UKAWA waitisha kikao cha dharura

UKAWA waitisha kikao cha dharura

Hii ni tactic za kuwapa breathing space CCM na kuwatupa off guard through deviatonal tactics- mahali ambapo yuko Lowassa ogopa sana ni akili tu inatumika-si campaign mnaona inavyokwenda watu kama wanasuasua-wakiingia mikoani maximum impact hadi hatuamini-na bado nyepesi nyepesi za chini ya carpet-LOWASSA has still got an ace in his sleeve na habari zinasema mkulu has got wind of this-hiyo siku nchi itasimamia vidole


Endelea kujipa moyo
 
Kweli CCM choka mbaya, mwaka huu mmelaaniwa. Rudini tena kwa aliewatuma, hizo sio propaganda za level ya kuwekwa JF. Mwambieni na hiyo mmefail awape technic nyingine.
 
Haaa, ukiwa wameshikwa vibaya, wamebakia kutapatapa tu.
 
UKAWA IPO IMARA,WANAFIKI NA MAADUI HAMUWEZI PATA CHOCHORO LA KUUVUNJA UMOJA WETU,CHAGUA UKAWA,CHAGUA LOWASSA,HUTA JUTAi
 
Watazidi kuvurugana wao kwa wao, shughuli huku inaendelea.
 
Ukawa ni jumuiya za mpito, zinavuma na kusinyaa ghafla, tatizo ni tamaa ya madaraka.
 
UKAWA KUWA NA KIKAO CHA DHARURA

Kufuatia hali kuwa tete ndani ya kambi ya UKAWA, viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo wanatarajia kukutana kwa dharura kesho kujadili mwenendo wa umoja wao.

Taarifa za ndani ya UKAWA zinasema Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ambaye yupo nchini Marekani atalazimika kurudi haraka nchini na inaelezwa huenda akaingia usiku huu au mapema kesho kwaajili ya kikao hicho cha dharura ambacho kitaamua hatma ya umoja huo.

Mbali na Mbowe, timu yote ya kampeni za mgombea urais na mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza wanatarajia kusitisha kampeni na kurudi Dar es Salaam kwa siku ya kesho hadi watakapopata mwafaka wa masuala yanayobishaniwa ndani ya umoja huo.

Taarifa zinasema, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa viongozi wa CUF kulalamikia kutotimizwa kwa makubaliano yaliyofikiwa wakati wanaungana na kupjnga jinsi Chadema wanavyoendesha umoja huo hadi kufikia hatua ya mgombea mwenza wa Chadema Juma Duni kutangaza kujitoa kwenye chama hicho na inaelezwa kikao hicho kitatumika kumuomba asijitoe.

CUF wanalalamikia UKAWA kuendeshwa na mtu mmoja ambaye ni Mbowe badala ya kuendeshwa kama taasisi na amekuwa akichukua maamuzi bila kushirikisha wengine.

"UKAWA ni Mbowe na yeye ndo anaendesha mambo anavyotaka kwa maslahi yake na mkwewe mzee Mtei. Huu ni uhuni ambao tulikuwa tunausikia tu ila leo tunajionea baada ya kuingia ndani" alisema kiongozi mmoja wa CUF ambaye alisisitiza kama Mbowe lengo lake lilikuwa ni kuua CUF amefanikiwa ila dhambi hiyo itamtafuna na watahakikisha Chadema haibaki salama

Chama ambacho hakina mbele wala nyuma hatuwezi kukipa madaraka.
 
Mbowe kashachukua kilichochake, wafuasi hawajitambui wao wanazidi kubuluzwa tu, kweli nimeamini CCM itabaki madarakani milele.
 
Chama kila kukicha ni migogoro, wakubwa wanagawana wenyewe afu shida tunapata sisi wanainchi wa kawaida. Hata tutakuwa makini kutokubali ujinga huu kamwe.

toka uwepo hapa tz chama gani kimewah kukuletea hela nyumbani kwenu zaid ya kukomaa na shida ww na familia yako pumba tupu kama unaiman kiongoz wa taifa lolote lile atakutatulia shida zako bila ww kujiongoza ktk maisha yako na kupambana
 
Hivi kuna mtu makini atafanya maamuzi ya kuchagua kwa kuangalia mbowe makaidi na mbatia wanaelewana ama la! mimi nitachagua mabadiliko hata wakigombana niliowataja.
 
mbowe kama ameenda marekani anatuacha tunapambana wenyewe hapo kuna shida huko juu, kibaya zaidi mgombea wetu ni shida kujieleza mwenyewe.

mimi simsemi vibaya mh.lowasa, lakini toka aanze kampeni hajawahi kutawala jukwaa isipokuwa hisia za wananchi ndiyo zimetawala majukwaa.
Kuna clip zinaoneshwa, daah....i wish tumwombee awe na uzima, swala la kupata uraisi kupata na kukosa yote yanamhusu kama candidates wengine
 
Nimemwonyesha Mwenyekiti hii posting amecheka sana. Anasema hicho kikao cha dharura labda amekiita mwenyekiti wako siyo yeye. Anasema kikao chochote atakachofanya hakitakuwa cha dharura kwa sababu CDM ina mpangilio. Mwenzako pia mapema alisema kuwa Mbowe yuko Marekani kumwomba Dr. Slaa msamaha. Hii forum watu kama wewe mnaifanya iwe ni mahali pa majungu badala ya kuitumia kama inavyotakiwa-mahali pa kubadilishana mawazo. Mpaka mwezi wa kumi ufike mtapata shida sana.

Tehtehteh okey, kwa hiyo hata ile press ya nccr mageuzi juzi star tv ilikuwa ni uzushi sio?? Yaan mabavicha bana, sijui mbowe kawalisha nini aisee.. Daah,!! Mkapa alikuwa sahihi kabisa...
 
Jamani hili VUGUVUGU la UKAWA halina muelekeo.halina makubaliano kisheria.halikusajiliwa.mwisho kila chama kitabaki chenyewe
 
Yani kiitendo tu,Cha dharura kuwa"Dharula"Imeonekana aliyeandaa uzushi huu alivyo kilaza
Cc Moderator
yaani wewe unadhani Dhalula ndiyo sahihi na siyo dharura, LMAO,Sasa sijui kilaza nani aliyeandika Dharura au aliyedhani Dharula ndiyo sahihi?wenye kujua kiswahili wanisaidie.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom