Mema Tanzania
Member
- Feb 23, 2020
- 66
- 65
Kila mwaka ifikapo tarehe 6, Februari dunia huadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga ukeketaji.
Je, unatambua wanawake na mabinti takribani milioni 7.9 wamepitia ukeketaji Tanzania?
Licha ya serikali na wadau mbalimbali kupambana vilivyo na ukeketaji, kuna maeneo bado ukeketaji dhidi ya wanawake na wasichana umeendelea kufanyika kwa kiwango cha juu hasa mikoa ya Manyara, Dodoma na Arusha imeendelea kuongoza.
Ukeketaji ni moja ya ukatili mkubwa wa kijinsia na waathirika wamekumbwa na kadhia kadhaa ikiwemo maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kuathirika kisaikolojia kupoteza damu nyingi na kupelekea kifo kwa baadhi yao.
Kila mmoja wetu anayo nafasi ya kumaliza ukatili wa kijinsia kwa kupaza sauti, kutoa elimu hasa kwa maeneo yenye kiwango kikubwa na kutoa taarifa pindi uonapo vitendo/ viashiria vya kufanyika ukeketaji.
-
🔗 BMC Public Health 2015 & TDHS-MS 2015/16
#SayNoToFGM #ZuiaUkatili
Je, unatambua wanawake na mabinti takribani milioni 7.9 wamepitia ukeketaji Tanzania?
Licha ya serikali na wadau mbalimbali kupambana vilivyo na ukeketaji, kuna maeneo bado ukeketaji dhidi ya wanawake na wasichana umeendelea kufanyika kwa kiwango cha juu hasa mikoa ya Manyara, Dodoma na Arusha imeendelea kuongoza.
Ukeketaji ni moja ya ukatili mkubwa wa kijinsia na waathirika wamekumbwa na kadhia kadhaa ikiwemo maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kuathirika kisaikolojia kupoteza damu nyingi na kupelekea kifo kwa baadhi yao.
Kila mmoja wetu anayo nafasi ya kumaliza ukatili wa kijinsia kwa kupaza sauti, kutoa elimu hasa kwa maeneo yenye kiwango kikubwa na kutoa taarifa pindi uonapo vitendo/ viashiria vya kufanyika ukeketaji.
-
🔗 BMC Public Health 2015 & TDHS-MS 2015/16
#SayNoToFGM #ZuiaUkatili