Watalipwa,Hamna sharia inayozuia kulipwa. Mkwara tu huo...Kuna wachezaji mpira wao wapo bench tokea ligi inaanza mpaka inamaliza. Na wanapata mshahara na posho pia sasa kuna kosa gani kwa wabunge wa Ukawa kuidai haki yao? Mbona kuna wabunge wanachangia kuvuliwa kibarahashia tu na posho wanapewa.
Wabunge njaa..Nimekua nikiwaunga mkono lakini hapo wamekoseaa sanaaaaa.
Na hiyo itakuja kuwatesa sanaaaa hapo mbeleni. Wataonekana wanaeka maslahi yao mbele kuliko ya wananchi.
Zitto is the only one who is leading the way sasa hivi kwenye kuleta mapinduzi na mabadiliko ya kweli. Hawa wengine naanza kupata wasiwasi nao.
Wanalala hotel za Buku 5000 na kushindia mihogo.. Mag noma sanasasa kwa nini walikataa posho pindi spika alipowanyima, wakati wanajua ni haki yao? au hawakuielewa katiba inasemaje juu yaposho. AU UKATA UMEZIDI. MAGU KAFICHA PESA.
kwani bungeni mwenye jukumu la kuratibu na kuongoza bungeni ni nani si spika?
ikiwa hawamtaki naibu spika kwa nn wasilete hoja bungeni na kuipeleka mahakamani, mpk wazunguke mitaani inamaana hawajui namna ya kumuengua spika. katiba inassema spika atachaguliwa na wabunge pia kutenguliwa na wabunge kwa kufuata sheria, mbona wao hawafati sheria
Ukawa njaa kali,mikopo ya magari na mikopo ya mishahara,marejesho ni lazima upate posho kwa sababu safari hakuna,lazima sasa wanalaumiana kuingizana mkenge,Tulia bado anapeta na wala hana dalili za kujiuzulu achilia mbali kung'olewa
Halafu mahakama haina mamlaka na yanayozungumzwa bungeni labda kama ni kufafanua vifungu vya katiba,alichoamua naibu spika akiwa kwenye kiti hakihojiwi na chombo chochote,hiyo kesi itaanguka siku ya kwanza tu,ukawa waache kuwadanganya wafuasi wao
Mbowe anawaburuza wenzake wakati yeye ana vyanzo mbadala vya mapato ikiwemo hata access ya ruzuku,hawa wengine wenzangu na mimi ndio watakua wamelianzisha hili la kwenda mahakamani.Basi haya kama ni wa Lumumba waweke no zao apa warushiwe buku 7 zao
Hivi wewe wakati unasoma primary ilikuwaje,wewe ukiitwa jina ukaitika nipo ata kama ulikuwa,unasinzia,itakuwa sawa na yule ambae hayupo darasani?Kwani wale waliokaa pale na kunyamaza kimya wamefanya kazi gani? Au yule wa kujenga mnara wa push up, ingekuwa watu wanalipwa kwa performance na zinatoka mfukoni mwako, ungempa ngapi yule?
kama wana madai wana haki lkn ninashauri waanze kumshitaki mwajiri wao office za labour ikishindikana waende baraza la upatanishi na usuluhishi ndiyo wakikwama waende mahakamani#JamboLEO Wabunge UKAWA kwenda mahakamani baada ya kunyimwa posho kutokana na kuingia bungeni kusaini kisha kutoka
View attachment 363530
Nasoma kitabu cha darasa la nne 1997 SIZITAKI MBIVU HIZI.
Vipi kuhusu KITWANGA tangu alipotumbuliwa hakuwepo Bungeni je wewe mleta mada unaweza kutupatia taarifa je huyo KITWANGA alilipwa posho au hakulipwa posho? na tunajua Ndugai hakuwepo bungeni je na yeye kapewa posho za vikao vya Bunge au kanyimwa?Wabunge wa UKAWA waliositishiwa posho zao baada ya ule mchezo wa kutoka bungeni sasa kudai posho zao mahakamani.
View attachment 363532
Hiii sijui imekaaje mtu kuhangaikia pato ambalo hujalifanyia kazi.
Posho kupata ni mpaka uhudhurie kikao au uingie na kusaini, wale hawakuwepo kabisaTutapata ufafanuzi soon
Alafu wale wa Bunge wa CCM waliopewa mpaka barua na chama kwa kutohudhuria vikao nao walinyimwa posho?
hivi wewe ni mlipa kodi katika nchi hii kweli.? nina wasiwasi. utakuwa under age. hivi walipwe kwa kitu gani. si bora pesa hiyo ipelekwe kununulia madawati mashuleni au madawa hospitalini. ni nani aliwatuma wagome.? kuna yeyote alienda kwenye jimbo lake na kuomba watu wake kuwa anaenda kugoma bungeni na akakubaliwa. ni lazima tujue wabunge wameomba kazi kwa wananchi majimboni. wakapewa kazi na ni lazima waende bungeni kuwafanyia kazi. na sio kwenda kugoma kula na kulala tu. nani anagharamia muda huu uliopotea. tena ningeshauri hata mishahara yao ingekatwa kwa siku zilezote ambazo hawakufanya kazi.
Kitabu cha Kusoma Darasa la III/73. Shairi 'Sizitaki Mbichi Hizi'. Mchoro Sungura amekodolea macho ndizi mbivu. Kitabu kina mashairi 2; shairi la kwanza ni la Sikili (mtoto mvivu).
Sikili mimi maskini uvivu wangu nyumbani, nikiwa humu njiani nakufa hapa kwa nini,
Sadiki sasa ashiba chakula kingi kwa baba, nirudi tena nyumbani nakufa hapa kwanini?
Posho: Tulia alitumia Mwongozo wa Spika wa Bunge wa 2008 (precedence) kuamua UKAWA wanyimwe posho. Mahakamani watakwenda kupoteza muda mwingine. Walaumu uongozi wao na wao wenyewe kushindwa kujiongoza vizuri. UKAWA Bungeni have lost both the battle and war, period. Tunaojua tuliwashauri tangu mwanzo kuwa they were heading and trending to fail.
Tulia alitumia sheria ya Mungu inayosema asiyefanya kazi na asileWako sawa kabisa! Kuna kanuni/sheria inayosema usipohudhuria vikao vya bunge unanyimwa posho. Sheria ipi aliitumia Tulia kuwanyima posho? It makes sense , ni kuwa watu hatujui haki zetu. Ni sawa kama upuuzi anaoufanya Fastjet kuahirisha safari bila kuwa na alternative air transport or accommodation to the would be passengers! Only recently one advocate has approached the court to that effect and has won the case!
Nadhani hukunielewa ndugu. Shairi la kama mnataka mali:Sio kweli, umesahau pia kama mnataka mali mtazipata shambani, sizitaki mbichi hizi, sadiki na chitemo