Ukawa kuandamana nchi nzima

Ukawa kuandamana nchi nzima

kesho wanakongamano tena Itv,kisha keshokutwa wataandika strong worded letter kwa Rais wakimwambia asitishe bunge haraka ama sivyo wanaingia msituni.

Dar es Salaam kuna msitu? au wanaenda kuanzia HAI na HIFADHI YA NGORONGORO?
 
tatizo nin mpaka tunataka kufika hapa. Wananchi tunataka serikari moja itakayoleta usawa katika nyanja zote muhimu
 
kama wanaona mahakama za Tanzania hazitawatendea haki, waende the hague kabisa waache kutuzingua na kiswahili chao cha NJI HII
 
Kuna angalizo lisemalo, "mtu yeyote akikueleza jambo la kijinga na kipuuzi akafahamu kabisa jambo analokueleza ni la kijinga na kipuuzi nawe pia ukalikubali jambo hilo, basi atakudharau sana".

Hili Tamko nila kijinga na kipuuzi na kama tutalikubali wakati tunafahamu nila kijinga na kipuuzi, basi hiki kikundi kinachojiita UKAWA kitatudharau sana.

Hiki kikundi kinadai kuwa Rais Kikwete hawezi kuongoza halafu hapo hapo kinataka kikutane na Rais Kikwete.

Hiki kikundi kinadai CCM haiwezi kuisimamia serikali yake halafu hapo hapo kinataka kikutane na CCM.

Wenye hekima wanafahamu kuwa, kumpuuza mpuuzi ni adhabu inayojitoshereza.

Rais Kikwete amekipuuza kikundi kinachojiita UKAWA na adhabu ya kuwapuuza imeanza kuwaingia kwenye akili zao, ndiyo maana wameanza kupiga kelele.

Kwa kupitia hii video na maandiko, Rais Kikwete aliwaambia hivi,

[video=youtube_share;7Rnlngg0x6A]http://youtu.be/7Rnlngg0x6A[/video]


Ndugu Wananchi;
Tulizibuni ngazi hizi nne kwa dhana kwamba kile ambacho hakikuonekana au hakikuwekwa sawa katika ngazi moja kitaonekana na kurekebishwa katika ngazi inayofuata katika ngazi zile tatu za mwanzo. Na, iwapo Katiba iliyotungwa haitawaridhisha wananchi wanayo haki ya kuikataa. Kwa kufanya hivyo, wananchi ndiyo waliopewa turufu ya mwisho.

Ndugu wananchi;
Kwa kweli, napata shida kuelewa mkanganyiko unatoka wapi na hasa wale wanaoongoza kuhoji mamlaka ya Bunge Maalumu kuwa ni wale wale waliotunga Sheria ya Mabadiliko ya Katiba tena hatua kwa hatua. Nashangazwa zaidi ninapoona wale wale waliotunga Kanuni za Bunge Maalumu ndiyo wanaoongoza kuhoji uhalali wa kile walichokitunga.

Kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, Ibara ya 33 (8) inasema: Nanukuu: "Wakati wa mjadala, Mjumbe yoyote anaweza kutoa mapendekezo ya marekebisho, maboresho au mabadiliko yaliyomo katika Sura za Rasimu ya Katiba zinazojadiliwa kwa utaratibu ufuatao: (a) Ikiwa ni marekebisho, maboresho au mabadiliko yanayobadilisha jambo la msingi, au yanayobadilisha maudhui ya Ibara, mapendekezo ya marekebisho yatapelekwa kwa maandishi kwa Katibu siku moja kabla ya mjadala wa Ibara husika. (b) Ikiwa ni marekebisho madogo, ambayo hayabadili msingi au maana, mapendekezo ya marekebisho yatawasilishwa na mjumbe wakati wa mjadala baada ya kupata ruhusa ya Mwenyekiti". Mwisho wa kunukuu.

Kanuni hii ilipotungwa, Wajumbe wote wa Bunge Maalumu pamoja na wale ambao baadae walisusia vikao vya Bunge walikuwepo Bungeni na walishiriki kuipitisha. Tena basi, baadhi yao walikuwa Wajumbe wa Kamati ya Kanuni iliyopendekeza Kanuni hizo. Unapowaona watu wale wale sasa wanakuwa vinara wa kuhoji mamlaka ya Bunge Maalumu la Katiba, unajiuliza maswali mengi kuhusu watu hao bila ya kupata majibu yaliyo sahihi na kutosheleza akili na ufahamu wetu.

Ndugu Wananchi,
Unaposoma Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Kanuni za Bunge Maalumu, hii ni dhahiri kwamba wote walikuwa na uelewa wa pamoja kuhusu mamlaka ya Bunge Maalumu ya kujadili Rasimu iliyoandaliwa na Tume na kutunga Katiba inayopendekezwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura.

