ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Sijui ni makusudi au bahati mbaya au coincidence. Ufukunyuku wa muda mfupi niloufanya nimegundua jambo hili limeanza kufanyika kwa kasi ya ajabu sana na baada ya muda kuna uwezekano yale majina ya familia yenye asili ya kibantu yatapotea kabisa na kubaki na yale ya kimagharibi mfano Stephen, McDonald, Clinton, Wycliff n.k.
Jamii na koo nyingi sasa zimeanza kuachana kabisa na majina yao ya kiasili kama Jilala, Kifurugobe, Matata, Kasenene, Mkude. Mfutakamba. Bado sijajua sababu hasa ni nini watu wanaona kuendelea kutumia majina yao ya ukoo ya kiafrika na ya asili. Najua mko mtakao bisha lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hili linatokea kwa kasi ktk jamii ya baadhi ya makabila hapa TZ.
Majina ya watu tuliyoyazoea kama Janeth Kamugisha, Catherine Massawe, Juieth Munisi, James Hawala, Edson Karumekenge, Kelvin Limbwata yameanza kupotea na tunaanza kuona yanapotea kwa kasi sana, sasa watu wanajiita Janeth Clinton, Catherine McDonald, Eveline Stephen, Juieth Williams, yaani ki westeni zaidi kuliko kiafrika. Mbaya zaidi linapokuja suala la kuomba kazi maofisini hapo ndo utashangaa majina ya ukoo ya kibantu ndo hutayaona kabisaaaaaaa, ila mtu akipata kazi tu, ndo anaanza kulazimisha sasa ofisi ilitambue rasmi jina lake la ukoo lenye lafudhi ya kiafrika.
Kama haujui basi nakupa 'hint' kwamba kwa sasa bogo kuna makabila mawili hapa Bongo ambayo kwayo tabia hii miongoni mwa watu wake yanaongoza kwa kuficha majina yao ya ukoo ya kiafrika, lakini huyafufua na kutaka yatumike rasmi pindi wanapopata ajira.
Nakaribisha critics na maoni yenu!
'Buriani'!
Jamii na koo nyingi sasa zimeanza kuachana kabisa na majina yao ya kiasili kama Jilala, Kifurugobe, Matata, Kasenene, Mkude. Mfutakamba. Bado sijajua sababu hasa ni nini watu wanaona kuendelea kutumia majina yao ya ukoo ya kiafrika na ya asili. Najua mko mtakao bisha lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hili linatokea kwa kasi ktk jamii ya baadhi ya makabila hapa TZ.
Majina ya watu tuliyoyazoea kama Janeth Kamugisha, Catherine Massawe, Juieth Munisi, James Hawala, Edson Karumekenge, Kelvin Limbwata yameanza kupotea na tunaanza kuona yanapotea kwa kasi sana, sasa watu wanajiita Janeth Clinton, Catherine McDonald, Eveline Stephen, Juieth Williams, yaani ki westeni zaidi kuliko kiafrika. Mbaya zaidi linapokuja suala la kuomba kazi maofisini hapo ndo utashangaa majina ya ukoo ya kibantu ndo hutayaona kabisaaaaaaa, ila mtu akipata kazi tu, ndo anaanza kulazimisha sasa ofisi ilitambue rasmi jina lake la ukoo lenye lafudhi ya kiafrika.
Kama haujui basi nakupa 'hint' kwamba kwa sasa bogo kuna makabila mawili hapa Bongo ambayo kwayo tabia hii miongoni mwa watu wake yanaongoza kwa kuficha majina yao ya ukoo ya kiafrika, lakini huyafufua na kutaka yatumike rasmi pindi wanapopata ajira.
Nakaribisha critics na maoni yenu!
'Buriani'!