DodomaTZ
Senior Member
- May 20, 2022
- 161
- 200
JINA : HAMIS MBWANA MZENGA
Awali ya yote kwa niaba ya wahanga wenzangu, Tunamshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kuwatetea wanyonge. Tunaimani na kauli mbiu yake ya KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE.
Sisi tuliokuwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, tunakuomba Mama yetu mpendwa Mhe. Samia Suluhu Hassan utusaidie kupata haki yetu ambayo tumekuwa tunahangaika kwa viongozi wa Serikali ambao wamekuwa wanashindwa kutusaidia tena ni viongozi wa ngazi ya juu.
MZENGA
Mamlaka ya Bandari TPA iliomba askari kutoka JKT katika Makambi ya JKT Mgulani na JKT Mlalakuwa mwaka 2009. Maombi ambayo JKT walijibu kwa kuwaeleza Bandari kwamba wanavijana 81 ambao 28 ni darasa la 7, na 28 kidato cha nne, kutoka JKT Mgulani na vijana 25 kutoka JKT Mlalakuwa, Bandari wakajibu walete kwa barua hizi hapa.
KWA MASIKITIKO
Katika zoezi la uhakiki wa vyeti tulitakiwa kupeleka vyeti vya kidato cha nne na muajiri wetu Bandari. Tukawajibu hatuna hivyo vyeti kwani hata ajira zetu tumeajiliwa tukifahamika ni darasa la saba (7).
Hatimaye tarehe 15/09/2018 tulipewa barua ya kufukuzwa kazi kwa kosa la kujipatia ajira pasipokuwa na sifa sitahiki kwa upande wetu tunashangaa kosa la kufukuzwa kazi kwa kusema tumejipatia ajira wakati wao ndio waliotufuata kwenye makambi ya JKT tuliokuwa tunafanya kazi.
Tumeitumikia Mamlaka kwa miaka kumi (10) hadi tunafukuzwa kazi muda wote wa ajira yetu na ndani ya mikataba yetu ya ajira kulikuwa na kipengelecha cha 35% ya mishahara yetu tunalipwa kwa ajili ya kodi ya nyumba. Kwa masikitiko makubwa baada ya kufukuzwa kazi mamlaka ya Bandari imetulipa malipo madogo mfano kama mimi HAMIS MZENGA nimelipwa Tsh. 3,200/= tu ikiwa ni nauri ya mimi na familia yangu, mshahara wa mwezi mmoja (1) badala ya NOTICE na gharama za kufungasha mizigo 238,000/= jambo ambalo nimeshindwa kuelewa hii pesa niliopewa mbona haifanani na muda wangu wa utumishi? Na hata muda niliokaa kusubiri hayo malipo.
OMBI
Tunakuomba Mhe. Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania utusaidie kupata stahiki zetu pamoja na pesa za kujikimu huku tukisubiri kurudishwa maskani tulikotoka. Kwani tumefanya kazi kwa uaminifu kwa zaidi ya miaka kumi (10).
Tumekuwa tukikutana na majibu ambayo kwa upande wa Mamlaka ya Bandari wanasema wametulipa malipo hayo kutoka na maelekezo ya serikali, na malipo yenyewe ni kama hayo ya Tsh. 3,200/=. Kwa muda wote wa utumishi wangu au wetu kwa ujumla. Hivyo kupitia Mama yetu mpendwa tunaimani tutapata stahiki zetu kwa muda wote tuliofanya kazi kwani sisi tuliombwa kuja kufanya kazi ambayo tulifanya kwa uaminifu mkubwa lakini ndio tulipwe Tsh. 3,200/=. Mama yetu wewe ndio tumaini letu kwasasa
Mwisho MWENYEZI MUNGU amlinde na kila jambo Amiin
KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE
MSEMAJI
Awali ya yote kwa niaba ya wahanga wenzangu, Tunamshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kuwatetea wanyonge. Tunaimani na kauli mbiyu yake ya KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE
Tumelazimika kuwaita Waandishi wa Habari ili muweze kutufikishia malalamiko yetu kwa Mama yetu na Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tunaamini Mhe. Rais mama yetu mpendwa aufahamu hiki kilio chetu cha muda mrefu zaidi ya miaka sita 6 ambacho tumekosa haki zetu tulizostahili kulipwa kutoka kwa aliekuwa muajiri wetu.
Ikiwemo haki ya malipo ya kujikim wakati tukisubiri kurudishwa maskani kwetu tulikotoka kwa muda miaka minne 4 pamoja na haki ya malipo utumishi kwa kipindi chote cha utumishi wetu.
Mhe rais mama yetu tumelazimika kutumia waandishi wa habari ili waweze kutufikishia kilio chetu kwako tukiamini wewe ndio mkombozi wetu wa kutuokoa na mateso tunayoyapia kwa muda mrefu wa kuhangaika kwenye ofisi mbalimbali za Wasaidizi wake bila kupata msaada zaidi ya kutupa majibu ambayo tunakosa haki zetu tuliozostahili kupata. Kimsingi tulistahili kulipwa posho ya kujikimu huku tukisubiri kurudishwa makwetu pamoja na malipo ya utumishi wetu.
