Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Hongera sana Mnyika.
Wengi wana imani kubwa sana na wewe. Wewe ni kielelezo kizuri sana kwa vijana.
Keep it up.
Ushauri wangu wa haraka kwa ajili ya mafanikio yako ya kisiasa. NAJUA MENGI NINAYOSEMA HAPA UNAYAJUA NA PENGINE UNAYATEKELEZA HATA KWA ZAIDI LAKINI KUYASIKIA TENA KUTAKUPA KUYAIMARISHA.
1. Endelea na moyo wa kweli wa kutumikia watu - usirihusu uheshimiwa uingie moyoni. Jiite mtumishi moyoni na usikubali kulewa uheshimiwa.
2. Jilinde na suala la umaarufu. Umaarufu utatokea kwa wale wasioutafuta.Tafuta daima maslahi ya wengi.
3. Uwe mwangalifu na wanaokuzunguka tafuta wakweli wachache wakupe maoni na mtazamo wa kweli hata kama ni kukuonya uwe na watu hao, hao ni wazuri kuliko watakaokusifia kwa kila kitu huku pembeni wakikulaumu.
4. Pata nafasi kila wiki angalao mara moja ya kusoma kila kinachowezekana kwa habari za kimataifa.
5. Hakikisha kuwa unashiriki ibada kila wiki popote ulipo licha ya shughuli nyingi ulizo nazo ( kama ni Mkristo usiende kwenye nyumba moja tu au dini moja tu.) Nenda kwenye nyumba tofauti za ibada kila inapowezekana na sio lazima iwe ya dhehebu lako. Utajifunza mengi sana.
Wabunge wengi huanza kwenda kwenye nyumba za ibada wakati wa kampeni.
6. Anzisha sanduku lako la maoni jimboni mwako na hakikisha una mtu anayeyasoma na wananchi wako wajue kuwa kuna sanduku la maoni.
Utatukanwa katika maoni hayo, utalaumiwa, Usijali wala kuacha, kwani pia utaupata uwekli mwingi kuhusu hali halisi. Wape watu uhuru wa kutokuandika majina yao.
ASANTE SANA. HAYO TU. HAYA NINGEWEZA KUKUTUMIA BILA KUYAWEKA HAPA KAMA KUNGEKUWEPO NA EMAIL YAKO.
Wengi wana imani kubwa sana na wewe. Wewe ni kielelezo kizuri sana kwa vijana.
Keep it up.
Ushauri wangu wa haraka kwa ajili ya mafanikio yako ya kisiasa. NAJUA MENGI NINAYOSEMA HAPA UNAYAJUA NA PENGINE UNAYATEKELEZA HATA KWA ZAIDI LAKINI KUYASIKIA TENA KUTAKUPA KUYAIMARISHA.
1. Endelea na moyo wa kweli wa kutumikia watu - usirihusu uheshimiwa uingie moyoni. Jiite mtumishi moyoni na usikubali kulewa uheshimiwa.
2. Jilinde na suala la umaarufu. Umaarufu utatokea kwa wale wasioutafuta.Tafuta daima maslahi ya wengi.
3. Uwe mwangalifu na wanaokuzunguka tafuta wakweli wachache wakupe maoni na mtazamo wa kweli hata kama ni kukuonya uwe na watu hao, hao ni wazuri kuliko watakaokusifia kwa kila kitu huku pembeni wakikulaumu.
4. Pata nafasi kila wiki angalao mara moja ya kusoma kila kinachowezekana kwa habari za kimataifa.
5. Hakikisha kuwa unashiriki ibada kila wiki popote ulipo licha ya shughuli nyingi ulizo nazo ( kama ni Mkristo usiende kwenye nyumba moja tu au dini moja tu.) Nenda kwenye nyumba tofauti za ibada kila inapowezekana na sio lazima iwe ya dhehebu lako. Utajifunza mengi sana.
Wabunge wengi huanza kwenda kwenye nyumba za ibada wakati wa kampeni.
6. Anzisha sanduku lako la maoni jimboni mwako na hakikisha una mtu anayeyasoma na wananchi wako wajue kuwa kuna sanduku la maoni.
Utatukanwa katika maoni hayo, utalaumiwa, Usijali wala kuacha, kwani pia utaupata uwekli mwingi kuhusu hali halisi. Wape watu uhuru wa kutokuandika majina yao.
ASANTE SANA. HAYO TU. HAYA NINGEWEZA KUKUTUMIA BILA KUYAWEKA HAPA KAMA KUNGEKUWEPO NA EMAIL YAKO.