Miss Halima
Senior Member
- Aug 4, 2026
- 170
- 376
"Ukikimbia kuingia chumbani, wanakichoma moto," anasema Fatima, akielezea shambulio la hivi karibuni katika kijiji chake Zamfara, kaskazini magharibi mwa Nigeria. "Ukitoka nje na kuanza kukimbia, wanakupiga risasi."
Watu hao waliojihami kwa silaha, waliofanya shambulio hilo saa nane usiku (saa 02:00), waligawanyika katika makundi ili kuwazingira wakazi, kundi moja kwenye lango la kuingilia kijijini, jingine katikati na la tatu nyuma.
"Walianza kufyatua risasi bila kujali lolote, wakipiga risasi ovyo ovyo," mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 55 aliambia BBC World Service kwa sauti ya chini.
Ilikuwa ni mojawapo ya mashambulio mengi yaliyosababisha taharuki katika jamii hiyo ambayo wakazi wake wengi ni Waislamu na wanaishi kwa hofu ya kutekwa nyara ili kudaiwa fidia.
Fatima anaelezea jinsi mashambulio hayo yanavyofanyika, "Unaweza kuona pikipiki 100, na kila moja ikiwa imebeba watu watatu."
Watu hao waliojihami kwa silaha, waliofanya shambulio hilo saa nane usiku (saa 02:00), waligawanyika katika makundi ili kuwazingira wakazi, kundi moja kwenye lango la kuingilia kijijini, jingine katikati na la tatu nyuma.
"Walianza kufyatua risasi bila kujali lolote, wakipiga risasi ovyo ovyo," mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 55 aliambia BBC World Service kwa sauti ya chini.
Ilikuwa ni mojawapo ya mashambulio mengi yaliyosababisha taharuki katika jamii hiyo ambayo wakazi wake wengi ni Waislamu na wanaishi kwa hofu ya kutekwa nyara ili kudaiwa fidia.
Fatima anaelezea jinsi mashambulio hayo yanavyofanyika, "Unaweza kuona pikipiki 100, na kila moja ikiwa imebeba watu watatu."