Ukijitathmini; Hivi unaishi au Unaishia?

Ukijitathmini; Hivi unaishi au Unaishia?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
34,309
Reaction score
79,941
Kwema Wanazengo!

Sio lengo langu kumkwaza yeyote, lakini embu tujadili kidogo.

Hivi ukijitazama ukajitathmini, Unaishi au Unaishia?

Kama huli chakula ukitakacho, unaishi au Unaishia?

Kama huvai utakacho, unaishi au Unaishia?

Kama hujawahi hata kumiliki usafiri hata wa punda, unaishi au Unaishia?

Kama hujawahi kusafiri nchi za mbali, unaishi au Unaishia?

Kama Akaunti yako haijawahi kufika hata milioni moja achilia mbali milioni kumi, je bado utasema unaishi au Unaishia?

Kama makazi yako na makazi yako ni Kama Karakana, je unaishi au Unaishia?

Kama kazi yako inayokuingizia kipato huifurahii, unaifanya Sura umeikunja, bado utasema unaishi? Mmmh! Labda Kuishia!

Kama ukienda nyumba za ibada kila siku maombi ni Yale Yale, hivi Unaishi kweli au unaishilizia Kama sio kuyoyoma?

Kama hujawahi kulala Hoteli hata ya laki moja Kwa siku, hivi utasema unaishi kweli? Labda kuishilizwa.

Kama hujawahi kuiona Ardhi na milima, na Bahari Kwa chini ukiwa juu ya Ndege, utasema unaishi kweli ndugu yangu, Acha kujidanganya, wewe Unaishia hivyo Kama jua la machweo.

Kama ukienda kununua bidhaa una-bargain, basi jua hauishi Bali unayoyoma.

Embu tutafakari kidogo.

Kuna Wanaoishi
Wanaoishia
Wanaoishlizia
Na mwisho kabisa WALIOISHA

Kuishi, Kuishia, kuishilizia na kuisha
 
Zote hizo ni changamoto zinazotufanya tupate mori kupambana maana hata njaa ni mwalimu wa shibe
 
Mimi naishi japokuwa sina vingi kati ya ulivyovitaja, lakini namshukuru Mungu kwa kunijalia afya njema mpaka leo hii na kuridhika kwa kile ninachokipata na yale ninayoyapitia😊
 
Mimi naishi japokuwa sina vingi kati ya ulivyovitaja, lakini namshukuru Mungu kwa kunijalia afya njema mpaka leo hii na kuridhika kwa kile ninachokipata na yale ninayoyapitia😊


😃😃😃😃😃

Hongera Mkuu Kwa kuishi.
Bila Shaka Una Makazi, unakula utakacho, unavaa ukipendacho, unaenda popote utakapo,

Ila Kama unajaribu hayo upo kwenye kundi la wanaoishia, yaani wanaomalizikia😃😃😃

Lakini Kama kujaribu kabisa umeshindwa basi umeishilizia kabisa na umeisha
 
😃😃😃😃😃

Hongera Mkuu Kwa kuishi.
Bila Shaka Una Makazi, unakula utakacho, unavaa ukipendacho, unaenda popote utakapo,

Ila Kama unajaribu hayo upo kwenye kundi la wanaoishia, yaani wanaomalizikia😃😃😃

Lakini Kama kujaribu kabisa umeshindwa basi umeishilizia kabisa na umeisha
Kuishi ni mtazamo, unaweza kuishia ukiwa na makazi lukuki, chakula cha kila aina, mavazi ya gharama na uwezo mkubwa wa kifedha !
 
Back
Top Bottom