UKIMWI bila Pesa ni hatari...

UKIMWI bila Pesa ni hatari...

Siku nilipogundulika nina VVU nilishtuka ila nikaja kuzoea na nikasema sitakuwa kwenye mahusiano na ikawa hivyo; tatizo ni siku za karibuni familia yangu haijui tatizo langu na imeyumba kiuchumi.

Kiukweli naona nafika mwisho, sina hela! Muda mwingine hata ya kula; nahitaji kwenda hospital pia nashindwa.

Mungu anilinde na marafiki mniombee nina wakati mgumu sana!

pole dada angu..Mungu azidi kukupa ujasiri..tafuta mtu unayemuamini..ongea nae usikae nalo moyoni peke ako..utapata kazi and all will be well again.Ubarikiwe
 
Ok, nitakutumia PM nione namna gani naweza kukusaidia uondokane na tatizo hilo.
 
Nimekugongea LIKE sio kwamba nimependa ulivyopata UKIMWI, ila ujasiri wako huo, Basi MUNGU wetu aonaye sirini na haja za mioyo yetu akakujibu siku ya shida yako, mtumaini yeye tu, usimwangalie mwanadamu awaye yeyote, kama yeye aliruhusu uwe hai hadi leo hii basi ataruhusu na MEMA yaje kwako.

Kuna wimbo wa Bukuku-Bahati naupenda sana una maneno yanasema hivi; wewe ni MUNIGU tena ni MUNGU, hivi leo nimejua wewe ni MUNGU, kama ulivyoruhusu mabaya yaje kwangu, ndivyo uruhusu na mema yanipate, kama ulivyoruhusu MAGONJWA yaje kwangu ndivyo uruhusu UZIMA uje kwangu........Ni wimbo ambao una ujumbe mzito sana sana, MUNGU wangu wa Mbinguni ninayemtumaini na kumtegemea akakujibu haja ya MOYO wako leo, akasikie kilio chako, akasikie ombi lako leo, umuitapo akujibu upesi tena Martha Mwaipaja nae anasema hivi, Jaribu kwa mtu si kwamba ni mtenda dhambi ila ni kikombe tu ambacho ni lazima apitie, usimwone mtu anapita kwenye jaribu........Muombe MUNGU aondoe kikombe hicho, hujatenda dhambi ndugu.
Abihudi Misholi kwenye latest CD aliyotoa ana wimbo pia unasema kuwa, hakuna kikombe kinachoponyesha UKIMWI, kikubwa ni TOBA na hii ndio itakuweka huru. Basi nakuombea toba ya kweli, uzidi kuwa huru katika Kristo YESU, sote tuseme AMen
Aaamen.
 
Shikamooooooooooooooooooooooooo kaka Mungi_unataka kumhamishia ghetto mazima ama...?

Nilitaka kumwuliza kama anapata hisia nikaona nyie mtaanza kupiga filimbi
 
Nimeumia mpaka nakaribia kulia pole wote tutapita humu duniani ila ingelikuwa vizuri ukafunguka mana njaa ni hatari hata kama usingeumwa plz plz funguka wadau tujipigepige maisha yetu ni ya mda hapa duniani yamejaa matatizo!ubarikiwe kwa ujasiri
 
Mtumaini Mungu tu ndugu yangu yeye ndo last solution for each and everything,.YEYE NI MUNGU MTENDA MAAJABU DI
ZO SIFA ZAKE.
 
you have extreme complications which are unhelpful, ningekuona wa maana kama ungemuomba na akaunti ya mpesa, tigopesa etc, ili angalau umtupie hapo chochote akabiliane na changamoto zinazomkabili......maswali yako mengine hayana mashiko kabisa jombaa.
Pole sana dada,,, japokuwa maelezo yako hayajanyooka vizuri lakini umeeleweka..

Itapendeza kama ukitueleza in details, uligunduliwa mwaka gani, na kazi uliacha lini?, na je una familia may be mme na watoto, etc

Mungu akuongoze na akuponye kabisa vvu,, kwa imani ninaamini VVU vitaondoka vyote mwilini mwako kwa uwezo wa Mungu wetu..Amina, ubarikiwe sana dada
 
Siku nilipogundulika nina VVU nilishtuka ila nikaja kuzoea na nikasema sitakuwa kwenye mahusiano na ikawa hivyo; tatizo ni siku za karibuni familia yangu haijui tatizo langu na imeyumba kiuchumi.

Kiukweli naona nafika mwisho, sina hela! Muda mwingine hata ya kula; nahitaji kwenda hospital pia nashindwa.

Mungu anilinde na marafiki mniombee nina wakati mgumu sana!

pole sana dada, ILA naomba uendelee kuwa na Moyo wa kijasiri kama ulivyoanza! Samahani ningependa kujua uko wapi? Mimi niko dar naomba pls kama hutaona shida tukutane popote hapa dar kama uko maeneo haya ntakupa namba yangu ya simu
 
admin please mverify kama kweli then wana jamvi watakao guswa wanawaza kufanya chochote
 
Pole sana dada,,, japokuwa maelezo yako hayajanyooka vizuri lakini umeeleweka..

Itapendeza kama ukitueleza in details, uligunduliwa mwaka gani, na kazi uliacha lini?, na je una familia may be mme na watoto, etc

Mungu akuongoze na akuponye kabisa vvu,, kwa imani ninaamini VVU vitaondoka vyote mwilini mwako kwa uwezo wa Mungu wetu..Amina, ubarikiwe sana dada

Je details hizi zitakusaidia nini? Kama umeguswa please wasiliana nae umsaidie,kaishaeleza tatizo lake ni la kiuchumi
 
sasa hapo cha kufanya wewe tumia hii mitandao ya kijamiii kujiuza piga picha za kutamanisha kisha aanza kusanbaza hapo itakua fresh mpaka dawa ipatikane 2015 utaishi nao fureshi

sikiliza ningeamua ni kazi rahisi sana ila mungu ananipenda na ninawapenda wenzangu mimi sio mungu siwezi kukuhukumu ila utapata ugonjwa wa aibu zaidi ya uo
 
sikiliza ningeamua ni kazi rahisi sana ila mungu ananipenda na ninawapenda wenzangu mimi sio mungu siwezi kukuhukumu ila utapata ugonjwa wa aibu zaidi ya uo
achana nae maria...asikusababishie dhambi bure huyo
 
Nimemaliza ba ya sociology and social work nashukuru kwa ushauri wenu coz watu wengi ni fake umu ndani kuna kipindi nilitafuta mwenza mwenye vvu watu tulikuwa tunawailiana siku moja shida yao wanione then basi kumbe hawana ugonjwa
 
Pole dada. Mungu akupe nguvu za kupambana na changamoto na zitakazokukabili hasa baada ya jamii kujua hali uliyonayo.
 
dada yangu ondoa uoga hakuna ambaye hajaasirika na hili gonjwa kama si yeye basi ndugu yake wa karibu.ongea na jamii iliyo kuzunguka nenda kwa watu watoa ushauri .da!sijui nisemeje mungu wetu ni mwenye upendo wa ajabu jiachie kwake utapona
 
igwe usimjaji mtu au usimuhukumu mtu.kwani kwa kiasi ulicho ukumu ndivu utakavyo ukumiwa na mungu ambaye ndiye pekee anaweza hukumu.na mwisho siku moja watu wata kujaji hivyo hivyo
 
Back
Top Bottom