomshangaza hadi Mwakyembe mwenyewe! Tendo alilofanya Edward lilinikumbusha Ibrahim baba wa imani alivyomchukua Isaka kimyakimya kuelekea ile madhabahu iliyoitwa baadae Jehova Yire!