Kinachojadiliwa Bungeni ni Rasimu ya Tume

Ndugu Wananchi;
Yapo madai yanayotolewa na kuenezwa na Wajumbe waliosusia Bunge Maalumu la Katiba kwamba kinachojadiliwa Bungeni siyo Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ndiyo maana basi wanaweka sharti la kujadiliwa Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba ndipo warudi Bungeni. Madai haya nayo yananipa taabu kuyaelewa. Ndugu zetu hawa walishiriki siku zote 19 za Kamati 12 zilipokutana kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita za Rasimu ya Tume. Halikadhalika. walikuwepo na kushiriki kwa ukamilifu wakati taarifa za Kamati, tangu ya Kwanza mpaka ya 12, zilipowasilishwa kwenye Bunge zima. Aidha, na wao walishiriki kutoa maoni ya wachache kwa dakika 20 na kutoa ufafanuzi kwa muda wa dakika 30 kwa kila Kamati. Haya maneno ya sasa kwamba kinachojadiliwa Bungeni siyo Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba bali nyingine kabisa ambayo wanadai eti ni ya CCM yanatoka wapi.

Mimi nadhani kuwa huenda katika Kamati kumefanyika marekebisho kwenye Rasimu ambayo hayakuwapendeza. Kama hivyo ndivyo, wawe wakweli kuhusu jambo hilo kuliko kusema mambo yasiyowakilisha ukweli halisi wa Rasimu inayojadiliwa. Matokeo yake ni kuwafanya wafuasi wao na wapenzi wao na hata watu wengine waamini kuwa kinachojadiliwa siyo Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba bali nyingine tena ni ya CCM. Jambo hilo si kweli na wenyewe wanajua kwamba si kweli ila sijui kwa nini wameamua kupotosha ukweli.

Ndugu Wananchi;
Kinachonishangaza, zaidi ni kwamba, kama hawakuridhishwa na yaliyofanyika, kwa nini wasingetumia mifumo waliyojitengenezea wenyewe kwenye Kanuni kumaliza tofauti zao? Kanuni zinaelekeza kuwa mambo wasiyoridhika nayo yajadiliwe kwenye Kamati ya Mashauriano na Maridhiano. Ukiacha mifumo ya maridhiano ndani ya Bunge ukaenda nje kwa wananchi au vyombo vya habari na mitandao si jawabu la tatizo.
 
mkuu pamoja na kwamba UKAWA wanaudhi na hawajui walifanyalo, wapuuze tu wala usiwape credit kwa matusi, dawa ya watu kama UKAWA ni JK, wanapandisha mori, mzee yeye kimya anawaangalia tu wakichoka utasikia mkuu tunaomba kuja kunywa juice, naye anawaambia njoooni, wakitoka wameinamisha vichwa kama mabundi
mkuu haya makenge yanakera mpaka basi ndo maana nikamuuliza kama atamualika mama yake kwenye maandamano ili nijue yupo makini.
 
we ask the constitution assemble to STOP IMMEDIATELY or we are going to write a VERY ANGRY letter to presdent Jk telling him so.
 
kama wanaona mahakama za Tanzania hazitawatendea haki, waende the hague kabisa waache kutuzingua na kiswahili chao cha NJI HII

Mwenye kiswahili hicho si 'mtu' wa Lumumba anayefanya kazi zenu nje ya ofisi zenu.
 
Kuna angalizo lisemalo, "mtu yeyote akikueleza jambo la kijinga na kipuuzi akafahamu kabisa jambo analokueleza ni la kijinga na kipuuzi nawe pia ukalikubali jambo hilo, basi atakudharau sana".

Hili Tamko nila kijinga na kipuuzi na kama tutalikubali wakati tunafahamu nila kijinga na kipuuzi, basi hiki kikundi kinachojiita UKAWA kitatudharau sana.

Hiki kikundi kinadai kuwa Rais Kikwete hawezi kuongoza halafu hapo hapo kinataka kikutane na Rais Kikwete.

Hiki kikundi kinadai CCM haiwezi kuisimamia serikali yake halafu hapo hapo kinataka kikutane na CCM.

Wenye hekima wanafahamu kuwa, kumpuuza mpuuzi ni adhabu inayojitoshereza.

Rais Kikwete amekipuuza kikundi kinachojiita UKAWA na adhabu ya kuwapuuza imeanza kuwaingia kwenye akili zao, ndiyo maana wameanza kupiga kelele.

Rais Kikwete aliwaambia hivi,

[video=youtube_share;7Rnlngg0x6A]http://youtu.be/7Rnlngg0x6A[/video]

Waache watape tape mkuu
 
mkuu haya makenge yanakera mpaka basi ndo maana nikamuuliza kama atamualika mama yake kwenye maandamano ili nijue yupo makini.
nasikia yule mama mwenye macho mekundu wanamwita kijo bisimba atakuwemo kuandamana.
 
hawana lolote kazi kuhamisha goalpost. shida ya cdm sio katiba ila kufanya siasa waingie ikulu. ccm wanajua na wana ozoefu zaidi kufanya siasa. muhimu zaidi ccm wana ridhaa kubwa ya wananchi na hawalazimiki kua na muafaka na cdm kwa jambo la msingi katika sera yao. ukawa walijue hili na waepuke kuleta fujo bali kungojea kama watapewa ridhaa kwenye uchaguzi.
 
Afu hili ndio tatizo la Vyama kuongozwa na watu wehu. Kama wanaweza waandamane tu JK amewazoea na hatasitisha kitu. Polisi watafanya kazi yao kama ile ya Waislamu 2012
 
Back
Top Bottom