TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 24,873
- 11,253
na wewe taja jimbo lako watu waseme yaliyo ya moyoni bana....hongera sana mheshimiwa john mnyika. Ulipata ushindi mzuri na wa kujivunia na umeanza vizuri kazi uliyopewa. Mimi pia ni mmoja wa wakazi wa jimbo lako kwani nina makazi kimara na muda mwingi familia yangu inaishi huko, kwa hiyo wewe ni mbunge wangu na ninaona fahari kuwa na mbunge kijana, mbunifu, mwepesi na mchapakazi. Nitaangalia baadaye uwezekano wa kufahamiana na wewe kibinafsi ili kama lipo la kushirikiana na kushikana mikono, basi tufanye hivyo kwa manufaa ya wananchi wakazi wa eneo letu na taifa kwa ujumla.
Nakutakia kila la heri katika utumishi wako. Mungu akutangulie na daima maslahi ya taifa yakae mbele
mungu ibariki tanzania,
mungu ibariki afrika
kidumu chama cha mapinduzi