JITIHADA TULIZOZIFANYA
Baada ya kulipwa nje ya muda tena kwa malipo pungufu tulimuandikia mwajiri wetu ambae ni Mamlaka ya Bandari kuomba stahiki ya Posho ya kujikimu muda tukisubiri malipo ya kurudishwa makwetu. Mwajiri alijibu na kukiri kuchelewesha kufanya malipo akisubiri maelekezo kutoka Serikalini Ofisi ya Utumishi wa Umma. Kwa barua yenye Kumb namba BA. 534/583/01-A/74 ya tarehe 20/OCT/2022 tunaambatanisha.
Baada ya majibu hayo kwa makundi tofauti tofauti tuliiandikia barua tume ya Utumishi wa Umma tukiomba haki zetu ambako nako tulipata majibu ya tume ikituelekeza kupeleka malalamiko yetu kwa Katibu Mkuu Utumishi wa Umma kwa barua yenye kumbu Na. CAD. 26/55/012/31-17/JAN/2023 tunaambanisha. Tulifanya hivyo kama tulivyoelekezwa na Tume.
Kumuandikia Katibu Mkuu utumishi wa Umma tunasikitishwa na majibu ya Katibu Mkuu kwa kusema hatulistahili kulipwa kwa sababu tulifukuzwa kazi kwa kosa la kujipatia ajira pasipokuwa na sifa stahik hali akijua sisi tuliombwa kuja kufanya kazi kutoka JKT na baadhi yetu tuliokuwa vibarua wa muda mrefu kuanzia miaka ya 1993 na kuendelia na baadae kupewa ajira.
Bila kuangalia madai ya msingi au kisheria katibu mkuu utumishi alitujibu kwa barua yenye kumbukumbu namba CA.271/313/01/A/36 ya 10/01/2025 tunaambanisha Katika jitihada za kuomba msaada wa kuomba haki yetu, tuliandika barua kwenda kwa Mhe. Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mama yetu mpendwa, kuomba msaada wa utatuzi wa swala letu.
Majibu ya awali kutoka kwa katibu mkuu kiongozi ambayo kwa barua yake hiyo alikiri kwa tunastahili kulipwa na alita vilelezo kutoka kwa muajiri wetu barua yenye kumbukumbu namba SBA.91/558/04B/33 ya 05/07/2024 naambatanisha.
Kwa masikitiko makubwa mara baada ya kupeleka vilelezo tulipata majibu yakwamba hatustahili kulipwa kwani tayari tumeshalipwa jambo ambalo tunaamini kwamba taarifa aliyopewa kutoka kwa muajiri wetu sio sahihi ya kwa tumelipwa stahiki zetu zote. Tunalazika kusema wasaidizi wako wanakuangusha au hawakusaidii kutenda haki kama vile wewe unavyotutendea wananchi wako.
Mama tunakupongeza kwa kazi iliyotukuka kwa watanzania, tunaamini kupitia wewe mama yetu mpendwa utatusaidia kupata haki yetu. Mama tumekuwa kunasikitishwa na hiki kinachofanywa na wasaidizi wako IKIWA TAASISI IMEOMBA WAFANYAKAZI KUTOKA TAASISI NYINGINE KABLA YA KUPEWA WALISHAPEWA SIFA ZAO NA WAO WAKASEMA WALETE TUNAWAHITAJI inakuwaje unakuja kumfukuza kazi kwa kumdharirisha? Tena unamnyima haki zake kwa madai alijipatia ajira huku ukijua wakati wa ajira yake hakufanya udanganyifu wowote.
Mhe. Rais tumekuwa tunapitia kipindi kigumu sana, kwani hadi hivi sasa bado tuko kwenye vituo vyetu vya kazi kwani nauli tuliopata ni ndogo kutokana na madeni ya kodi ya nyumba tulikuwa tumepangishiwa na bandari tulio wengi vitu vyetu vimezuiwa na wenye nyumba baada ya bandari kutolipa kodi huku tukisuburia kurudishwa makwetu.
Mhe. Rais kwa waliotokea JKT wamefanyakazi miaka kumi 10 na waliokuwa vibarua wa muda mrefu na kupewa ajira ni zaidi ya miaka hiyo unakuja kumfukuza kazi na kumlipa Tsh. 3,200/= kama stahiki zake hii kwetu imekuwa ni zaidi ya maumivu. Tunaamini kupia wewe mama yetu kipenzi cha watanzania tutapata msada wa kupata tumaini jipya kwenye maisha
Mhe Rais tunalazimika kusema wasaidizi wako wanakuangusha kwani baada ya kufukuzwa kazi aliekuwa muajiri wetu aliandika barua mara nyingi kwenda WIZARA YA UTUMISHI akiomba nafuu ya kurudishwa kazini kwa watumishi wa aina yetu darasa la saba, pamoja na watu wengine tisa 9 ambao walitoka kwa swala la vyeti. Kwa masikitiko makubwa kwa upande wetu WIZARA ilikataa kuturudisha kazini badala yake wakarudishwa kazini wale watu 9 ambao walitolewa kwa kosa la vyeti vya kugushi. Tumejaribu kufuatilia sehemu mbali mbali bila mafanikio
Ahsanteni Sana,
Imeandaliwa na
…………………………
MWENYEKITI WA KAMATI
Pia soma ~ Askari wa JKT tulioishia Darasa la 7 hatujalipwa stahiki zetu na TPA tangu tulipoachishwa kazi Mwaka 2018